Kitabu cha Gaddafi, THE GREEN BOOK

Kitabu cha Gaddafi, THE GREEN BOOK

Jamani that green book ni katiba ya nchi au ni nini?
Na je, hivi Libya wamewahi kuwa na mjengo wa bunge na wabunge?
Wamewahi kuwa na uchaguzi ndani ya hiyo miaka 41 na ushee?

Nauliza tu wakuu!
 
Hivi kuna watu wanapoteza muda kuwasoma hawa madikteta kama kina Gaddafi?

Sasa huyu anakaa kwenye power miaka 42 kama mfalme na watu wanataka kumsoma bado? Ana tofauti gani na Kim Il Sung na Juche?

Sababu pekee ya kusoma kitabu hiki ni kuchunguza delusion za megalomaniac narcissistic personalities tu.

Bora hata Nyerere aliposhindwa alijua kuachia ngazi.

Mkuu Kiranga heshima yako! Katika watu ambao nawaheshimu na kuwakubali
hapa jamvini, basi mmoja wapo ni wewe! yaani huwa nazimika kwa mahoja yako
yaliyojaa busara na hekima. keep up mkuu!
 
Wekeni kitabu cha waasi walio mchapa Coward Gadafi.
 
Wewe unashabikia mambo ya Gadafi umememjua baada ya kuwa mzee maana kila mtu akizeeka huanza kurejewa japo na busara na huruma kidogo hata kama alikuwa mnyama kama osama. Gadafi alishawahi kushirikiana na Nduli amini kututwanga sisi halafu leo hii unamsifia? Labda mnashare vitu fulani labda dini ndiyo maana unampenda lakini wengine hata sura yake tu hatuipendi.
 
Mkuu kama unatumia computa attach kama picha. Nitafurahi kukisoma mm pia ni mfwasi wa Gadaf japo ana mapungufu yake lakini Libya watamkumbuka. Bora kuwa na kiongozi kama Gadaf kuliko kubadili viongozi kila temu na kila anayeingia bora aliyepita

Hiyo demokrasia ya uongozi kwa temu imewasaidia Ghana,Botswana na Namibia pekee

Kwingine kote Africa bora ya Libya
 
Mnamo mwaka 1988 Gadhafi alimtumia Al-Megrahi kulipua ndege ya Pan Am iliyokuwa na abiria 243 wafanyakazi 16 ambao wote kwa ujumla wao waliteketea pamoja na raia 11 waliokuwa maeneo hayo Lockerbie nchini Scotland.<br />
<br />
Mwaka 2003 serikali ya Gadhafi ilikiri kuhusika na unyama huo na baadae kukubali kuzilipa fidia ya US$ 2.7 billion familia za wahanga wa tukio hilo.<br />
<br />
Sakata hili na nyingine nyingi zinaweza kukuonyesha ni kwa jinsi gani Gadhafi alivyokuwa akifuja hazina ya Libya jinsi anavyotaka bila kuhojiwa na yeyote yule.<br />
<br />
Hata kama huyu bwana alikuwa mtawala mzuri namna gani hakuwa na uhalali wowote kuitawala Libya kwa miongo minne au maisha maanake hakuwa na mipango ya kung'atuka kwa ufupi alikuwa rais wa maisha na mwisho wa siku angemkabidhi mwanae nchi aendeleze usultani.<br />
<br />
Kwa mtizamo wangu Gadhafi alilewa hela za mafuta akageuka dikteta na gaidi ndiyo maana hata majirani zake walikuwa hawampendi to hell with dictator Gadhafi and his son Islam.
 
Ndugu zangu wana fikra nzito!!! Ninajua wengi wetu tumeumia na tunasikitika na yanayotokea Libya.

Mimi ni mpenzi mkubwa wa siasa za Kanali Gaddafi. Ninapenda ku-share nanyi kitabu chake kinachoitwa THE GREEN BOOK.

Ninacho hitaji kwenu ni kunielewesha namna ya ku-upload kitabu hicho ambaacho ninacho katika soft copy. Nielekezeni namna ya ku-upload ili nanyi muweze kukipata.
mkuu asante sana. sisi wengine kimetufaa sana. achana na haya mavuvuzela ambayo yenyewe kila kitu ni kupinga tu hata kama kina tija.
 
mkuu asante sana. sisi wengine kimetufaa sana. achana na haya mavuvuzela ambayo yenyewe kila kitu ni kupinga tu hata kama kina tija.
Kama kina tija mbona hakijamsidia yeye.
 
Kama kina tija mbona hakijamsidia yeye.

wewe unailinganisha Libya na Tanzania, katika nyanja ya kiuchumi na kielimu?- Libya ina asset Katika nchi kibao Africa sisi tuna nini?, West walifreeze zaidi ya dola billion 130 za libya, hizo pesa zilipatikana na kutunzwa vizuri chini ya uongozi wa nani?

Sattelite ya kwanza ya Africa ya mawasiliano ni nani alitoa dola million 300?

Unaijua the great manmade river, mto ambao maji yake yametolewa chini ya jangwa la sahara na kuwa supplied katika miji ya Libya, dola billion 33 zilitumika katika hiyo project, ni kiongozi gani alipreside katika hiyo project?

kila mwezi kila mlibya anawekewa katika account yake dollar 500, ni lini bongo tutafikia hali hiyo?

Elimu bure mpaka University, sisi bongo hata hiyo form four ni ndoto!

Mlibya akitaka kwenda abroad kusoma serikali inafinance, bongo unaielezeaje?.

Unaujua mchango wa Ghadafi katika kupambana na Apartheid kule south Africa, jiulize ni kitu kilimfnaya Mandela kufunga safari kwenda Libya kumshukuru Ghadafi licha ya vikwazo vya anga west walivyokuwa wameiwekea libya.

Unaulezeaje mchango wa Libya kussurport vikundi vilivyokuwa vinapambana na France installed puppet regimes throughout Africa?

Kuhusu kumsurport Iddi-Amin, anyway ile vita kwanza ni contraversial kuna vitu vingi sisi bado hatuvielewi, Sisi bongo tumewahi kumsurport Savimbi at one time, naamini nayo ilikuwa ni mistake pia. Lakini Mwalimu Nyerere alikuwa rafiki wa Ghadafi na aliendelea kuwasiliana naye hata baada ya kug'atuka (hata msikiti wa Mwalimu uliojengwa butiama, fedha ilitoka kwa Ghadafi).

Gadafi alikuwa ametenga dola billion 30 ili zitumike kuunda Africa Monetary Fund , lakini hizo pesa zikawa freezed na serikali ya Obama, mwezi March, unaweza kuona ni kwa namna gani huyu bwana alikuwa na vision ya Africa.

Ghadafi ni mwanamapinduzi wa Ukweli, hawa waasi wa Bengazi si wanamapinduzi chochote, ni vibaraka tu wa West, na soon watajuta kwa kuwakalibisha wakoloni katika nchi yao!
 
Companero

Don't be blinded by books of politics and politicians most of them containing lots of rumors and lies, they preach democracy they practize ridiculous.
We are not blinded by the books, what is important is the content and knowledge not the writer.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom