KIPANYA LEO: Msaada kwenye tuta!

KIPANYA LEO: Msaada kwenye tuta!

Huyo Tai chakula chake kikubwa ni mizoga inayoachwa na wanyama huko porin sasa , porini kumekauka na hakuna tena mizoga ndio kaibuka makaburini labda anaweza kubahatisha mzoga . Kifupi picha hiyo inaelezea Janga la NJAA ambalo lipo Bongo .Kwa maoni yangu, labda mtu mwengine anaweza kutufafanulia zaidi.
 
Kuna mtu alisema Tai kakosa minofu iliyohai kaenda kufukua Makaburi. Hiz dot zake nilizielewa kidogo, nahisi kama kuna Bundi pembeni wanasaidizana hiv kujiandaa kufukua Makaburi


Nahisi ile kauli ya hatuta fukua makaburi inakwenda kwisha taratibu. Tunyooshe mzee kama tulipinda
 
Ni kwamba Tai anakula mizoga, ameenda kuvizia mizoga makaburini (madhambi ya zamani) sasa anakula mzoga huu bila kumaliza anahamia kaburi la pili, ndiyo ujumbe kinachofanywa na Makonda
 
Darubini kali ya Maoudi kipanya, nami sijapata hasa wazo analojaribu kujenga kwa kutumia picha. Sawa Brother masoud!!
 
Nihisi ni ile ya kuzika juu ya makaburi mengine ndio anamaanisha kuwa tai anakuja kujiokotea mizoga ktk hayo makaburi. Ila kwann ni misalaba (makaburi ya wakristo? ) hapo sina jibu

Misalaba au makaburi ya wakristo ni rahisi kufahamika kwa muundo wake. Isingeeleweka haraka kama hayo ni ishara ya makaburi kama angetumia ya kiislam
 
Kiukweli huwa naelewa sana kazi yake but leo nimefail kuelewa nini alikuwa anamaanisha...

View attachment 474188
Kwanza kabisa huyu ndege sio Tai. Ni dumbusi, ndege mla mizoga, maiti.

Hasa hapo ukicheki vizuri utaona mafuvu na kama ishara ya maji maji (damu) kwenye misalaba, ikimaanisha kuna vitu vimekufa na mizoga ina tafunwa ( kwamba mambo yana hariba zaidi ).....…..
 
.....
 

Attachments

  • Vulture.jpg
    Vulture.jpg
    30.6 KB · Views: 38
Kipanya ni hatari Leo nimecheka sana kwenye PB kuwa kuna watu wanapaswa kuendelea kushikilia nyadhifa zao zile zile kwa maana wakipromotiwa kwenda level zingine wanaharibu kwa maana hawana uwezo
 
Nahisi ile kauli ya hatuta fukua makaburi inakwenda kwisha taratibu. Tunyooshe mzee kama tulipinda
Ni kweli point yako
kwa sasa makaburi hayatafukuliwa tena waliokwisha tuhumiwa na madwa ndio hao hao
Tai kachoka na haioni mizoga tena ni STOP sasa
 
Ukungu Umetanda , Kazi ya Tai Kufukua Makuburi inaonekana kumuwia Ngumu , anaonekana kachoka na Mazingira si Rafiki kwake Tena kuendelea na Jukumu hilo.
Pia kama kuna michirizi sijui ya damu au kinyesi yupo hoi dhurfil hali.
 
Back
Top Bottom