Rejao na avatar yake ya kishetani, huwa na namuona kama shetabi tu. Hapa kachukua picha ya zamani anaanza kubwabwaja! Sorry, I hate you!
Ana pesa mingi lakini bado ana tamaa na ni mnafiki!Mkuu jaribu kutumia akili zaidi ya kuropoka bila uelewa.Mbowe alirudisha gari la KUB ili kuweka msisitizo kuhusu ulazima wa serekali kubana matumizi na kupunguza expenses ambazo zinawaumiza wananchi.kwamba alionyesha kwamba chadema hawako bungeni kwaajili ya kujinufaisha ila kutetea haki za wanyonge.baada ya kuprove hilo akaenda kuchukua gari lake.ni wazi kwamba hilo gari lingeendelea kutumiwa tu na serekali kama asingeamua kulichukua...Muhimu message aliyokusudia ilifika kwa walengwa.Mbowe ana pesa mingi sio mtu wa kushadadia v8..
Hahaha...hata awe nazo kumi, that is not our concern. Tunachoangalia hapa ni kwanini alinga'ang'anie hili alilolikataa kwa mbwembwe.Mbowe ana VX V8 mbili mimi nimeziona kwa macho yangu Moshi!
Kwa hiyo si ajabu kachukua moja na kuweka plate namba ya KUB!
Kiherehere cha nini??
Hahaha...hata awe nazo kumi, that is not our concern. Tunachoangalia hapa ni kwanini alinga'ang'anie hili alilolikataa kwa mbwembwe.
Rejao ingekuwa vema ukaorodhesha hayo mengi ili sisi ambao tumeamua kuwa wafuasi tujitoe haraka kabla mambo hayajaharibika, tafadhali ndugu yangu tusaidie kwa hilo ili angalau tusije juta baadae..View attachment 54426
Kwa taarifa tulizonazo na wanachi wengi wanavyofahamu, tayari hili gari V8 limekwisharudishwa na Mh. Freeman Mbowe. Lakini cha kushangaza bado huyu mkuu analitumia.
Nashindwa kuwaelewa hawa CDM, kelele zote wanazopiga ni kutuhadaa tu wananchi? Kama kwa hili dogo huyu Mh. kashindwa kulitekeleza, je hayo anayoyahubiri kila siku majukwaani ataweza kuyatekeleza?
Hii inanifanya nikose imani na wapinzani, yapo mengi tu wanayoyazungumza mbayo ukijaribu kuyaangalia utekelezaji wake ni kitu kisichowezekana. Cha muhimu hawa viongozi wetu wasiwe ni watu wa kutudanganya ili kujipatia umaarufu. Kama ukiamua kufanya kitu, fanya kweli!!
Hii habari ina uzushi gani?Yaani katika huu uzi Rejao na Ritz wangeongea jambo la maana ndo ingekuwa mara yangu ya kwanza kuona hawa watu wameleta kitu cha maana hapa jamvini.
siku zote hao ni habari za uzushi na zisizo na maana kwa taifa hili lenye umaskini wa kusababishiwa na Baba zao akina JK, Lowassa, Rostam, Chenge, Che Mkapa n.k
Kukataa gari moja si kutatua tatizo, tatizo lilipo ni mfumo uliopo, uhajitajika muundo mpya wa kiutawala utakaoleta tija kwa maendeleo ya wananchi wetu. VX V8 moja kamwe haiwezi kuleta kitu, lazima uwepo umoja wenye nia moja ya kufika malengo yaliyo sawa. Kwa sasa tujiulize ni viongozi wangapi wako aware na vision na mission za serikali yao? hapo ndipo utakapojua kuwa viongozi wengi hawajui wanaelekea wapi na kwa nini. niishie hapa kwa leo.
Tusijibu kishabiki tu kwa sababu tuna mapenzi na Chama husika. Jaribu kupima alichokizungumza na anachokitekeleza sasa. Ni vitu ambavyo haviwiani. Ni bora angekaa kimya aendelee tu kujifaidia V8 lake.
Matumizi ya hilo gari kwa mwenzi garama yake inatosha kuwalipia wanafunzi 10 wa UDSM ada.Wakati mwingine kweli kutetea Magamba lazima uwe na kichwa kama cha mwendawazimu, waziri mkuu alishawahi kusema magari ya bei kubwa yasinunuliwe fedha hiyo itumike kununua matrekta, serikali ya CCM ikaamua kununua, Pinda kasema hawezi kutumia ilhali gari limenunuliwa, saa hilo la Mbowe limenunuliwa na serikali yenu, kama pale mwanzo alilikataa, kama alikuja kuliomba tena kwanini msingemkatalia? sasa leo mnatuletea upuuzi huo, aheni tuam,bieni kwani hali ya maisha inazidi kuwa ngumu hadi wanafunzi UDSMM wanajiuza hilo la Mbowe na hiyo gari si hoja hapa.Kwanza nina imani hata kama si hilo gari kifedha Mbowe bado ana uwezo wa kununua zaidi ya hilo