Kitabu: Jasusi Komando (based on a true story)

Kudo

JF-Expert Member
Nov 2, 2017
1,809
6,081
RIWAYA: JASUSI KOMANDO

NA; BAHATI MWAMBA.

SIMU: 0758573660

1.

BERBERA, SOMALIA (Somaliland).

Alivuta pumzi zake kwa kasi kisha,alizishusha taratibu huku akiwa amefumba macho yake na kichwa chake akiwa amekiinamishia mbele kiasi, kidevu chake kiliegama kifuani mwake.

Zoezi lile alikuwa amesharirudia zaidi ya mara nne. Mara ya tano lilianza kuvuna matunda alioyatarajia. Alilegeza mwili wake, kisha alifumba macho na kubana pumzi. Masikio yake, yalibaki kusikia namna mapigo ya moyo, yalivyopishana kila baada ya sekunde moja.

Mikono yake iliofungwa nyuma ya kiti alichokalia, haikumpa hali ya maumivu tena, makovu yaliojiwekea makazi kwenye mwili wake,hayakuwa kitisho tena, hata joto kali liloletwa na taa iliofungwa sentimita chache kutoka kichwani kwake na kuwaka muda wote na, kumletea joto utosini kwake, hakusikia tena adha ile.

Mawazo yake yalisafiri hatua nyingi kutoka alipo. Mwili wake haukufanya kazi yoyote zaidi ya kuacha akili ipokee hatua nyingine ya mwanadamu; hatua ambayo, binadamu wengi hawaifikii na hawajui kama wanaouwezo wa kufika hatua hiyo.

Bwana huyu alikuwa anafanya tahajudi; tahajudi ya tiba. Aliona ni wakati muafaka kufanya tahajudi ya tiba, baadaa ya kupitia misukosuko kwa siku kadhaa, ambazo hakujua idadi yake. Hakuwa anajua usahihi wa siku alizopitia mateso na shuruba kubwa, shuruba za kupigwa na kugombaniwa na makundi ya wapiganaji ndani ya nchi ya Somalia yenye vinchi vingi ndani ya ardhi moja.

Alifanya tahajudi kwa kuwa alihisi kifuani mwake kumejaa rundo la vumbi, damu nayo haikutembea vyema mwilini mwake na, akili yake, ilikuwa nzito isioweza kufikiri vyema. Tahajudi ilikuwa ni tiba tosha katikati ya wanadamu wenye roho mbaya, wanadamu ambao hawajali machozi ya wenzao.

Licha ya kumtesa sana, lakini hakuna alieshauri apelekwe kwenye matibabu ili kumweka sawa kiafya, hivyo aliona ni vyema kufanya tahajudi ya tiba kisha atajua cha kufanya baada ya matokeo ya zoezi lake.

Akiwa bado ameyafumba macho yake, akili yake ilishirikiana na mlango mmoja wa fahamu, kisha aligundua kulikuwa na mtu karibu na chumba alichofungiwa.

Haraka aliamua kulisitisha zoezi lake. Alishusha pumzi nyingi kisha alifumbua macho yake na kufanya moyo wake udunde kwa shangwe ya kupunguziwa uzito kwa tahajudi.

Aliendelea kutulia na kumngojea mtu aliemsikia akitembea nje ya chumba alichokuwamo. Ngojeo lake lilimkutanisha na mtu aliemtegemea kuingia katika chumba kile kwa wakati kama huo.

Mtu yule alikuwa amebeba sinia la chakula, kiunoni mwake alikuwa na bastola asiopenda kuiacha mara zote aingiapo chumbani mle.

Mtu yule alimtizama kwa tuo kana kwamba ilikuwa ni siku ya kwanza kukutana.

“Leo umeletewa nyama ya kuku, hii si ishara nzuri kwako!” Alizungumza mtu yule, huku akiweka chini sinia lililosheheni nyama ya kuku na ugali mkubwa.

“Tunajua wewe ni mtanzania, na huitwi Rebu, bali unaitwa Obimbo Mtei” Alisema tena mtu yule, huku akishika kiuononi mwake kwa mikono yote miwili.

Obimbo Mtei aliekuwa amefungwa kitini, alimtizama bwana yule. Maneno yake yalimwingia vyema, lakini hakushituka. Alijua ni lazima watu wale wangelijua utambulisho wake sahihi licha ya kuukana mara kadhaa mbele yao.

“Sasa kwa nini unanambia haya?” Obi alimuuliza mtu yule.
“Kwa sababu nchi yako imekana kukujua hivyo kuendelea kukaa na wewe hapa, ni kujiletea hasara na hatari zisizo takiwa!”

“Lakini tangu mwanzo niliwambieni mimi si mtanzania, natokea Lilongwe Malawi na siko hapa kwa ujasusi, bali nafanya kazi na shirika lisilo la kiserikali.” Obi alimwambia mtu yule, huku macho yake yakikitizama chakula kilichokuwa kando ya miguu yake.

Njaa ilimuuma lakini alijizuia kuomba kufunguliwa ili ale chakula kile. Hisia zilimtuma vibaya juu ya chakula kile, hakujua ni kwanini lakini alisita kabisa kukifurahia. Akili yake ilikuwa inafanya kazi kubwa kuamua la kufanya juu ya chakula kile.

Alikitizama kwa tuo, aligundua kimepikwa kiswahili,kimepikwa na mpishi anaejua aina ya vyakula vya Tanzania. Alijua kuna kitu hakiko sawa juu ya matayarisho ya chakula kile na, alijua wanamtega ili kuujua utaifa wake ambao amekuwa akiukana tangu aingie mikononi mwa watu wale.

“Mimi bado ni lulu kwa hawa jamaa, hawawezi kuniua, wanataka hakika ya utaifa wangu….” Obi alijiwazia.

“Vipi rafiki, huhitaji kufunguliwa ili ule?” Aliuliza bwana yule alieleta chakula, ambae wakati wote alikuwa akimtizama Obi bila kusema kitu.
“Umekuwa ukifanya hivyo kila siku, fanya sasa ili nihudumie tumbo langu”

Baada ya kujibiwa, bwana yule alimfungua kamba za mikono, kisha aliondoka ndani ya chumba kile.

Obimbo Mtei alikiinamia chakula kile na alipotaka kumega alisita, alilegeza mwili wake kisha alitulia. Alihisi kuna mtu anamtizama, haraka aligeuka na kukutanisha macho na mtu aliekileta chakula. Mtu yule alikuwa amesimama mlangoni na ameelekeza macho yake kwa Obi.

“huu ni mtego!!” Obi alijiwazia kisha alianza kuumega ugali na, aliumega tofauti na matarajio ya mtu aliekuwa akimtizama.

Obi aligundua mtego wake upo kwenye umegaji wa ugali; kawaida waswahili wengi hawamegi ugali kuanzia juu, humega ugali chini kabisa kiupande. Lakini mataifa mengi ya Afrika, watu humega ugali vile watakavyo. Obi alitegua mtego ule kirahisi sana na nyuma yake alisikia mlango ukifungwa.

Obi alikula harakaharaka, kuna kitu alitaka kukifanya kabla ya muda wa kufungwa haujawadia; muda ambao ni dakika saba tu baada ya kupewa chakula.

Kwa makadirio yake alikuwa ametumia dakika tatu kumaliza chakula, alisimama haraka na kukichukua kijiko kilichokuwa chini ya kiti alichokuwa akifungiwa. Alinyata kwa kutumia ncha za vidole vyake. Alifika mlangoni na kukitazama kitasa cha mlango, kitasa ambacho vishikio vyake(bolt), vilizingwa na kutu kiasi. Obi alilichukulia lile ni kosa la watu waliomteka, pengine walijua na kupuuzia au hawakujua kabisa.

Obi alitumia kijiko kulegeza vishikio vile na, ndani ya dakika tatu, alikuwa amelegeza nati tatu na kubakiza moja ambayo alikuwa ameshailegeza tangu alipogondua udhaifu wa mlango ule.

****

Mleta chakula alirejea akiwa ameongozana na mtu mwingine aliekuwa na bunduki ya kivita aina ya AK 47. Watu hawa ilikuwa ni kawaida yao kushirikiana kumfunga kwenye kiti na kumwacha pale kila siku. Lakini kitu kimoja hawakujua, ni mipango ya Obi juu yao. Obi hakutaka kulala tena ndani ya kambi ile ya wanamgambo wa Hizbul Islam.

Walipomaliza kumfunga na kutoka, Obi alirudia zoezi lake la tahajudi, lakini wakati huu hakufanya tahajudi ya afya, alifanya tahajudi ya hisia na nguvu za ziada. Alifumba macho na kutulia tuli.
Tahajudi ilimletea matokeo alioyatarajia, alisikia maji yakimwagika sehemu na aligundua ni mkondo wa maji umepita chini ya nyumba ile aliohifdhiwa.

Alifumbua macho yake na kushusha pumzi nyingi. Aligundua eneo alilofungwa.
Kulingana na ramani ya nchi ya Somalia, ni mji mmoja tu ulio na miundombinu ya mikondo ya kumwaga maji machafu baharini na mji huo ni Berbera, kaskazini mwa Mogadishu na kusini mwa guba ya Aden.

Obi aliguna kisha alijiangusha chini na kiti chake na kutulia. Hakutgemea kuwaona walinzi wakiingia ndani ya chumba kile, kwa sababu alishafanya mazoezi ya sauti ya kishindo na kugundua ni sauti kiasi gani inaweza kuwakurupua na kuja ndani ya chumba kile.

Zoezi hilo alilifanya kwa kupiga komeo la mlango na kijiko kila alipoletewa chakula, hivyo alipojiangusha chini, alikadiria kishindo ambacho kisingeweza kuwagutua walinzi waliokuwa kando ya mlango.

Obi alipodondoka chini, alifanya jitahada na kukifikia kijiko kwa kujiburuza na kiti chake, kisha alianza kuzikata kamba kwa kutumia kijiko.
Ilimchukua dakika thelathini kufanikiwa kuzikata kamba. Hatimae mikono yake ikawa huru na alijifungua kamba za miguuni mwake na kusimama wima.
Aliifuata taa iliokuwa inawaka,aliinyofoa na kufanya giza libebe nafasi ndani ya chumba kile.

Hakuwa na viatu miguuni mwake, hiyo ilikuwa ni faida kwake kwa kuwa aliweza kutembea ndani ya chumba bila hatua zake kusikiwa na mtu aliekuwa karibu na chumba.

Heka heka alizozoea kuzisikia, taratibu zilianza kupungua na hiyo ilikuwa ni ishara nzuri kwake, maana alijua huo ni usiku na watu wengi kwenye nyumba ile hupumzika na kuwaacha walinzi watatu wakilinda chumba alichokuwemo na, walinzi wale hulala fofofo katikati ya usiku mkubwa na alijua ni sauti kiasi gani ingesikiwa na walinzi wale katikati ya usingizi wao, hivyo alijua atumie sauti gani ili asiwaamshe wakati wa kutoroka.

****

Hatimae muda ambao aliutarajia ulifika. Tayari alikuwa amefanikiwa kuhamisha mfumo wa kitasa na mlango ulikubali kufunguka.

Aliuvuta taratibu bila kelele, kisha alinyata na kutoka nje ya chumba na kujikuta kwenye korido pana na kando ya mlango kulikuwa na walinzi watatu wakiwa wamelala kwenye viti na silaha zao.

Aliwatizma kwa haraka haraka na kumuona mmoja akiwa amening’iza rundo la funguo kwenye suruali njiwa aliovaa.

Obi alinyata na kumfikia, kisha alianza kumpuliza shingoni na upepo wa mahaba. Hii ilikuwa ni mbinu ya kiueledi wanayofundishwa makomando wawapo mazoezini na huaminika upepo shingoni humzidishia mtu kilele cha usingizi na kumfanya mzito kuamka.

