Kisa cha daktari wa macho Muhimbili

Mfiaukweli

JF-Expert Member
Aug 30, 2018
5,636
8,774
Kisa cha kufukuzwa kazi mtumishi wa serikali (anaedaiwa kuchana juzuu) kimenikumbusha kisa cha daktari fulani wa macho Muhimbili mwishoni mwa miaka ya 70 na mwanzoni mwa miaka ya 80.

Huyo Daktari alipata scholarship kwenda Ujerumani Magharibi (kusomea taaluma ya macho shahada ya kwanza). Alifanya vizuri sana na Wajerumani wakamuongezea nafasi ya kusomea shahada ya pili, lakini kwa kuwa ruhusa (study leave) ilikuwa imeisha alilazimika kurudi nyumbani kuomba ruhusa upya kabla ya kuendelea na masomo.

Enzi hizo ilikuwa ni lazima mtu afanye kazi japo miaka miwili kabla hajarudi tena masomoni; na kwa kigezo hicho, daktari huyo hakupewa ruhusa, ila alishauriwa kusubiri miaka miwili. Ilipopita hiyo miaka akanyimwa tena ruhusa, na tena na tena.

Daktari akapata "kichaa" hadi kulazwa wodi ya vichaa. Kule Ujerumani wakaamua kumfuatilia kujua ni kwanini hakurudi kuendelea na masters yake (official correspondence ya Muhimbili kwenda Ujerumani ilikuwa: Jamaa ana kichaa kwa hivyo tunamteua mtu mwingine aje badala yake). Wajerumani wakamtuma supervisor wake kuja kuthibitisha. Na kweli wakamkuta mwanafunzi wao psychiatric ward na akiwa huko zaidi ya miaka miwili.

Supervisor alipomu-assess aliwaomba akae naye hotelini kwa siku 2. Daktari "kichaa" akapelewa Motel Agip na ndani ya saa 36 alishabadilika.

Wajerumani wakamchukua na alikuja kuwa specialist wa macho wa kutegemewa. Assume huyo Daktari asingefuatiliwa na hao Wajerumani angeishiaje? Tuna ma-specialist wangapi kwenye fani tofauti tuliowapoteza kwa kuwa tu hatuoni umuhimu wa kuponyesha badala ya kuadhibu?

God have mercy on this country.
 
Kitaalamu tunasema jamaa alikuwa insane at the material time (wakati anachana hizo juzuu).

Lakini kwa kuwa wamelihandle kisiasa as usual basi ndio kwisha habari yake.

Ewe muafrika ukipata nafasi ya kupotea hili bara fanya hivyo hima maana hili bara linasemwa ni la giza na kweli bado kuna giza jingi sana.


Unforgetable
 
Tuwekee jina lake hapa huyo daktari mkuu, pengine tunaweza kumfahamu. Ila serikalini watu huwa wanafanyiana mtimanyongo sana hasa miaka hiyo uliyoitaja.

Tukirudi kwenye mada, bandiko lako hili unalhusisha vipi na tukio la yule jamaa kuchana kitabu cha dini?
 
Kitaalamu tunasema jamaa alikuwa insane at the material time (wakati anachana hizo juzuu).

Lakini kwa kuwa wamelihandle kisiasa as usual basi ndio kwisha habari yake.

Ewe muafrika ukipata nafasi ya kupotea hili bara fanya hivyo hima maana hili bara linasemwa ni la giza na kweli bado kuna giza jingi sana.


Unforgetable
Para ya mwisho ndio yenyewe. Ni bora kutokomea kusikojulikana, kwa mtu mwenye akili sawasawa matukio kama haya yanakudumaza kiakili kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuchana Quran na Biblia ilitakiwa kuwa sehemu ya free speech.

Nchi zilizoendelea kama Marekani unaruhusiwa kuchana Biblia, Quran.

Unaruhusiwa hata kuchoma moto bendera ya Marekani.

Ila ununue yako uichome yako mwenyewe.

Ni free expression.

Ni huko tunakofuta ujinga bado ndiyo mnajiletea matatizo ambayo hayapo.

Na labda ni sawa.

Kwa sababu mnafuta ujinga bado.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo maana cha muhimu ni kutafuta namna, ukiweza unaondoka kwenye hili bara la giza. Maana mambo ya wakazi wake yamejaa giza tupu, si wasomi wala si wasiosoma, hawana tofauti ukiacha tofauti ya kujua kiingereza na kuajiriwa kwenye ajira rasmi.
 
Yaani kama mimi saa hizi ni wanted, japo nasaidia watu matatizo yao kila siku ikiwemo hao wanaonitafuta.
 
Tuwekee jina lake hapa huyo daktari mkuu, pengine tunaweza kumfahamu. Ila serikalini watu huwa wanafanyiana mtimanyongo sana hasa miaka hiyo uliyoitaja.

Tukirudi kwenye mada, bandiko lako hili unalhusisha vipi na tukio la yule jamaa kuchana kitabu cha dini?

Nimeficha jina kwa makusudi maana hajanipa ruhusa nimtaje (na siamini kuwa watoto,wajukuu au ndugu zake) wangependa nimtaje. Ila nina uhusiano nae kiukoo.
Huyo anaedaiwa kuchana juzuu nae yaweza kuwa ni mgonjwa anaestahili kusaidiwa (ili arejee kutimiza majukumu yake ya kifamilia, kijamii na kiserikali). Inawezekana kabisa kuwa jamaa ni mfanyakazi mzuri tu na kawa distressed tu hadi kuchana juzuu.
 
Hivi unawajua waislam weye? Eti achane kitabu cha Allah halafu useme alikuwa na tatizo la kiakili anahitaji kusaidiwa.
My brother stay out of this.
Nimeficha jina kwa makusudi maana hajanipa ruhusa nimtaje (na siamini kuwa watoto,wajukuu au ndugu zake) wangependa nimtaje. Ila nina uhusiano nae kiukoo.
Huyo anaedaiwa kuchana juzuu nae yaweza kuwa ni mgonjwa anaestahili kusaidiwa (ili arejee kutimiza majukumu yake ya kifamilia, kijamii na kiserikali). Inawezekana kabisa kuwa jamaa ni mfanyakazi mzuri tu na kawa distressed tu hadi kuchana juzuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom