Basi hapo mwanzo abunuasi alibahatika kuwa na mbuzi jike hivyo basi akawa na fikra za kuwa tajiri hapo baadae kwani alijua kwamba ipo siku ambapo mbuzi wake angezaa na yeye angekuwa tajiri kwa kuwa na mbuzi wengi.Basi siku moja alienda nambuzi wake malishoni na wakati alipokuwa anatembea mara akaona kiatu kizuri sana tena cha gold njiani lakini kutokana na upungufu wake wa mawazo hakukiokota kile kiatu akaamua kuendelea na safari basi baada ya mwendo kama wa masaa mawili aliona kiatu kingine cha gold yaani mwenza wa kiatu kile cha mwanzo,safari hii aliamua kukiokota kile kiatu akakiweka sehemu ambapo alimfunga mbuzi wake na kuamua kurudi kukifwata kiatu cha mwanzo kwa bahati mbaya alipofika eneo husika hakukikuta kiatu kile ndipo alipoamua kumrejea mbuzi wake pamoja na kiatu cha pili alicho kiacha cha kushangaza hakumkuta mbuzi wala kiatu ndipo alipoanza kuhuzunika na kulia kwani ndoto yake yakuwa tajiri ilikuwa imetoweka .MWISHO