Obi alichomoa funguo na kuanza kuanza kutoka kwenye ile korido na kuafuata upande ambao aliamini hakukosekani jiko. Alihitaji kutoroka kwa kutumia upande wa jiko, ambako aliamini kuna chemba ya kumpitisha kwenye mkondo wa maji machafu.
Nyumba nyingi za Berbera zimejengwa kwa mfumo huo na ni kwa sababu ni mji uliokaliwa na waingereza na kuugeuza eneo la kijeshi.

Obi alitaka atoroke bila tafrani, maana hakuwa na nguvu za kutosha na mwili wake ulikuwa dhaifu, kashikashi yoyote asingeweza kukabiliana nayo

NB: RIWAYA HII NI KITABU NA KINATOKA RASMI, KATIKATI YA MWEZI WA 11 MWAKA HUU.

BEI YAKE NI TSH 10,000/=

KITABU HIKI SI CHA KUKIKOSA KWENYE MAKTABA YAKO....

WEKA ODA YAKO SASA KWA KUWASILIANA NA MWANDISHI KWA NAMBA; 0758573660.

KUMBUKA: KITABU HIKI KINATOKA KWA ODA MAALUMU, HIVYO ODA YAKO ITAKUKUTANISHA NA KITABU HIKI MAPEMA KABISA.

KARIBU.
 
RIWAYA HII NI KITABU NA KINATOKA RASMI, KATIKATI YA MWEZI WA 11 MWAKA HUU.

BEI YAKE NI TSH 10,000/=

KITABU HIKI SI CHA KUKIKOSA KWENYE MAKTABA YAKO....

WEKA ODA YAKO SASA KWA KUWASILIANA NA MWANDISHI KWA NAMBA; 0758573660.

KUMBUKA..KITABU HIKI KINATOKA KWA ODA MAALUMU, HIVYO ODA YAKO ITAKUKUTANISHA NA KITABU HIKI MAPEMA KABISA.

KARIBU.
 
RIWAYA; JASUSI, KOMANDO.

NA; BAHATI MWAMBA.

SIMU; 0758573660.

1.

BERBERA SOMALIA (Somaliland).

Alivuta pumzi zake kwa kasi kisha,alizishusha taratibu huku akiwa amefumba macho yake na kichwa chake akiwa amekiinamishia mbele kiasi, kidevu chake kiliegama kifuani mwake.

Zoezi lile alikuwa amesharirudia zaidi ya mara nne. Mara ya tano lilianza kuvuna matunda alioyatarajia. Alilegeza mwili wake, kisha alifumba macho na kubana pumzi. Masikio yake, yalibaki kusikia namna mapigo ya moyo, yalivyopishana kila baada ya sekunde moja.

Mikono yake iliofungwa nyuma ya kiti alichokalia, haikumpa hali ya maumivu tena, makovu yaliojiwekea makazi kwenye mwili wake,hayakuwa kitisho tena, hata joto kali liloletwa na taa iliofungwa sentimita chache kutoka kichwani kwake na kuwaka muda wote na, kumletea joto utosini kwake, hakusikia tena adha ile.

Mawazo yake yalisafiri hatua nyingi kutoka alipo. Mwili wake haukufanya kazi yoyote zaidi ya kuacha akili ipokee hatua nyingine ya mwanadamu; hatua ambayo, binadamu wengi hawaifikii na hawajui kama wanaouwezo wa kufika hatua hiyo.

Bwana huyu alikuwa anafanya tahajudi; tahajudi ya tiba. Aliona ni wakati muafaka kufanya tahajudi ya tiba, baadaa ya kupitia misukosuko kwa siku kadhaa, ambazo hakujua idadi yake. Hakuwa anajua usahihi wa siku alizopitia mateso na shuruba kubwa, shuruba za kupigwa na kugombaniwa na makundi ya wapiganaji ndani ya nchi ya Somalia yenye vinchi vingi ndani ya ardhi moja.

Alifanya tahajudi kwa kuwa alihisi kifuani mwake kumejaa rundo la vumbi, damu nayo haikutembea vyema mwilini mwake na, akili yake, ilikuwa nzito isioweza kufikiri vyema. Tahajudi ilikuwa ni tiba tosha katikati ya wanadamu wenye roho mbaya, wanadamu ambao hawajali machozi ya wenzao.

Licha ya kumtesa sana, lakini hakuna alieshauri apelekwe kwenye matibabu ili kumweka sawa kiafya, hivyo aliona ni vyema kufanya tahajudi ya tiba kisha atajua cha kufanya baada ya matokeo ya zoezi lake.

Akiwa bado ameyafumba macho yake, akili yake ilishirikiana na mlango mmoja wa fahamu, kisha aligundua kulikuwa na mtu karibu na chumba alichofungiwa.

Haraka aliamua kulisitisha zoezi lake. Alishusha pumzi nyingi kisha alifumbua macho yake na kufanya moyo wake udunde kwa shangwe ya kupunguziwa uzito kwa tahajudi.

Aliendelea kutulia na kumngojea mtu aliemsikia akitembea nje ya chumba alichokuwamo. Ngojeo lake lilimkutanisha na mtu aliemtegemea kuingia katika chumba kile kwa wakati kama huo.

Mtu yule alikuwa amebeba sinia la chakula, kiunoni mwake alikuwa na bastola asiopenda kuiacha mara zote aingiapo chumbani mle.

Mtu yule alimtizama kwa tuo kana kwamba ilikuwa ni siku ya kwanza kukutana.

“Leo umeletewa nyama ya kuku, hii si ishara nzuri kwako!” Alizungumza mtu yule, huku akiweka chini sinia lililosheheni nyama ya kuku na ugali mkubwa.

“Tunajua wewe ni mtanzania, na huitwi Rebu, bali unaitwa Obimbo Mtei” Alisema tena mtu yule, huku akishika kiuononi mwake kwa mikono yote miwili.

Obimbo Mtei aliekuwa amefungwa kitini, alimtizama bwana yule. Maneno yake yalimwingia vyema, lakini hakushituka. Alijua ni lazima watu wale wangelijua utambulisho wake sahihi licha ya kuukana mara kadhaa mbele yao.

“Sasa kwa nini unanambia haya?” Obi alimuuliza mtu yule.
“Kwa sababu nchi yako imekana kukujua hivyo kuendelea kukaa na wewe hapa, ni kujiletea hasara na hatari zisizo takiwa!”

“Lakini tangu mwanzo niliwambieni mimi si mtanzania, natokea Lilongwe Malawi na siko hapa kwa ujasusi, bali nafanya kazi na shirika lisilo la kiserikali.” Obi alimwambia mtu yule, huku macho yake yakikitizama chakula kilichokuwa kando ya miguu yake.

Njaa ilimuuma lakini alijizuia kuomba kufunguliwa ili ale chakula kile. Hisia zilimtuma vibaya juu ya chakula kile, hakujua ni kwanini lakini alisita kabisa kukifurahia. Akili yake ilikuwa inafanya kazi kubwa kuamua la kufanya juu ya chakula kile.

Alikitizama kwa tuo, aligundua kimepikwa kiswahili,kimepikwa na mpishi anaejua aina ya vyakula vya Tanzania. Alijua kuna kitu hakiko sawa juu ya matayarisho ya chakula kile na, alijua wanamtega ili kuujua utaifa wake ambao amekuwa akiukana tangu aingie mikononi mwa watu wale.

“Mimi bado ni lulu kwa hawa jamaa, hawawezi kuniua, wanataka hakika ya utaifa wangu….” Obi alijiwazia.

“Vipi rafiki, huhitaji kufunguliwa ili ule?” Aliuliza bwana yule alieleta chakula, ambae wakati wote alikuwa akimtizama Obi bila kusema kitu.
“Umekuwa ukifanya hivyo kila siku, fanya sasa ili nihudumie tumbo langu”

Baada ya kujibiwa, bwana yule alimfungua kamba za mikono, kisha aliondoka ndani ya chumba kile.

Obimbo Mtei alikiinamia chakula kile na alipotaka kumega alisita, alilegeza mwili wake kisha alitulia. Alihisi kuna mtu anamtizama, haraka aligeuka na kukutanisha macho na mtu aliekileta chakula. Mtu yule alikuwa amesimama mlangoni na ameelekeza macho yake kwa Obi.

“huu ni mtego!!” Obi alijiwazia kisha alianza kuumega ugali na, aliumega tofauti na matarajio ya mtu aliekuwa akimtizama.

Obi aligundua mtego wake upo kwenye umegaji wa ugali; kawaida waswahili wengi hawamegi ugali kuanzia juu, humega ugali chini kabisa kiupande. Lakini mataifa mengi ya Afrika, watu humega ugali vile watakavyo. Obi alitegua mtego ule kirahisi sana na nyuma yake alisikia mlango ukifungwa.

Obi alikula harakaharaka, kuna kitu alitaka kukifanya kabla ya muda wa kufungwa haujawadia; muda ambao ni dakika saba tu baada ya kupewa chakula.

Kwa makadirio yake alikuwa ametumia dakika tatu kumaliza chakula, alisimama haraka na kukichukua kijiko kilichokuwa chini ya kiti alichokuwa akifungiwa. Alinyata kwa kutumia ncha za vidole vyake. Alifika mlangoni na kukitazama kitasa cha mlango, kitasa ambacho vishikio vyake(bolt), vilizingwa na kutu kiasi. Obi alilichukulia lile ni kosa la watu waliomteka, pengine walijua na kupuuzia au hawakujua kabisa.

Obi alitumia kijiko kulegeza vishikio vile na, ndani ya dakika tatu, alikuwa amelegeza nati tatu na kubakiza moja ambayo alikuwa ameshailegeza tangu alipogondua udhaifu wa mlango ule.

****

Mleta chakula alirejea akiwa ameongozana na mtu mwingine aliekuwa na bunduki ya kivita aina ya AK 47. Watu hawa ilikuwa ni kawaida yao kushirikiana kumfunga kwenye kiti na kumwacha pale kila siku. Lakini kitu kimoja hawakujua, ni mipango ya Obi juu yao. Obi hakutaka kulala tena ndani ya kambi ile ya wanamgambo wa Hizbul Islam.

Walipomaliza kumfunga na kutoka, Obi alirudia zoezi lake la tahajudi, lakini wakati huu hakufanya tahajudi ya afya, alifanya tahajudi ya hisia na nguvu za ziada. Alifumba macho na kutulia tuli.
Tahajudi ilimletea matokeo alioyatarajia, alisikia maji yakimwagika sehemu na aligundua ni mkondo wa maji umepita chini ya nyumba ile aliohifdhiwa.

Alifumbua macho yake na kushusha pumzi nyingi. Aligundua eneo alilofungwa.
Kulingana na ramani ya nchi ya Somalia, ni mji mmoja tu ulio na miundombinu ya mikondo ya kumwaga maji machafu baharini na mji huo ni Berbera, kaskazini mwa Mogadishu na kusini mwa guba ya Aden.

Obi aliguna kisha alijiangusha chini na kiti chake na kutulia. Hakutgemea kuwaona walinzi wakiingia ndani ya chumba kile, kwa sababu alishafanya mazoezi ya sauti ya kishindo na kugundua ni sauti kiasi gani inaweza kuwakurupua na kuja ndani ya chumba kile.

Zoezi hilo alilifanya kwa kupiga komeo la mlango na kijiko kila alipoletewa chakula, hivyo alipojiangusha chini, alikadiria kishindo ambacho kisingeweza kuwagutua walinzi waliokuwa kando ya mlango.

Obi alipodondoka chini, alifanya jitahada na kukifikia kijiko kwa kujiburuza na kiti chake, kisha alianza kuzikata kamba kwa kutumia kijiko.
Ilimchukua dakika thelathini kufanikiwa kuzikata kamba. Hatimae mikono yake ikawa huru na alijifungua kamba za miguuni mwake na kusimama wima.
Aliifuata taa iliokuwa inawaka,aliinyofoa na kufanya giza libebe nafasi ndani ya chumba kile.

