Kiswahili cha "SOFT COPY" na "Hard Copy"

Kiswahili cha "SOFT COPY" na "Hard Copy"

Mkuu kiswahili bado sana katika misamiati ya kiteknolojia. kwa kifupi bado changamoto ni kubwa sana
lakini ametunyegesha hapo tuamke na kuibua yetu, wanasema if the only fruit you have is a lemon try to lemonade it and dont cry for an orange which you dont have
 
Kwa uelewa wangu nnavojua mm ni Rudufu tepe na Rudufu ngumu(Ila kwenye hard copy sijapata kiswahili chake sanifu)
 
Kwa uelewa wangu nnavojua mm ni Rudufu tepe na Rudufu ngumu(Ila kwenye hard copy sijapata kiswahili chake sanifu)
Duhu, ni aheri tu tuziite kopi kakamavu (hard copy) na kopi legelege (soft copy), apo itakuwa mchezo wote tumemaliza!
 
Kaka,

Nachukua fursa hii kukutahadharisha kuwa neno wajuvi halina maana sawa na neno wajuzi

Wajuvi kwa Kiswahili sanifu lina maana mbaya kama ifuatavyo:

1. Watu wanaojifanya kujua kila kitu [neno muhimu ni "wanaojifanya. Kwa lugha nyengine "much know"]

2. Watu wajeuri, wajuba,
Nilipoona neno wajuvi nikaogopa kuchangia. Ahsante
 
Nilipoona naambiwa kuwa "bado kuna muktadha hapo" baada ya kutoa maelezo ya mjuvi kwa mtoa mada, ikabidi nikae pembeni
Nilipatwa na fadhaa kidogo mwili ukwa tutwee! bahti nzuri kauli yako ikaleta faraja na afueni.

Yasemwa kuwa ni rudufu tepe na rudufu ngumu, ahli yetu Marwa akisema.
Nami nalitilia ubani maana rudufu ndiyo hiyo ikisema copy.
Mashallah ukiongeza tepe na ngumu haijambo, halijaharibika jambo.

Almaarufu Amavubi, nshakufahamu nasi tukuwia radhia marwiyatan, sote twajifunza na hakika hakuna mtimilifu ila maanani peke yake. Tuswemehe kwa sintofaham iliyojitokeza, ndio ndio ubinadam ivoo!
 
Nilipatwa na fadhaa kidogo mwili ukwa tutwee! bahti nzuri kauli yako ikaleta faraja na afueni.

Yasemwa kuwa ni rudufu tepe na rudufu ngumu, ahli yetu Marwa akisema.
Nami nalitilia ubani maana rudufu ndiyo hiyo ikisema copy.
Mashallah ukiongeza tepe na ngumu haijambo, halijaharibika jambo.

Almaarufu Amavubi, nshakufahamu nasi tukuwia radhia marwiyatan, sote twajifunza na hakika hakuna mtimilifu ila maanani peke yake. Tuswemehe kwa sintofaham iliyojitokeza, ndio ndio ubinadam ivoo!

Wallah hapajaharibika neno, maana wakti mwengine kheri huwa mikononi mwa shari.

Na imependezayo machoni ni ile ghuri ya kutafuta ilmu na sio kutosarifika kwa yale uambiwayo.
 
Kuna mtu alinambia eti ni RUDUFU NGUMU na RUDUFU MDEBWEDO respectively
 
Wallah hapajaharibika neno, maana wakti mwengine kheri huwa mikononi mwa shari.

Na imependezayo machoni ni ile ghuri ya kutafuta ilmu na sio kutosarifika kwa yale uambiwayo.
Kuntu!
 
Nilipoona naambiwa kuwa "bado kuna muktadha hapo" baada ya kutoa maelezo ya mjuvi kwa mtoa mada, ikabidi nikae pembeni
dawa ya tatizo si kulikimbia bali kulikabili
 
Nilipatwa na fadhaa kidogo mwili ukwa tutwee! bahti nzuri kauli yako ikaleta faraja na afueni.

Yasemwa kuwa ni rudufu tepe na rudufu ngumu, ahli yetu Marwa akisema.
Nami nalitilia ubani maana rudufu ndiyo hiyo ikisema copy.
Mashallah ukiongeza tepe na ngumu haijambo, halijaharibika jambo.

Almaarufu Amavubi, nshakufahamu nasi tukuwia radhia marwiyatan, sote twajifunza na hakika hakuna mtimilifu ila maanani peke yake. Tuswemehe kwa sintofaham iliyojitokeza, ndio ndio ubinadam ivoo!
Basi farijianeni kwa maneni hayo...........
 
Wallah hapajaharibika neno, maana wakti mwengine kheri huwa mikononi mwa shari.

Na imependezayo machoni ni ile ghuri ya kutafuta ilmu na sio kutosarifika kwa yale uambiwayo.
swadaktaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Omonto unachosema ni sahihi kabisaa kwa sababu hata wataalamu wa lugha wanamaizi kuwa hakuna lugha iliyo bora kuliko nyingine, lugha yoyote ni bora kwa sababu inawawezesha wanayoitumia kuwasiliana! Kiswahili ni lugha inayojitosheleza katika nyanja zoote
 
Tupe uduvi wako na wewe
Omonto unachosema ni sahihi kabisaa kwa sababu hata wataalamu wa lugha wanamaizi kuwa hakuna lugha iliyo bora kuliko nyingine, lugha yoyote ni bora kwa sababu inawawezesha wanayoitumia kuwasiliana! Kiswahili ni lugha inayojitosheleza katika nyanja zoote
 
Back
Top Bottom