only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...Hakuna anayeweza kupinga kuwa kipindi cha DK 45 kinachorushwa na ITV chini ya S.Semunyu kama mtayarishaji na mtangazaji kilivuta usikivu na hisia za watu sana wakati kinaanza.Na hii inatokana na umahiri wa mtangazaji kuwahoji maswali wageni wake pale studio.Tangu kimeanza hiki kipindi ni kama kina mwaka mmoja na miezi kadhaa hivi,lakini kinachosikitisha kila siku tunapata wageni walewale tena kwa kurudia zaidi ya mara moja.Hii haitoi uwanja mpana wa kupata maoni kutoka pande mbalimbali za uongozi.
...Mbaya zaidi ni bora kama mtayarishaji wa hiki kipindi angekuwa anawaalika watu tofauti tofauti toka huko CCM,lakini cha kushangaza sasa ameanza kurudia kuwaita watu aliokwisha waalika muda mfupi uliopita.Alianza Wasira na sasa Chami...sidhani kama kwa mwendo huu hiki kipindi kitaendelea kujijengea heshima,nahisi kitaanza kupiromoka kwa kasi sana.Kwanini hataki kuwaalika watu toka upande wa pili,toka vyama vya upinzani au watu wengine na sio kurudia watu wale wale tena wengine wameanza hata kutoka kwenye mawazo ya watanzania na hawataki kuwasikiliza.
...Hali hii inaweza kuchukuliwa kama ilikuwa ni janja ya huyu jamaa kuanzisha kipindi kwasababu ya kulinda maslahi ya watu fulani,na kwa kweli ifahamike wazi kuwa kwa sasa waandishi wengi wa habari wameanza kukosa weledi wanafanya mambo kwa maslahi ya kundi fulani la watu.
Nawasilisha!!
...Mbaya zaidi ni bora kama mtayarishaji wa hiki kipindi angekuwa anawaalika watu tofauti tofauti toka huko CCM,lakini cha kushangaza sasa ameanza kurudia kuwaita watu aliokwisha waalika muda mfupi uliopita.Alianza Wasira na sasa Chami...sidhani kama kwa mwendo huu hiki kipindi kitaendelea kujijengea heshima,nahisi kitaanza kupiromoka kwa kasi sana.Kwanini hataki kuwaalika watu toka upande wa pili,toka vyama vya upinzani au watu wengine na sio kurudia watu wale wale tena wengine wameanza hata kutoka kwenye mawazo ya watanzania na hawataki kuwasikiliza.
...Hali hii inaweza kuchukuliwa kama ilikuwa ni janja ya huyu jamaa kuanzisha kipindi kwasababu ya kulinda maslahi ya watu fulani,na kwa kweli ifahamike wazi kuwa kwa sasa waandishi wengi wa habari wameanza kukosa weledi wanafanya mambo kwa maslahi ya kundi fulani la watu.
Nawasilisha!!