Hakuwa na viatu miguuni mwake, hiyo ilikuwa ni faida kwake kwa kuwa aliweza kutembea ndani ya chumba bila hatua zake kusikiwa na mtu aliekuwa karibu na chumba.

Heka heka alizozoea kuzisikia, taratibu zilianza kupungua na hiyo ilikuwa ni ishara nzuri kwake, maana alijua huo ni usiku na watu wengi kwenye nyumba ile hupumzika na kuwaacha walinzi watatu wakilinda chumba alichokuwemo na, walinzi wale hulala fofofo katikati ya usiku mkubwa na alijua ni sauti kiasi gani ingesikiwa na walinzi wale katikati ya usingizi wao, hivyo alijua atumie sauti gani ili asiwaamshe wakati wa kutoroka.

****

Hatimae muda ambao aliutarajia ulifika. Tayari alikuwa amefanikiwa kuhamisha mfumo wa kitasa na mlango ulikubali kufunguka.

Aliuvuta taratibu bila kelele, kisha alinyata na kutoka nje ya chumba na kujikuta kwenye korido pana na kando ya mlango kulikuwa na walinzi watatu wakiwa wamelala kwenye viti na silaha zao.

Aliwatizma kwa haraka haraka na kumuona mmoja akiwa amening’iza rundo la funguo kwenye suruali njiwa aliovaa.

Obi alinyata na kumfikia, kisha alianza kumpuliza shingoni na upepo wa mahaba. Hii ilikuwa ni mbinu ya kiueledi wanayofundishwa makomando wawapo mazoezini na huaminika upepo shingoni humzidishia mtu kilele cha usingizi na kumfanya mzito kuamka.

Obi alichomoa funguo na kuanza kuanza kutoka kwenye ile korido na kuafuata upande ambao aliamini hakukosekani jiko. Alihitaji kutoroka kwa kutumia upande wa jiko, ambako aliamini kuna chemba ya kumpitisha kwenye mkondo wa maji machafu.
Nyumba nyingi za Berbera zimejengwa kwa mfumo huo na ni kwa sababu ni mji uliokaliwa na waingereza na kuugeuza eneo la kijeshi.

Obi alitaka atoroke bila tafrani, maana hakuwa na nguvu za kutosha na mwili wake ulikuwa dhaifu, kashikashi yoyote asingeweza kukabiliana nayo

NB; RIWAYA HII NI KITABU NA KINATOKA RASMI, KATIKATI YA MWEZI WA 11 MWAKA HUU.

BEI YAKE NI TSH 10,000/=

KITABU HIKI SI CHA KUKIKOSA KWENYE MAKTABA YAKO....

WEKA ODA YAKO SASA KWA KUWASILIANA NA MWANDISHI KWA NAMBA; 0758573660.

KUMBUKA..KITABU HIKI KINATOKA KWA ODA MAALUMU, HIVYO ODA YAKO ITAKUKUTANISHA NA KITABU HIKI MAPEMA KABISA.

KARIBU.
Soft copy yake kiasi gani mkubwa
 
RIWAYA; KOMANDO, JASUSI.

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660.


SEHEMU YA PILI

Aliwatizma kwa haraka haraka na kumuona mmoja akiwa amening’iza rundo la funguo kwenye suruali njiwa aliovaa.

Obi alinyata na kumfikia, kisha alianza kumpuliza shingoni na upepo wa mahaba. Hii ilikuwa ni mbinu ya kiueledi wanayofundishwa makomando wawapo mazoezini na huaminika upepo shingoni humzidishia mtu kilele cha usingizi na kumfanya mzito kuamka.

Obi alichomoa funguo na kuanza kuanza kutoka kwenye ile korido na kuafuata upande ambao aliamini hakukosekani jiko. Alihitaji kutoroka kwa kutumia upande wa jiko, ambako aliamini kuna chemba ya kumpitisha kwenye mkondo wa maji machafu.
Nyumba nyingi za Berbera zimejengwa kwa mfumo huo na ni kwa sababu ni mji uliokaliwa na waingereza na kuugeuza eneo la kijeshi.

Obi alitaka atoroke bila tafrani, maana hakuwa na nguvu za kutosha na mwili wake ulikuwa dhaifu, kashikashi yoyote asingeweza kukabiliana nayo.

Alitembea kwenye korido ile ndefu, hadi alipoona chumba kimoja kikiwa wazi upande wa kushoto mwa korido ile.
Obi alitizama nyuma yake kisha alitizama mbele na hakuona dalili ya kuwapo walinzi wengine waliokuwa macho.
Hakujua ni kwa nini kulikuwa na ulinzi dhaifu kwenye nyumba ile iliokuwa imejengwa kama madarasa ya shule.

Obi hakutaka kupoteza muda kwa kuuwaza ulinzi ambao ulimfanikisha yeye kufika hapo alipokuwa.
Aliingia ndani ya chumba kile kwa kunyata, alikutana na mwanga wa taa ukimulika kwenye kile chumba, macho yake yalisafiri kwa kasi na kujaribu kuangaza kila pande ya chumba kile. Hakuona mtu na bahati ilibaki upande wake, kwa sababu kile chumba kilitumika kama jiko.
Obi alijitosa ndani yake, kisha aliweka sikio lake sakafuni na kusikiliza.

Kwa mbali alisikia mjongeo wa maji na hiyo ilikuwa ni ishara nzuri kwake. Alisimama na kusogelea dirisha dogo lililokuwa kwenye chumba kile, dirisha ambalo lilijengwa maalumu kwa kupitisha moshi.

Macho yake yaliona upande wa pili wa nyumba aliokuwa amefungiwa wakati wote aliokuwa pale; kulikuwa na nyumba nyingine zilizokuwa zimejengwa mfano wa kota za watumishi wa serikali na kutoka kwenye nyumba zile hadi kwenye nyumba aliokuwemo, kulikuwa na utenganisho wa uwanja mpana. Upande ule pia, aliona walinzi waliovalia suruali njiwa na viremba vichwani mwao. Walinzi wale walikuwa wanaranda huku na huko kuhikisha usalama wakati wote.

Obi alijipongeza kwa maamuzi yake ya kutotumia nguvu kubwa kujitoa mateka. Angelitumia nguvu, asingefika popote.

Alitoka pale dirishani na kuanza kuangaza kila pande ya chumba kile na, kona moja aliona pipa la maji likiwa limeegeshwa juu ya kitu. Alisogea na kuinama kuangalia ni kitu gani kilichotumika kulibeba pipa lile kubwa. Alikutana na mfuniko wa chuma na, alielewa mfuniko ule ulifunika nini. Haraka alianza kulisogeza pipa lile ambalo halikujaa maji.
Dakika mbili zilitosha kulisogeza pembeni na kubaki akitazamana na mfuniko wa chemba ya maji machafu na sasa aliweza kusikia sauti ya maji yakitiririka.

Alitoa funguo alizoshika na kuanza kufungua kufuli lilokuwa limefungwa pale.
Funguo ya kwanza haikufungua, lakini funguo ya pili ilifungua, nae hakufanya ajizi alifungua chemba ile na kutizama kwa chini. Pua zake zilipokea na harufu kali ya uvundo wa maji yale yaliobeba uchafu wote wa mji wa Berbera.
Hakujali!!.

Alijitosa ndani yake na kukutana na ngazi nyembamba za chuma. Alihitaji kufanya jambo kabla hajashuka chini hadi kwenye ule mkondo wa maji machafu. Alisimama kwenye ngazi, kisha alishika mfuniko wa chemba na kujifunikia ndani ya chemba na alitumia kufuli alilolikuta na kufunga kwa ndani, kisha funguo alizitupa ndani ya maji.

Baada ya zoezi lile, taratibu alianza kushuka kwa umakini mkubwa, hakutaka kuamini uimara wa ngazi.
Tofauti na matarajio yake, ngazi haikumfikisha kwenye kina cha maji machafu, bali, ngazi zilichukua uelekeo mwingine kwa kuingia kwenye chemba nyingine iliokuwa imetengenezwa kwa kutumia bomba kubwa Japo haikumuwezesha kusimama na ilihitaji kutambaa. Bado aliendelea kumshukuru Mungu kwa kumuongoza katika njia zilizo salama zaidi.

Alitambaa umbali wa mita mia moja, pua zake zilinasa harufu kali ya uozo wa kiumbe,lakini haukuwa uozo tu, bali kulikuwa na uozo uliochanganyikana na harufu ya mkojo wa kiumbe hai.

Giza lilimfanya atulie ili kujua usalama wa njia anayoenda kupita, dhahiri mbele yake kulikuwa na mzoga na mzoga huo ulikuwa unadondokewa na mkojo wa kiumbe hai.
Kiumbe gani? Hakukijua.

Obimbo mtei aliendelea kutulia alipokuwa. Alilala kifudifudi na kunyoosha mikono yake mbele, kidevu chake alikilaza chini na macho yake aliyaelekeza mbele mita kadhaa. Alihitaji kuendelea kulizoea giza ili walau aweze kuona kilichokuwa mbele yake.

Akiwa ametulia huku akihema taratibu, juu ya mgongo wake alihisi kuna kiumbe anatembea na kudondosha udongo. Hapo akili yake ilimwambia ni lazima kutakuwa na mpasuko wa lile bomba kiasi kuliweza kudondosha udongo na kuruhusu kiumbe kupita bila kuteleza.
Mjongeo wa kiumbe yule, ulimpa shaka Obimbo Mtei. Alihisi kiumbe yule nae alikuwa mawindoni na yawezekana ni yeye aliekuwa windo.

Lakini ni kiumbe gani sasa anaemwinda?

Jibu halikukawia, kiumbe aliekuwa juu ya mgongo wake alijifyatua kwa kasi na kudondoka kando ya mikono yake kisha ilifuatia sauti kali ya kilio cha uchungu na maumivu.

Alikuwa ni nyoka aliefanikiwa kumwinda panya.
Obi alimeza funda la mate kwa ahueni.

Aliamua kurudi nyuma kidogo ili kumpisha nyoka afurahie windo lake, huku yeye akipanga namna ya kupishana na nyoka yule bila kudhuriwa.

Kwa kawaida nyoka wenye viini kwenye macho, hupenda kuishi kwenye mapango na kuwinda nyakati za usiku na nyoka hawa, huwa na vichwa mithili ya pembe tatu na wana meno marefu yaliopinda kwa mbele. Nyoka hawa ni wenye sumu kali, pia ni nyoka wenye visasi na hawapendi bugudha kutoka kwa binadamu. Wanakasi ya matendo na mwendo, sumu yao inachukua uhai wa binadamu ndani ya dakika ishirini tu.

Ukikutana nao, tulia bila kutikisika, ondoa hofu na legeza mwili, kwa sababu hofu yako, kwao huhisi ni hatari kubwa na ili wajihami na hatari hiyo, huamua kushambulia.

Obi alitulia tuli akingoja nyoka yule amalize kazi yake na kujiondokea.

Wakati akisubiri zoezi lile likamilike, mawazoni mwake alijichulia yeye ndie panya, asipofanya jitihada basi, aweza kufa akiwa ndani ya Somalia. Hakutaka kuwa panya tena anaewindwa, alitaka kuwa mwindaji anaewinda na kuwindwa na hakuhitaji kuwa anaewindwa peke yake.

********

Mawazo yake yalikatishwa na sauti ya mbawa nyingi na milio ya kuogofya,kisha alisikia mtatariko wa kiumbe mbele yake.

Obi alijawa na hofu, kisha aliamua kuchukua maamuzi ya haraka kujilaza kiubavu huku akiwa amenyoosha mikono yake mbele na hakutaka kutikisika.

