Maana halisi ya neno kipembe inatokana na pembe, yaani "umbo linalofanywa na ncha mbili zinapokutana". Katika matumizi ya kawaida, neno kipembe linatumika zaidi katika jengo, nyumba.
Pengine kwa sababu hiyo ndio maana kipembe likaitwa gereza kwa lugha ya mitaani kwani ni pahala pa kujitenga panapotumiwa na mfungwa anapokuwa na woga, huzuni au upweke, hukaa kipembeni mwa chumba.