Nilianza kuwa na mvi nikiwa o-level...nikapataga mafuta flani yanaitwa 'Restoria' pale SH Amon kariakoo sijui Posta sikumbuki vizuri...yalikuwa mazuri sana mvi zinapotea taratibu ila kwa uhakika..nilivyofika chuo nikawa naziachia tu mvi mpaka leo...juzi kati nimempeleka mdau mmoja hapendi mvi sh amon ya Arusha wakatuambia hawajayaagiza miaka mingi...labda ununue online...ni ya South Africa.
Ila mpaka leo najiuliza yale mafuta yanatumia mechanism gani maana mvi zinapotea kabisa halafu mafuta yenyewe ni meupe.