Bado masikio yake yaliendelea kuumizwa na sauti kali ya milio ya popo; popo ambao walikuwa wanamshambulia nyoka aliekuwa kwenye himaya yao.
Kwa uzoefu wa Obi, alijua wale ni popo wanaokula nyama na ni ngumu yule nyoka kupona, kwa sababu alikuwa na windo mdomoni na kwa wingi wa popo wale hata angelijaribu kutema, bado asingeliweza kutoka salama.

Kuharibiwa kwa starehe ya nyoka na windo lake, kuliibua wazo jipya kichwani mwa Obi. Alikumbuka namna alivyoharibiwa ratiba yake pale Mogadishu siku kadhaa huko nyuma na kujikuta ndani ya mikono ya makundi ya wapiganaji,kisha kusafirishwa hadi Berbera bila kujua.

Ujio wake ndani ya Somalia ulikuwa wa siri sana, lakini alishangaa namna adui walivyopata habari na kumkamata kama kuku akiwa hotelini. Lakini hilo la kukamatwa lisingeweza kumpa shida sana. Alipata shida kwa kuwa, waliomkamata walikagua begi lake la nguo na kukuta kitambulisho chake cha bima ya afya.

Kumbukumbu zake zilimwambia, hakuwa amekiweka kitambulisho kile kwenye begi lake na kamwe hakuwahi kufanya kosa kwenye safari za siri kama hizo.

Alijiuliza kilifikaje kwenye begi na hakukiweka?

Kuna mtu alifanya vile, ni nani sasa!

Obi alipumua taratibu hakuwa amepata jibu la swali lile tangu siku anakamatwa na kuwekwa mikononi mwa wahuni wale wa Somalia. Mtu aliemuuza alimfananisha na popo wale walioharibu windo la nyoka


****
 
we nelson nan kakudanganya humu jf tunatumia majina yetu halisi? utakosa uhuru wa kuchangia mada, pole yako.., ilibid uulize kwanza... nakuambia hv kwa vile mi ni jirani yako tena swaiba kabisa lakin cdhan kama utakuja nfaham naitwa nan
 
we nelson nan kakudanganya humu jf tunatumia majina yetu halisi? utakosa uhuru wa kuchangia mada, pole yako.., ilibid uulize kwanza... nakuambia hv kwa vile mi ni jirani yako tena swaiba kabisa lakin cdhan kama utakuja nfaham naitwa nan
Mbona kawaida Komred mi sijifichagi nilivyo.Nina penda mtu anifahamu kiundani uli asiseme mi ni upepo wa mashariki unaovuma nyuma yako.
 
RIWAYA; JASUSI, KOMANDO

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA TATU...


Kumbukumbu zake zilimwambia, hakuwa amekiweka kitambulisho kile kwenye begi lake na kamwe hakuwahi kufanya kosa kwenye safari za siri kama hizo.

Alijiuliza kilifikaje kwenye begi na hakukiweka?

Kuna mtu alifanya vile, ni nani sasa!

Obi alipumua taratibu hakuwa amepata jibu la swali lile tangu siku anakamatwa na kuwekwa mikononi mwa wahuni wale wa Somalia. Mtu aliemuuza alimfananisha na popo wale walioharibu windo la nyoka.

***

Kukurukakara za nyoka na popo zilipungua. Ni dhahiri nyoka alikubali yaishe na aliwe bila kujitoa jasho katikati ya wahuni wa giza. Popo nao waliamua kuanza kugombana wao kwa wao, baada ya adui kushindwa na kukubali yaishe.

Obi aliamua kucheza pata potea, alitaka kutumia utamu wa nyama ya nyoka kupita katikati ya kundi la popo wakali. Aliamini mawazo ya wanyama wale, yalikuwa kwa kitoweo chao na si harufu ngeni himayani mwao. Pia alitaka kutumia turufu ya kila kiumbe chenye damu, kuwa na hofu pindi kikurupushwapo.

Obi alijifyatua kwa kasi kubwa na kwenda kulikumba kundi la popo lililokuwa linagombea mwili wa nyoka. Kama alivyotarajia, ndivyo ilivyotokea. Popo walisambaa huku wakipiga kelele za taharuki. Obi hakujali kelele zao, alizidi kutambaa kwa kasi kubwa ili atoke kwenye himaya ya popo wale kabla hawajajipanga na kumshambulia.

Mwili wake ulitota uchafu na kinyesi cha popo, pia alikwaruzana na mabaki ya kiumbe ambae hakumfahamu. Jibu la harufu kali ya uozo alilipata hapo.
Dakika chache badae, Obi alikuwa mbali na eneo lile lilomtia jamba jamba, japo alihisi michubuko kifuani na kwenye viwiko vya mikono yake, lakini hakujali kwa kuwa alifunzwa ukakamavu katika hali yoyote atakayokutana nayo awapo kazini.


Chemba ile iliotengenezwa kwa bomba maalumu, ilimfikisha kwenye makutano ya midomo mingi ya chemba zilizokuwa zinamwaga maji kwenye mkondo aliotokea. Kulikuwa na ngazi zilizoelekea juu kwenye makutano yale. Lakini ili uzifikie ni lazima usimame wimba, hivyo ni lazima uloweshwe na maji taka yaliokuwa yanamwagika kutoka kila pande. Obi hakuwa na chaguzi, alijitoa kwenye bomba na kusimama wima,kisha alibana pumzi ili asivute maji yale na alizishika ngazi na kuanza kukwea kuelekea juu. Ngazi zilimfikisha juu na alikutana na mfuniko wa chemba.

Alifanya jitihada kidogo na hatimae alifanikiwa kuusukuma na ukafunguka. Obi alitoa kichwa na kuchungulia pande zote. Hakuona mtu wala kiumbe yeyote aliekuwa anakatisha pale.

Chemba ile ilikuwa kando ya barabara.

Obi alisimama akiwa ameloa maji machafu, mwili wake ulitoa harufu kali ya uvundo na nguo fupi pekee iliokuwa mwilini mwake, nayo ilianza kumuwasha sehemu zake za uzazi.
Obi alihitaji kubadilisha mavazi ili aweze kuingia mtaani akiwa ni mtu miongoni mwa watu, hakutaka kuendelea kuzurura akiwa na chupi pekee.

Obi alianza kutembea katikati ya mji wa Berbera akiwa na chupi, huku mwili wake ukitoa harufu kali.

Obi alitembea hadi alipoifikia barabara, kisha alisimama katikati ya barabara na kutizama juu.

Alitaka kujua ilikuwa ni saa ngapi usiku na pale yupo upande gani wa mji Berbera. Alitaka kuyajua hayo, ili ajue anawezaje kuufikia usafiri kwa haraka na aweze kuelekea Mogadishu. Huku akiwa na wazo la kutaka kujua ni vipi watu waliomteka walipata taarifa, na aliamini kuwapata, kungemrahisishia kuyajua yale aliotumwa kuyajua.

Obi hakuijali taarifa ya taifa lake kumkana, alijua ni miiko ya kazi, hasa za ujasusi wa nje ya nchi. Hivyo ni sahihi nchi yake kumkana ili kuepuka mizozo ya kidiplomasia.

Alisimama na kutizama juu angani, aliona nyota nyingi zikilipamba anga la Berbera. Alikuwa anatafuta nyota moja ili ajue uelekeo gani alitakiwa kufuata.
Alitafuta nyota alioiona katikati ya mzingo wa nyota nyingi, wakati akiwa jijini Mogadishu. Nyota ile iliitwa Ndimila ni nyota ya mvua, na endapo angeliona tena, angejua ni wakati gani amekaa akiwa mateka.

Kwa nini!

Kwa sababu wakati anawasili Mogadishu ilikuwa utosini kwake, ikimaanisha ilielekea kipindi cha mvua kwa baadhi ya sehemu ndani ya nchi ya Somalia.

Macho yake yaoliona ile nyota, lakini wakati huu haikuwa utosini kwake, ilikuwa imehama zaidi ya sentimita kumi kutoka kilipo kichwa chake.

Obi alishangaa!!

Ina maana nimekaa hapa zaidi ya mwezi mmoja na siku zake?.
Obi alijiuliza huku akijishika kiuno kwa masikitiko.
Kwake haikuwa ishara nzuri, na kama adui atakuwa ameshapiga hatua nyingi mbele yake.

Komando hufundishwa kila kitu, hufundishwa kuhesabu muda kwa njia mbalimbali, walifundishwa kuendana na vipindi kwa njia ya kisasa ama ujima.
Hapo Obi alitambua muda aliokaa mateka kwa njia ya ujima. Alitaka pia kujua wakati huo itakuwa ni saa ngapi.
Bado bahati ilikuwa kwake, kwani kulikuwa na mbalamwezi iliowaka bila kujificha mawinguni.

Akiwa katikati ya barabara, Obi alitizama kivuli chake. Kivuli kilikuwa kirefu kwenda mbele, hiyo ilimaanisha ilikuwa ni saa tisa kwenda saa kumi alfajiri. Ili kujiridhisha zaidi, alitizama mbalamwezi ilipo. Aliona ikiwa imegeukia magharibi tayari kuzama.

Haraka alianza kutoka barabarani na kuelekea kwenye makazi ya watu, hakutaka kupambazuke nae akiwa bado na chupi huku akinuka mwili mzima.

Hakuujua vizuri mji ule wa Berbera, zaidi alijua ni mji wa biashara kwa kuwa ulikuwa na bandari ya kisasa, iliotumiwa na nchi za Djibouti na Ethiopia.

Kadri alivyokwenda, ndivyo alivyozidi kukutana na vichochoro vyenye giza na makazi yaliotulia. Akiwa amefika njia panda moja, hakuelewa afuate uelekeo upi.
Alisimama na kutafakari, lakini hakupata jibu.

Akiwa katika tafakuri hiyo, mara alihisi kuna mtu anamtizama kutokea pahali fulani. Alijaribu kuangaza mbele yake, lakini hakuona mtu.

Haraka aligeuka nyuma yake na kuona mtu akiwa mlango wa nyumba alioiacha nyuma yake akimtizama.

“Isma… Isma.” Mtu yule aliita na sauti ilikuwa ni ya kike.

Obi hakuitika na aliona hiyo ni turufu kwake, alipiga hatua na kuelekea kwenye nyumba ile.

Mwanamke yule hakuwa mjinga, aliona yule mtu sie aliemtegemea, haraka alifunga mlango na kurudi ndani.

Obi hakukata tamaa, aliendelea kwenda huku akipanga kutumia njia yoyote ile ili aweze kuingia ndani ya nyumba ile.

Alifika mlangoni na kugonga mara kadhaa bila kupewa majibu. Aliutizama mlango kama anaweza kuubomoa au kuufanyia jitihada zozote ili aweze kuingia ndani.

Mawazo yake yalikwama. Mlango haukuwa wa kawaida, ulikuwa ni mlango wa chuma uliotengenezwa maridadi. Kuuvunja ilihitaji vifaa maalumu ama bomu la mkono.

Alishika kiuno, alichoka akili na mwili na wakati ulizidi kusogea na zilisalia saa chache kabla watu hawajaamka kuendelea na shughuli zao.

Alianza kupiga hatua zake ili kujiondokea pale. Nyuma yake alisikia mlango ukifunguliwa, nae alisimama na kugeuka nyuma.

Alitoka mwanamke mrefu akiwa ameshika sime, alivalia suruali ya kubana na fulana iliokatwa mikono.

Mwanamke yule aliwasha taa ya nje na mwanga ulifanya waonane vyema na Obimbo Mtei.

Mwanamke yule alimtizama Obi juu chini, kisha alishusha pumzi.

Obi nae alimtizama mwanamke yule, na kuona uzuri wa kisomali; pua ndefu, shingo ndefu macho makubwa kiasi na nywele zilizolambwa.

