Wanajamvi mnisaidieni Magufuri anaulizwa kipaumbele chake,anasema ni Ilani ya CCM.Huyu mtu kweli amejiandaa au anajua anachotakiwa kufanya?
Chanzo: EATV
Chanzo: EATV
Ujuavyo sivyo, kuna nchi ilani inatolewa na mgombea kama Marekani, lakini kwa Tanzania mgombea anayewakilisha chama anaenda kuuza kile ambacho chama kimepanga kifanyike, kumbuka chama ni jumuiya ya watu,wanakaa na kukubalina ni kipi kifanyike kwa wakati fulani, juzi wamepitisha ilani ya CCM 2015-2020, anayeibeba ilani hii ni mgombea urais.
Ni wajibu wake kuhakikisha anawaelewesha wananchi kilichopo kwenye ilani na akishinda akatekeleze yote yaliyopo kwenye ilani, ilani inabeba kila kitu unachokiwaza wewe,kipo mle Iwe utawala bora, iwe mapambano ya rushwa, iwe kilimo, iwe fursa kwa vijana na wanawake, elimu n.k vyote vipo mle...wajibu wake ni kuhakikisha hayo anayatekeleza vizuri na kwa kasi