Lakini Obi aliona zaidi ya hivyo.

Aliuona ujasiri wa mwanamke yule, mwanamke hakuonekana kuogopa lolote lile, na alikuwa na sime yake mkononi, tayari kwa lolote.

“Wewe ni nani!!” Mwanamke alihoji kwa lugha ambayo Obi hakuilewa.

Licha ya kutoelewa alichoulizwa, lakini Obi alihisi ameulizwa swali kati ya “Wewe ni nani” ama “Unataka nini”

Obi aliamua kucheza pata potea!

“Naitwa Rebu!” Obi alitaja jina bandia aliloingilia Somalia. Obi alijitambulisha kwa lugha ya kiingereza.

Berbera ni sehemu iliotawaliwa na waingereza na waitaliano, hivyo aliamini ni rahisi mwanamke yule kuelewa alichozungumza.

“Unatoka kabila gani!” Lilikuwa ni swali ambalo Obi hakulitegemea, na aliulizwa kwa lugha ya kiiengereza pia.

Somalia ni nchi inayoendekeza ukabila, na ili upate msaada kirahisi ni lazima uwe unatoka kwenye kabila moja wapo ndani ya Somalia na watakaokusaidia ni wanakabila wenzako na si kabila lingine.

“Mimi ni mgeni hapa Berbera!” Obi alijibu.
Mwanamke yule alimtizama tena Obi, kisha alimwambia.

“Kama wewe si mwenyeji hapa, hili sio eneo la wewe kuwepo, utauwawa muda si mrefu, mana kabila la Dir limezua vita hapa Berbera, wanataka kutawala. Hawataki watawaliwe na kabila letu la Isaaq.”

“Lakini sina mavazi, kama hutojali naomba unistiri kwa nguo yoyote unayohisi naweza vaa!”

“Hata nguo yangu?”

“Ndio!”
Mwanamke alitabasamu kwa huruma,kisha alimuomba Obi waongozane kuingia ndani.

“Usiguse chochote hapa ndani, unanuka sana!” Mwanamke alimwambia Obi baada ya kuingia ndani.

Obi alisimama katikati ya sebule na kujishika kiuno. Sebule ilikuwa imependezeshwa na samani za kiasili. Kulikuwa na viti vilivyotengenezwa kwa ngozi ya mnyama. Ukutani kulibandikwa picha kadhaa na moja ya picha ilimuonesha mwanamke aliempokea, pamoja na kijana mwingine mwenye wajihi wa Obi.
Waliendana kimo na upana wa mwili, lakini macho yake yalitangaza shari wakati wote na, hakuonekana kuwa mtu wa mzaha.

“Njoo huku uoge!” Mwanamke yule alimuita Obi.

Obi alipiga hatua mbili na kuingia ndani ya bafu aliloelekezwa. Bafuni alikuta sabuni ya maji na taulo safi jeupe.

Obi aliwaza ukubwa wa familia ile, aliona si familia yenye maisha duni sana, ni familia ya maisha ya kawaida, lakini alishindwa kuelewa kama; mwanamke yule na kijana aliemuona kwenye picha walihusiana vipi.

Hakutaka hilo limkae kichwani, alitaka kujiswafi na kuondoka ndani ya nyumba ile haraka iwezekanavyo.


***

Dakika kumi na tano zilitosha kumweka safi Obimbo Mtei. Alitoka bafuni akiwa amejifunga taulo na kwenda sebuleni.

Alikuta mwenyeji wake akiwa amekaa na sime yake, ni dhahiri hakumwamini mgeni wake.

Obi alishangaa, kwa sababu alijua amani itakuwa imetamalaki ndani ya nyumba ile, lakini kushikiwa sime, ilikuwa ni hali ya hatari imetangazwa upya.

“Nadhani ungeuliza zilipo nguo uvae, kuliko kunishangaa!” Alisema yule mwanamke huku akinyanyuka na kwenda kumpa nguo.

Obi alizipokea na kuzitizama. Ilikuwa ni surauli ya jinzi na fulana nyeusi.
Obi alizivaa.
Zilimtosha kama zilikuwa zake.

“Kama umetoshwa nguo, hata hivi viatu vitakutosha” Alisema yule mwanamke na kumpa Obi viatu aina ya raba, nazo zilikuwa nyeusi.

Obi alizitwaa na kuzivaa!.

Zilimtosha japo vidole vyake vilikuwa virefu kiasi.

“Ahsante!” Obi alishukuru.

“Mwenye hizo mali ni kaka yangu. Lakini omba usikutane nae huko mtaani. Kaka yangu ni kama Dubu.” Yule mwanamke alinyamaza kidogo, kisha aliendelea.


“Si unamjua Dubu?” Aliuliza. Obi alitikisa kichwa kukubali.

“Basi tabia za Dubu ndio anazo kaka yangu; haogopi, hajali hatari yoyote. Ni kama Dubu anavyotembea kwa miguu na mikono na akichoka anatembea miguu pekee,haogopi chui wala Puma. Haogopi Taiga wala Simba; popote vita!” Mwanamke alinyamaza na kusimama.

“Anaitwa nani kaka yako!” Obi aliuliza.

“Anaitwa Isma! Ni kiongozi wa kundi la makabila ya Isaaq, wanapambana na kundi la makabila ya Dir yanayotaka kuutawala mji wa Berbera!”

“Dir ina makabila mangapi?”

“Dir ni kabila kubwa lenye makabila mengine zaidi ya kumi, yani jamii yenye maelewano, lakini Isaaq ina makabila mengine zaidi ya ishirini, sasa wao wataka tutawala vipi”.


Obi alifikiria kidogo na kuuliza,…
“ Unaitwa nani!”
“Niite Bambi!”

“Ahsante sana Bambi, nitatamani kukuona tena” Obi aliaga.

“Omba uzima Rebu!” Bambi aljibu.


Obi aliondoka ndani ya nyumba ile, nje alikutana na machweo japo giza lilikuwa bado la kurashia.

Lakini kitu kimoja Obi hakujua ni kuwa; Kaka yake Bambi huweka walinzi wa kulinda nyumbani kwao bila dada yake kujua. Hivyo wakati anaingia na wakati anatoka, tayari taarifa zilishamfikia Isma kaka wa Bambi.
Obi kama alihisi ameacha na Bambi alijidanganya na, kama alihisi yupo salama pia alijidanganya.

Historia mpya alianza kuijengea pale Berbera, historia yenye mengi ya kutisha na kusisimua.

Obi hakujua yajayo.
IMG_1rwu0j.jpg
 
RIWAYA; JASUSI, KOMANDO.

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660.

SEHEMU YA NNE...


Obi aliondoka ndani ya nyumba ile, nje alikutana na machweo japo giza lilikuwa bado la kurashia.

Lakini kitu kimoja Obi hakujua ni kuwa; Kaka yake Bambi huweka walinzi wa kulinda nyumbani kwao bila dada yake kujua. Hivyo wakati anaingia na wakati anatoka, tayari taarifa zilishamfikia Isma kaka wa Bambi.
Obi kama alihisi ameacha na Bambi alijidanganya na, kama alihisi yupo salama pia alijidanganya.

Historia mpya alianza kuijengea pale Berbera, historia yenye mengi ya kutisha na kusisimua.

Obi hakujua yajayo.


-----------------

2
Dar es laam, Tanzania.

Maeneo ya Ilala kando ya ofisi za mkuu wa mkoa, kulikuwa na kikao cha siri. Kikao kile kilikutanisha watu sita pekee.
Kulikuwa na vijana watatu wakiwa wamevalia kijeshi na, mavazi yao yalikuwa ni maalumu kwa kazi za jangwa. Mbele yao kulikaa wazee watatu, wazee wale walikuwa wamevalia suti nadhifu na sura zao zilitangaza utashi wa akili zao.

Wazee wale waliongozwa na kamishina Zenge wa Zenge, ambae alikuwa ni kiongozi wa kikosi cha siri cha operesheni maalumu.

Kushoto kwake alikaa kiongozi wa operesheni na mafunzo kwa usalama wa nchi ya Kenya, bwana Abong’o Bin Aisha. Na kulia kwake alikaa kamishina wa operesheni maalumu jeshi la polisi Uganda, bwana Fredu Obiya.

Upande wa vijana waliokuwa wamevalia kijeshi; waliongozwa na Honda Makubi kutoka kikosi cha operesheni maalumu, chini ya kamishina Zenge wa Zenge. Pia alikuwepo komando Jose Mukasa kutoka jeshi la Uganda. Alikuwepo komando Odele Kennedy, kutoka jeshi la Kenya.

Watu hawa walikuwa wamekutana kwa kuwa kulikuwa na operesheni maalumu,iliohusisha nchi za Afrika Mashariki. Operesheni ile ilikuwa endelevu, na vijana wale walikuwa ni kwa ajili ya msaada, maana operesheni ilihitaji kutekelezwa na mtu mmoja tu, huku wengine wakibaki waokozi pale inapobidi.

Siku hii haikuwa nzuri kwa Honda Makubi. Hakuwa amefurahia maamuzi yaliokuwa yamefanywa na viongozi wake ambao ni wale wazee kutoka idara nyeti ndani ya majeshi ya nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.


“Huna haja ya kugafirika bwana Honda, ilibidi iwe vile ilivyokuwa.” Abong’o Bin Aisha alimwambia Honda ambae alikuwa amekaa kimya kwa muda mrefu.

“ Lakini kwa nini operesheni iliahirishwa,hata mimi bado nina mashaka na suala hilo!” Kamishina Zenge wa Zenge alimuuliza Abong’o Bin Aisha.

“Nimewambieni nilipokea taarifa kutoka kwa watu watu kule, Obi alihamishwa pale tulipolenga, dakika kumi kabla vijana hawajafika kwenye ile nyumba.” Abong’o alijibu.

“Lakini ilipaswa vijana waingie hadi ndani na kuhakikisha Obi hayupo pale ndani, kuliko kuagairisha misheni kirahisi namna ile!” Fredu Obiya nae alimaka.

“Ndugu zangu hatuna haja ya kulumbana, tuko hapa kuwakilisha mataifa yetu katika misheni hii. Kumbukeni tangu Obimbo atiwe nguvuni, wamekuwa wakimhamisha kila baada ya siku mbili. Lengo lao ni kuwapoteza wale wanaojaribu kuwafuatilia…” Abong’o alinyamaza kidogo na kisha aliendelea.

“….Picha za satellite zimekuwa zikituonesha namna kundi hili linavyomhamisha huyu bwana kila mara, hivyo sikuona sababu ya kuuza roho za vijana wangu, wakati mzigo tunaoutaka umeondolewa. Labda swali la kujiuliza; wao walijuaje sisi tutaenda pale, kwa sababu sehemu zingine alikaa siku mbili, lakini siku hiyo alikaa kwa saa chache kabla ya kuhamishwa.”

Ukimya ulitawala ndani ya chumba kile, lilikuwa ni swali la msingi sana kwenye kikao kile na, kila mmoja aliona uzito wake.

“Mbali na yote lakini, bado nashawishika kusema; Obi alikuwa ndani ya ile nyumba pale Somalia, lakini swali langu ni kwa nini kamanda alitutaka kuahirisha kuingia, tukiwa hatua chache kutoka ilipo ile nyumba?” Honda alihoji huku jicho lake akilitupa kwa Abong’o, dhahiri hisia zao hazikuwa sawa na kila mmoja alimuwaza mwenzake kwa utofauti.

“Honda!!” Kamishina Zenge wa Zenge alimwita Honda kwa ukali. Honda alipomtizama, aliona ishara nyingi juu ya uso wa kiongozi wake yule.

“Nadhani tujadili namna ya kuweza kupata tena fununu za wapi alipo Obi, kisha vijana wawahi kumuokoa. Wale wanamgambo hawatanii, wanaweza kumchinja kweli!” Fredu Obiya alitoa wazo.

Honda alisimama, kisha alivua mkanda na kofia.
“Wakuu, endeleeni na operesheni yenu, mimi najitoa rasmi na tafuteni mtu mwingine wa kukaa nafasi yangu. Siwezi kufanya kazi na kamati ambayo sijaridhika nayo.!” Honda alisema huku akivitupa alivyovua juu ya meza.

“Hili unalofanya ni kosa na litakugarimu, wewe ni mwanajeshi na umefunzwa kutii bila kuhoji wala kudharau wakuu wako, bado nafasi unayo, unaweza kubaki nasi!” Abong’o alimtahadharisha.

“ Bahati mbaya sana ni kuwa hata tukikamatwa hapa na vyombo vya usalama,mamlaka zilizotutuma zitatukana. Tuko hapa kisiri na hakuna atakaeniwajibisha kwa kazi ya siri, njia pekee labda uniue!” Honda alimjibu Abong’o na kuanza kuondoka ndani ya chumba kile.

“Acheni aende, namjua mimi na nitaweka mtu mwingine.. Nisameheni kwa utovu wa nidhamu wa kijana wangu.” Kamishina Zenge wa Zenge aliomba radhi.

“Miongoni mwa vijana uliowaamini ni huyu, kuondoka kwake naamini ni pigo kwa idara yetu hii isio na jina!” Fredu Obiya alisema.

Ukimya ulitanda ndani ya chumba kile.

“Naombeni tuendelee kukusanya taarifa kuhusu usalama wa kijana wetu kule Berbera. Tukutane saa moja jioni kwa taarifa zaidi!” Kamishina Zenge wa Zenge aliwambia wenzake.

Na kikao kiliahirishwa bila muafaka kamili, kila mmoja alichukua njia yake na kuondoka ndani ya chumba kile.

****

Baada ya kutoka kwenye kikao, Abong’o alienda yalipokuwa makazi yake ndani ya Havoc hotel huko Masaki.

Akiwa ndani ya chumba, alichukua mkoba wake kiofisi na kuufungua. Alitoa simu ndogo nyeusi na kuiwasha,kisha alituma ujumbe kwa mtu fulani.

“It’s showtime!” Ujumbe ulisomeka hivyo, kisha alifunga simu ile na kuirejesha ndani ya mkoba wake.

Wakati Abong’o akifanya mawasiliano, Kamishina Zenge wa Zenge alikuwa anamuwaza Honda Makubi. Huyu alikuwa ni kijana wake aliefanya nae kazi kwa muda mrefu na alimfahamu vyema.

“kuna jambo haliko sawa, Honda hawezi kuzira bila sababu, ukizingatia Obi ni rafiki yake wa karibu, mbali na kazi.” Kamishina Zenge wa Zenge alijisemea.

“ Lakini hawezi kuliacha hivi hivi, namuamini sana Honda, kuna njia ameona akiitumia, hili suala litaisha. Acha apite njia anazojua yeye!” Aliendelea kujiwazia, wakati akipanda ngazi kuelekea kwenye ofisi zake ndani ya makao makuu ya jeshi la polisi.

“Hili suala walioanzisha walikuwa sahihi, tatizo ni huyu kidudu mtu na fisadi alijipenyeza hadi chumbani kwetu, kiasi kila tunachoafanya kina wafikia maadui haraka. Obi hakuwa wa kukamatwa kizembe, ni lazima kuna mkono wa mtu kutoka ndani yetu!” Kamishina Zenge wa Zenge alijiwazia huku akisukuma mlango na kuingia ndani ya ofisi yake.

----

Honda Makubi alikuwa ndani ya gari akielekea nyumbani kwake. Njia nzima kuna jambo lilikuwa linatesa akili yake bila muafaka.

Honda alikuwa anateswa na operesheni ilioahirishwa dakika za mwisho kabisa. Hakujua sababu ni nini, hata kikaoni sababu haikumwingia.

“I say, abort mission…” Honda aliikumbuka sauti ya Abong’o kupitia earpiece zilizokuwa zimepachikwa masikioni mwao. Walikuwa watatu katika operesheni ile, na wote walitazamana baada ya kauli hiyo.

“Lakini tumebakiza hatua saba tu, kuingia ndani ya nyumba kamanda!” Honda alisema huku akitizama lango la nyumba moja iliokuwa kando ya bahari, kwenye mji wa Berbera. Walikuwa wamelala chini na bunduki zao mikononi.

“Hiyo ni kwa usalama wenu, Obi ameshaondolewa hapo dakika kumi zilizopita. It’s a trap kama mkiingia hapo!” Abong’o aliwatahadharisha tena.

“sisi ni makomando na tume….” Honda alinyamaza baada ya saa yake kuwaka mara mbili. Ilikuwa ni saa ambayo inauwezo wa kunasa muingiliano wa mawimbi.

Alishangaa!!

Ina maana kuwaka kwa kwa saa ile, kulikuwa na mtu mwingine aliekuwa anayasikiliza mazungumzo yao. Ni nani na yupo wapi.
Kwa namna saa ile ilivyoundwa, endapo mawimbi ya kunasa sauti yangelikuwa yametegwa wakati wote, saa ile ingeyanasa wakiwa mita mia moja, kutoka sehemu husika. Kuwaka kwa saa hatua saba kabla ya kufikia eneo lengwa, tena wakati ambao walikuwa katikati ya mazungumzo,ilimaanisha vifaa viliwashwa baada ya wawashaji kupewa taarifa za uwepo wao pale.

Ni nani alietoa taarifa, na kwa nini atoe taarifa wakati wa mabishano ya kutoelewana?

Honda hakujua!

Aliwatizama wenzake, kisha alipinda shingo kushoto kwake, ishara ya kuwataka waondoke eneo lile.

“Na wewe umekubaliana na kamanda?” Alihoji komando Jose Mukasa.

“Ni zaidi ya hiyo, tuondoke kamanda!” Honda alimjibu bila kumfafanulia.


Pipiiiiiii!!! Honda alishituliwa mawazo ni bodaboda iliompita kwa kasi.

Honda alishusha pumzi nyingi na kutizama kwenye kioo,lakini hakuweza kutia shaka kwenye msururu wa magari yaliokuwa nyuma yake.

“Kuna nini kwenye misheni hii, wale watu walijuaje tunafanya mawasiliano pale hadi wawashe mitambo yao?” Lilikuwa swali fikirishi na hakukuwa na wa kumjibu.

“Nitahakikisha nasafiri hadi Somalia, Obi hawezi kuchinjwa na wanaharamu kizembe namna hiyo!” Honda aliwaza peke yake huku akikata kona ya kuelekea nyumbani kwake.

Kitu kimoja ambacho Honda hakujua, nadhiri haitendwi. Na laiti angelijua yajayo, asingeliwaza safari ya Somalia. Lakini ni kwa sababu, yajayo hayajawahi kutoa taarifa.

Hakujua!!
 
RIWAYA; JASUSI,KOMANDO.

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA TANO.....


Honda alishusha pumzi nyingi na kutizama kwenye kioo,lakini hakuweza kutia shaka kwenye msururu wa magari yaliokuwa nyuma yake.

“Kuna nini kwenye misheni hii, wale watu walijuaje tunafanya mawasiliano pale hadi wawashe mitambo yao?” Lilikuwa swali fikirishi na hakukuwa na wa kumjibu.

“Nitahakikisha nasafiri hadi Somalia, Obi hawezi kuchinjwa na wanaharamu kizembe namna hiyo!” Honda aliwaza peke yake huku akikata kona ya kuelekea nyumbani kwake.

Kitu kimoja ambacho Honda hakujua, nadhiri haitendwi. Na laiti angelijua yajayo, asingeliwaza safari ya Somalia. Lakini ni kwa sababu, yajayo hayajawahi kutoa taarifa.

Hakujua!!

***
Honda aliingiza gari ndani ya uzio wa geti la nyumba yake. Ni baada ya kufungua geti kwa kutumia kitenzambali. Aliteremka na kulizima gari lake, kisha alitoa ufunguo wake na kuifunga milango vyema.

Alikuwa mbali na familia yake kwa muda wa wiki nzima. Aliikumbuka sana familia yake, hasa mwanae wa kiume aliepata kuwa na miaka saba.

Alitizama saa yake na kuona ilikuwa ni saa kumi na moja jioni. Alitegemea kusikia sauti za watu pale ndani. Lakini hakukuonekana kuwa na dalili ya uwepo wa mtu.

Jambo lile lilimfanya Honda alirudi nje kutizama mazingira.

Uwanja ulikuwa mchafu na hakuonekana kufanyiwa usafi siku za karibuni.

Aliguna!

Hisia zake zilimwambia, kuna kitu hakikuwa sawa pale nyumbani kwake.

Alichukua funguo zake na kufungua mlango, kisha alijitosa ndani taratibu na kwa umakini mkubwa. Alipokelewa na harufu ya vumbi, nyumba haikuwa imefanyiwa usafi kwa siku kadhaa, vumbi lilianza kutawala.

Honda aliitizama sebule na hakuona lolote jipya, alielekea chumbani kwa mwanae, huko pia hakuona jipya, alirejea chumbani kwake na mkewe.

Chumba kilikuwa kimepungua kitu fulani.

Nguo za mke wake!

Begi moja la nguo za mkewe, halikuwepo.

Amekwenda safari? Mbona hakuaga na wala hakuna taarifa alionipa?.
Honda alijiuliza kwa sauti na asipate wa kumjibu.

Alikiangalia chumba chake kama ni mgeni, na hakuwahi kukiona. Kwenye meza ya kitanda, aliona karatasi, lakini aliipuza.

Alitoa simu yake mfukoni na kumpigia mkewe.
Simu yake haikupatikana. Alijaribu kwa mara nyingine, na jibu lilibaki vilevile. Simu aliopiga, haikuwa ikipatikana.

Honda alishusha pumzi nyingi kwa mkupuo, alikumbuka kitu kingine cha kufanya.
Alipiga simu nyumbani kwa wazazi wa mke wake. Simu za wazee nazo hazikupatikana.
Honda alianza kubaha, aliona kuna kitu hakiko sawa, lakini hakuomba kiwe kibaya.

Haraka alitoka nje na kuingia ndani ya gari, kisha aliiwasha na kuondoka.

Safari yake ilimfikisha Feza school. Hapo alisoma mwanae, pia alifundisha mke wake. Hivyo taarifa za familia yake alitegemea kuzikuta pale.

Aliruhusiwa na walinzi kuonana na uongozi wa shule, alikutana na mwalimu mkuu msaidizi wa shule.

“Naitwa Honda Makubi, ni baba wa Jalali Makubi, pia ni mume wa mwalimu Subi.” Honda alijitambulisha.

Baada ya utambulisho, mwalimu mkuu msaidizi alimkaribisha kwa mazungumzo zaidi.

“Nimefika hapa nilikuwa naomba kuonana na familia yangu, kama bado wapo hapa shuleni!” Honda alimwambia mwalimu.

Mwalimu alivua miwani aliokuwa amevaa, kisha alishusha pumzi kwa wakati mmoja na kufuta macho yake, kisha aliivaa tena miwani yake.

“Bahati mbaya wiki yote hii mwalimu Subi hajahudhuria shuleni, na hakuna taarifa yoyote kuhusu yeye!”

Honda alihisi kichwa kikiwaka moto, haikuwa habari njema kabisa kwake.

“Taarifa za Jalali je!” Honda alihoji kuhusu mwanae Jalali.

Mwalimu alikuna kichwa kwa kidogo chake cha shahada, kisha alijiweka vyema kitini na na kumtizama Honda.

“Jalali hajaonekana shuleni kwa siku ya pili sasa, na alipoulizwa kuhusu mama yake, hakusema lolote zaidi ya kunyamaza, kiufupi hatuna taarifa kamali kuhusu watu hawa!” Mwalimu alimjibu Honda.

Honda aliegemea kiti chake na kutizama juu, hakujua ni tafakuri gani ilikuwa sahihi kwake, kila alilowaza hakuona kama lina msaada kwake.

Alimtizama mwalimu…

“Uongozi wa shule mlifanya jitihada gani kuhusu mwanafunzi na mwalimu wenu kutoonekana shuleni?”

“Uongozi wa shule huwa unautaratibu wa kuwasiliana na wafanyakazi wake, pindi wasipoonekana kazini na hawajatoa taarifa. Tulijaribu kuwasiliana na mwalimu Subi, lakini namba zake zote hazikupatikana.” Mwalimu alisema na kunyamaza kidogo, kisha aliendelea.

“…Kuhusu wanafunzi ambao husoma na kurudi nyumbani, huwa tunawasiliana na wazazi wao, lakini mzazi wa Jalali alieandikwa kwenye fomu ni mwalimu Subi na simu zake hazikupatikana.”
“My God!!” Honda alisema huku akiegemea kwenye kiti na mikono yake akiiweka kichwani.

Honda hakuwaza usalama, aliwaza hatari na hakujua itakuwa ni hatari gani ipo kwenye familia yake.

“Kazi hizi kuwa na familia, inahitaji moyo sana. Muda wowote familia inaweza kutumika kukuhujumu!” Honda aliyakumbuka maneno ya rafiki yake Obi. Ilikuwa ni siku chache baada ya kumaliza mkasa uliopewa jina la Mtumwa, na yalikuwa ni majuto ya Obi, baada ya wabaya wake kuitumia familia yake kumfanya watakavyo.

“ Haiwezekani bwana!!” Honda alijisahau na kuropoka peke yake, mbele ya mwalimu aliekuwa akimtizama wakati wote.

“Kuna tatizo lolote ndugu?” Mwalimu alihoji, baada ya kumuona Honda yuko mbali kimawazo.

“Hakuna tatizo Mwalimu!” Honda alijibu huku akisimama.

“Nadhani watakuwa nyumbani kwa bibi, na huko hakuna mtandao mzuri.” Honda alidanganya.

“Kama kuna tatizo, ni bora ukashirikiana na uongozi wa shule, ni familia yako na hujui ilipo, usalama unatoka wapi hapo?” Mwalimu alihoji.

“YSikuwa hapa nchini, nimerejea jioni hii na sikuwakuta, ndio nikaona nije hapa, hivyo wanaweza kuwa kwa bibi.”

“Sawa, kukiwa na taarifa zaidi tafadhali wasiliana na uongozi wa shule!”

“Haina shaka mwalimu!”
Honda alijibu huku akifungua mlango na kuondoka ndani ya ofisi za mwalimu mkuu.

Honda alitokwa na jasho la hofu, dhahiri mambo hayakuwa sawa kwa familia yake. Kwa haraka aliwaza kwenda nyumbani kwa wazazi wa mke wake. Lakini aliona ni mapema mno kufanya hivyo, na pengine lingezuka lingine zaidi kama angewashirikisha kwenye suala lile.

Alihitaji kufuatilia kwa makini ili ajue kinachoendelea.

Honda akiwa ndani ya gari, aliyakumbuka maelezo ya mwalimu. Alikumbuka Mwalimu alimwambia Jalali anasiku mbili haonekani shuleni, huku mama yake akiwa na wiki nzima.

Mama yake haonekani wiki nzima, mtoto siku mbili,..mmmh, kuna kitu hakipo sawa.
Honda aliwaza.

Kama siku zote mama hayuko shule, ni nani alikuwa anamwandaa Jalali? Na alikuwa analala wapi na gari la shule lilimchukulia wapi.

Honda aliendelea kuwaza, aliona alishindwa kufikiria vyema wakati anamhoji mwalimu kuhusu familia yake.
Alikumbuka nyumbani. Nyumba yake ilikuwa chafu na, uchafu wa zaidi ya siku tano.

Sasa Jalali alikuwa anaenda wapi na kwa nani?.. Afu….
Alisita kidogo, aliikumbuka karatasi aliokuwa ameiona ndani kwake kando ya kitanda.

Yeye na mke wake, hawakuwa na utaratibu wa kuhifadhi karatasi chumbani kwao; vitabu na karatasi nyingine huhifadhiwa kwenye chumba maalumu Kia ajili ya kujisomea na kufanya kazi nyingine zilizohusisha kalamu na karatasi.

Honda alihitaji kujua kuliandikwa nini kwenye ile karatasi, haikuwa bahati mbaya kuwepo pale.
Honda aliendesha gari kwa kasi kubwa, huku mara kadhaa akivunja sheria za barabara, kwa kuingilia barabara zisizomhusu na kutozingatia alama za barabarani.

Dakika ishiri badae, Honda alikuwa anaingiza gari kwenye uzio wa nyumba yake. Saa ilisomeka ni saa moja na dakika kumi na tano.
Honda aliingia ndani kwake na kuwasha taa.
Lakini wakati huu alinusa harufu ya manukato mageni puani mwake.

Kuna mtu aliingia ndani ya nyumba yake.
Aliingia kufanya nini, funguo alizipata wapi, hilo hakujua.

Kengele za tahadhari ziligonga kichwani mwake. Alirudia kuyatizama mazingira ya sebule yake.

Hata!!

Hakuna kilichokuwa kimebadilika, sebule ilikuwa vile vile kama alivyoiacha.

Haraka alipiga hatua ndefu na kuusogelea mlango wa chumba chake, alisikiliza kidogo, kisha aliusukuma kwa nguvu na kuingia ndani.
Alipokelewa na harufu ya manukato yale yale alioyanusa sebuleni. Macho yake yalikimbilia ilipokuwa meza kando ya kitanda.

Karatasi!!!

Kulikuwa na karatasi mbili tofauti na mwanzo kulipokuwa na karatasi moja.

Alichunguza chumba kwa umakini,lakini hakuona sehemu ilioguswa, chumba kilikuwa vile alivyokiacha.

Kilichomleta ni karatasi tu! Ni nani mtu huyu, alifuata nini?
Honda alijiuliza huku akisogea mezani. Alichukua karatasi moja kati ya zile mbili. Karatasi hii ilikuwa ni ile ya kwanza alioikuta wakati akiingia, alizitifautisha kwa sababu, katarasi alioichukua ilikuwa imenyofolewa kwenye daftari, huku karatasi nyingine ikiwa ni nyeupe isio na mistari.

Alikutana na mwandiko wa mkewe.

Kwako mume wangu kipenzi. Samahani kwa kutukosa nyumbani kwako. Maamuzi ya kuondoka ni kwa sababu wewe ni baba bora, lakini umesahau kuilinda familia yako. Kazi yako imegeuka hatari kwetu, kila siku tunafuatiliwa na magari tusioyafahamu. Magari hayo nina hakika hayakuhusu kabisa Baba Jalali.
Usomapo ujumbe huu, tambua nimeamua kujilinda mwenyewe na mwanangu. Nimeondoka na sitaweza kukwambia nilipo.
Baki na maisha ya kulitetea taifa, kuliko familia yako.
Ni mimi Subi, Mama Jalali.!


Eboh!!!

Honda alishika nyonga zake, hakuamini alichokisoma.

Kama kulikuwa na hatari, si ungenishirikisha Mama Jalali jamani!
Honda aliwaza huku akitisa kichwa.

Obi alikuwa sahihi, familia zina majaribu makubwa kwenye hizi kazi walahi!!.

Licha ya kuisoma barua ile, lakini bado hisia zake zilimwambia kulikuwa na la ziada. Kuna jambo halikuwa sawa kabisa.

Aliigeukia karatasi nyingine na kuichukua..

BLOCK 8, Sima Pub. Chumba namba 13.
Mchukue mwanao!!...

Alaaa!!!!

Yakoje mambo haya jamani!
Honda aliwaza. Mapigo ya moyo yalienda mbio, jasho lilimtiririka, mwili ulimtetemeka.

Mwandiko haukuwa wa mke wake, wala mtu aliemfahamu.

Familia yangu haipo salama, lakini wasithubutu kuidhuru.

Honda alijiapiza, huku akishindwa kuelewa vitu viwili; Barua ya mkewe ilionesha anaenda kujificha, lakini barua ya pili, ilionesha mtoto yupo Sima Pub.
Alifuata nini, mke yuko wapi na ni nani alimteka mwanae, anataka nini kwake.

Hayakuwa maswali ya kujibika. Honda hakuona mtu wa kumjibu, ikiwa ataendelea kujiuliza akiwa ndani ya nyumba yake. Alihitaji kutoka na kutafuta ufumbuzi wa mambo yale.

Honda aliifunga nyumba yake, kisha alipanda ndani ya gari na kuondoka.Alihitaji kuchukua silaha zake mahali fulani.

Wabaya walitangaza vita, nae alihitaji kuicheza hadi mwisho.

Katika maisha yake yote, kutembea nchi nyingi, lakini hakuwahi kukutana na lodge ama hotel yenye chumba namba 13. Kwake lilikuwa jambo geni na ambalo hakuwahi kufikiri kama litakuja kutokea, tena ndani ya nchi yake mwenyewe.

Sikuwahi kuona wala kusikia kuna nyumba za kulala wageni kuna chumba namba 13. Haya ni mageni kwangu.
Honda aliwaza.

***
 
RIWAYA; JASUSI, KOMANDO.

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660.

SEHEMU YA SITA..


Hayakuwa maswali ya kujibika. Honda hakuona mtu wa kumjibu, ikiwa ataendelea kujiuliza akiwa ndani ya nyumba yake. Alihitaji kutoka na kutafuta ufumbuzi wa mambo yale.

Honda aliifunga nyumba yake, kisha alipanda ndani ya gari na kuondoka.Alihitaji kuchukua silaha zake mahali fulani.

Wabaya walitangaza vita, nae alihitaji kuicheza hadi mwisho.

Katika maisha yake yote, kutembea nchi nyingi, lakini hakuwahi kukutana na lodge ama hotel yenye chumba namba 13. Kwake lilikuwa jambo geni na ambalo hakuwahi kufikiri kama litakuja kutokea, tena ndani ya nchi yake mwenyewe.

Sikuwahi kuona wala kusikia kuna nyumba za kulala wageni kuna chumba namba 13. Haya ni mageni kwangu.
Honda aliwaza.

***

Honda alifika kwenye makazi yake ya siri mnamo saa tatu kasoro. Alifungua geti la nyumba ile na kuingia, kisha alipaki gari lake na kuingia ndani.

Alielekea kwenye chumba maalumu, ambapo ilimlazimu kufungua kwa nywila. Alifungua chumba kile na kuingia.

Alikaribishwa na utulivu wa hali ya juu, aliwasha taa. Macho yake yaliishia kuona migongo mingi ya silaha mbalimbali. Kulikuwa na visu, panga, sime pamoja bunduki za kila aina.

Honda aliipenda silaha ya kisu, aliamini kisu kina ufanisi mkubwa kuliko bastola, hasa wakati ambao adui amekuzidi ujanja. Alichukua visu vidogo vinne na kuvipachika kwenye pindo la shati aliokuwa amevaa,kisha alichukua bastola yake na kuiweka kwenye ubavu wa kulia, mahali ambako angeliweza kuifikia kwa urahisi zaidi.

Alichukua dawa za kuongeza nguvu na kuziweka kwenye pindo la bukta aliokuwa amevaa, kisha alifunga kile chumba na kutoka. Alielekea chumba kingine ambako huhifadhi pikipiki yake aina ya Baja.

Aliikagua kidogo, kisha alichukua galoni la mafuta na kuijaza.
Nyakati kama hizo, Honda hupendelea kutumia usafiri wa pikipiki.

Alipohakikisha kila kitu kipo sawa, Honda aliitoa nje pikipiki yake na kuiwasha. Alitoka hadi nje, kisha aliiondoa kwa kasi na kuacha baadhi ya majirani wakishangaa.

-------

Sima pub ilikuwa ilikuwa ipo Sinza. Pub hii ilikuwa ni hadhi ya kila mtu. Waswahili husema ni pombe ya ngoma, kila mtu aliitumia bila kujali kipato alichonacho.
Ilifaa kwa kila mtu.

Pub hii ilikuwa na upande wa vyumba kwa wateja wanaopenda kupumzika baada ya kugida ulabu.
Biashara nyingi hufanyika hapo; halali na zisizo halali. Madada poa ilikuwa ni sehemu yao ya kujidai, kwa kuwa walikuwa na uhakika wa kupata mwanaume wa kulala nae, au kulala kwa dakika, wao hupenda kuita “Kuchetua”.

Usiku huo kulikuwa na band ya muziki ikitumbuiza. Ilikuwa ni band changa na haikuwa na ukubwa wa jina wala kufahamika. Nyimbo zao waliimba zilizokwisha imbwa na wasanii wakongwe wa muziki wa dansi, nao huzirudia na kufanya shangwe itamalaki ndani ya Pub, wakati wote.
Nje ya Sima Pub, Honda aliegesha pikipiki yake sehemu maalumu ya kuegesha. Alimlipa mlinzi wa kimasai aliemkuta pale,kisha alienda kujichanganya na ndani ya Pub ile kubwa. Hakutaka kuelekea upande wa vyumba vya kulala wageni. Alihitaji kujipa muda lau kidogo, aweze kuyaelewa mazingira ya pale Pub.

Alitafuta sehemu moja iliokuwa tulivu na hakukuwa na watu wengi, sehemu ambayo aliamini anaweza kuwaona watu wote watakaokuwa wanaingia na kutoka, upande wa vyumba. Pia wale ambao wangelikuwa wanacheza na wale wanaoenda kutuza wasanii.

Honda alikaa kwenye kiti na mikono yake aliiegesha kwenye meza, huku macho yake yakifanya ziara ya kutalii maeneo yote ndani ya Pub ya kisasa, ila yenye ufuska wa kutisha.

“Kaka twende nikuchetue,ni elfu kumi tu, bila vat.”

Honda alirejesha macho yake kando ya meza aliokuwa amekaa.

Alikutana na sura ya mwanamke mzuri, mwanamke alijua kurembua macho yake makubwa mithili ya kinyonga. Pua ilinusa harufu ya manukato ya bei ghali.

Vijana tunapitia majaribu sana, sasa huyu ukikutana nae ahsubuhi, hukawii kutangaza ndoa, utagombana na watu ili mradi ujipe umiliki kwa kiumbe kama huyu. Kumbe ni taxi bubu….. Honda aliwaza huku akimtizama yule mwanamke.

“Vipi baby, tunaweza kwenda? Chumba kipo ni bure kabisa, elfu kumi yako tu!” Mwanamke aliendelea kuchombeza.

Honda aliwaza kitu, kisha alimuuliza yule mwanamke…

“Nikitaka kulala je!”

Mwanamke aliguna, huku akitikisa makalio yake.

“Kulala bei kubwa… una laki moja?”

Honda nae aliguna..

“Laki sina, nina elfu themanini hapa!”

“Jamani bebi, toa laki, yani unapata huduma zote unazotaka!”

“Kama zipi!”

“Kukakanda mwili, ukitaka tigopesa, airtelpesa hata M-pesa.”
“Hizo ni huduma nyingi,mi nataka huduma ya kawaida tu!”

“Sawa, ila itabidi ugaramikie sehemu ya kulala!”

“Kwani hapa si wasema kuna chumba cha bure?”

“mh, hapa ni kwa kuchetua tu, hakuna nafasi za kulala.. Afu boss wetu huwa hapendi tulale na wateja hapa!”

Honda aliguna, habari ilianza kumuingia.

“Boss?, kivipi tena unakuwa na boss!”
“Yeye ndie anaetukaribisha hapa, anatupa chumba na kila kichwa kinachoingia, huacha elfu mbili mlangoni, hivyo ukilala unapunguza mapato.. Na …” Alinyamaza kidogo na kujichekesha kisimbe simbe.

Kisha alipeleka mkono begani kwa Honda.

“Bebi, naomba tuondoke, boss hajaniona, hivyo sitaki ajue nilifika na kwenda kulala na danga!” Mwanamke yule aliongea kwa kulegeza sauti yake nzuri na ya kuvutia.

Honda aliingiza mkono mfukuni mwake, kisha alitoa noti mbili za elfu kumi na kumpa yule mwanamke.

“Mi nataka kuchetua goli moja tu, nyingine utakunywa soda!”

mwanamke alitoa tabasamu zuri la kuvutia,alifurahi kupata pesa ya bure kwa kazi kidogo.

“Hivi waitwa nani vile!!” Honda alihoji kijanja.

“Kitemo, wengi huniita Malkia wa uswazi!”

“ooh malkia wa uswazi, unaishi wapi sasa malkia.!”

“Hapo sinza mori, karibu na sheli. Ukiulizia malkia hata kuku anakuleta ninapoishi!”
Kitemo alimjibu Honda, kisha alimshika mkono Honda na kuingia na kumnyanyua.

“Unanichelewesha hesabu bwana, twende nikuchetue!” Malkia alianza kumkokota Honda na kuwasukuma baadhi ya watu ili wapite.

Honda alitembea huku akitupa jicho lake kila pembe, aliyakariri mazingira vizuri na kuwatizama watu wote waliokuwa wakiserebuka muziki uliokuwa ukipigwa.

Honda na Malkia waliingia kwenye mlango wa vioo. Walipokelewa na mtu mmoja aliekuwa amesimama mlangoni, akiwa na funguo nyingi mkononi mwake.

“Nipe chumba, nina mgeni!!” Malkia alimwambia yule jamaa.

Walipewa funguo, kisha walianza kuifuata korido ndefu iliotenganisha vyumba kila upande.
Baadhi ya vyumba yalisikika makelele ya vilele vya mahaba, huku vyumba vingine kukiwa na ugomvi baina ya wageni na madada poa walioenda kuwastarehesha.

“Hao wameshindwana bei naona!” Malkia alimwambia Honda, huku akijitahidi kuchanganya hatua zake, na kufanya makalio yake yatatarike kama ameingiwa na siafu.

Walizidi kuviacha vyumba vile, kisha walikunja kulia na kufuata korido nyingine fupi. Korido ile ilikuwa imetenganisha vyumba sita. Vitatu kila upande.
Wakati wote huo, Honda hakuwa ameona chumba namba 13.

Au nimekosea? Alijiuliza.

“Lakini hapa ndipo Sima Pub, wala sijakosea.” Aliwaza tena.

“Karibu!!” Malkia alimkaribisha Honda, kwenye chumba kilichokuwa mwisho mwa korido ile, upande wa kulia kama ukiingia, na kushoto wakati ukitoka.

Honda hakutaka kuingia haraka, alitaka kuyasoma mazingira ya mle ndani.

Wakati akisita kuingia ndani; kilitokea kitu ambacho hakutarajia.
Kwenye mlango wa chumba cha pili, kutoka alipokuwa. Alitoka mwanamke aliekuwa amevaa hijabu nyeusi na kufunika uso wake wote.

Mwanamke yule hakuhangaika kutizama chumba cha jirani kunani, aliweka sawa mkoba wake begani na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea nje.

Honda alitaka kumpuuza na kuingia ndani, ili ambane maswali Malkia Maana lengo la kwenda nae kule, alitaka kujua kuhusu chumba namba 13.

Alisita kuingia!!

Mwendo!!

Mwendo wa yule mwanamke haukuwa mgeni machoni pake, anaufahamu mwendo ule.

“Mama Jalali!!” Honda alijisemea.

Mmh! Aliguna tena.

Mkoba!!

Mkoba aliufahamu vyema kabisa, ulikuwa ni mkoba wa Mama Jalali, mke wake. Mkoba ule aliununua mwenyewe kama zawadi siku ya kuzaliwa kwa mkewe.

Honda alifyatuka kwa kasi na kwenda kuuparamia mlango wa kile chumba alichotoka mwanamke aliemfananisha na mkewe.

Wivu!!!

Wivu ndio uliomfanya afyatuke kwa kasi kubwa na kuupamia mlango, alitaka aone mwanaume aliekuwa kwenye kile chumba na mke wake. Na kama kweli kulikuwa na mwanaume, Honda aliona atakuwa amedharauliwa sana na bwana huyo. Ile haikuwa sehemu sahihi kwa mkewe kupelekwa.

Patupu!!

Macho yake yalikutana na chumba tupu, hakukuwa na dalili ya uwepo wa mtu pale ndani, wala kitanda hakikuonekana kubeba kiumbe yeyote kwa muda mfupi uliopita. Honda alipiga hatua hadi maliwatoni,nako hakuona mtu.

“Lakini sijakosea, yule ni Mama Jalali. Yule ni Subi mke wangu!” Honda alijiwazia, huku mgongo wa kiganja chake ukigusa kitandani. Aliambulia ubaridi mkubwa, kuashiria hakukuwa na kiumbe hai kwenye kile kitanda.

Pembeni aliona kiti kikiwa tupu. Alipiga hatua na kukiendea, kisha alikigusa kwa mtindo ule ule aliogusa kitandani.

Joto!

Ngozi yake ilihisi joto la kiumbe hai, kilichokuwa juu yake, muda mfupi uliopita.

Maswali lukuki yalipita kichwani mwake, hakujua mkewe alikuwa pale anafanya nini. Je, anaishi kwenye Pub ile, au nae alikuja kumfuatilia mtoto?

Hakuna jibu lilokuwa sahihi kwa wakati huo.

Honda alitoka haraka kwenye kile chumba. Alikutana na Malkia wa Uswazi.

“Mwanaume malaya wewe, kaah mh, uliona sitakuchetua vizuri hadi unikimbie?” Malkia aliongea huku akiwa ameshika kiuno, na macho yake akiyachezesha juu chini, kwa dharau.
Honda alimtizama kwa hasira. Hakuwa na muda wa masihara tena, wala hakuhitaji mzaha.

“Pesa yako nimekupa, naomba utangulie nje ukatafute danga lingine!” Honda aliongea kwa utulivu mkubwa, huku sauti yake ikitangaza hasira iliojificha kifuani mwake.

Malkia alielewa. Hakutaka ubishi, alichanganya miguu yake na kutoka haraka. Huku makalio yake yakicheza tetema bila kupenda.

Honda aliachana nae. Akili yake iliwaza chumba namba 13. Chumba chenye namba ambayo hakuwahi kudhani kama kuna nyumba ya kulala wageni ingelitumia .
Hakujua kwa nini wamiliki hawajawahi kutumia namba hiyo kwenye milango ya vyumba.

Hilo lilikuwa ni swali ambalo, hakuhitaji jibu lake wakati huo.

Honda alipiga hatua na kuifuata korido iliokuwa upande wa kushoto wakati walipoingia na kuifuata iliokuwa upande wa kulia.

Alikutana na namba za vyumba kwenye milango iliotenganishwa na korido ile. Hakuwa ameona chumba chenye namba hiyo na, mbele yake vilisalia vyumba vinne; viwili kila upande.

Kulia kwake hakuona namba ile, lakini chumba cha mwisho upande wake wa kushoto, aliona namba 13 ikiwa juu mlangoni. Namba haikuwa imepachikwa katikati ya mlango, kama zilivyokuwa namba nyingine. Namba hii ilipachikwa juu kabisa ya mlango.

Kwa nini?

Hakujua!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom