Hivi kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni bado anatumia shangingi la serikali?

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Naomba kukumbushwa kwani aina hii ya magari ni miongoni mwa magari ambayo si tu ya thamani kubwa bali hata gharama za uendeshaji ni kubwa mno.Inasemekana gharama za uendeshaji wa V8 moja kwa mwaka ni zaidi ya 100ml.

Tunaambiwa vipuri vya magari haya bei yake ni kubwa mno pale inapotokea vimeharibika.

Kuna kipindi Mh Mbowe alionesha uzalendo wa hali ya juu alirudisha hili gari(KUB) lakini badae kukatokea uvumi alikata shauri nakulirudia tena kwani mwanzo alilirudisha kwa pressure kutoka kwenye chama lakini yeye alikua bado analipenda.

Wakati fulani mh Pinda nae alifurukuta kuishauri serikali iachane na matumizi ya haya Magari lakini alichemka.

Usitishwaji wa matumizi wa haya magari ni jambo la msingi sana hasa katika kipindi hiki ambacho nchi yetu inanyimwa misaada na nchi wahisani.

Kwa mwenye kufaham naomba kujulishwa kwa faida yangu na wanajukwaa wengine.
 
Bado analo...wakati alipolirudisha mara ya kwanza serikali haikulipaki likaendelea kutumika kaa kawa na serikali kuzidi kuingia kwenye gharama kubwa za kulihudumia...ikawa bora alichukue tena na kuendelea kulitumia kwa kazi zenye tija..
 
Bado analo...wakati alipolirudisha mara ya kwanza serikali haikulipaki likaendelea kutumika kaa kawa na serikali kuzidi kuingia kwenye gharama kubwa za kulihudumia...ikawa bora alichukue tena na kuendelea kulitumia kwa kazi zenye tija..
Mkuu hapo unamtetea huyu mjanja wa mjini,
Hem chukua mfano huu;
Jana wakenya wamechoma moto pembe za ndovu zilizokamatwa zenye thamani ya mamilioni ili kutuma salamu kwamba biashara ya pembe za ndovu ni haramu,sasa kama ni Mbowe hapo nahisi angeziuza ili kutopoteza pesa,
Tizama hili lingine la ZZK;
Zito alipolishawishi bunge juu ya uharamu wa posho nakuona haungwi mkono yeye ameendelea na msimamo wakutokupokea posho mpaka leo huku wanzeke wakiendelea kuzichukua,
Kama mbowe analitumia hili gari lenye kuiingiza serikali gharama kubwa anapaswa kutiliwa shaka juu ya uzalendo wake kwa taifa.
 
Mkuu hapo unamtetea huyu mjanja wa mjini,
Hem chukua mfano huu;
Jana wakenya wamechoma moto pembe za ndovu zilizokamatwa zenye thamani ya mamilioni ili kutuma salamu kwamba biashara ya pembe za ndovu ni haramu,sasa kama ni Mbowe hapo nahisi angeziuza ili kutopoteza pesa,
Tizama hili lingine la ZZK;
Zito alipolishawishi bunge juu ya uharamu wa posho nakuona haungwi mkono yeye ameendelea na msimamo wakutokupokea posho mpaka leo huku wanzeke wakiendelea kuzichukua,
Kama mbowe analitumia hili gari lenye kuiingiza serikali gharama kubwa anapaswa kutiliwa shaka juu ya uzalendo wake kwa taifa.
Ni kweli mkuu....siwezi kumsemea mbowe ambaye simfahamu hata kidogo... nahisi serikali yetu iliyoyanunua haya magari ndio tuiulize kwanza...maana kama ni uzalendo ungeanzia ndani ya serikali na wengine wakafata... mbowe anaweza kulirudisha hili gari je yatakuwa yamebaki mangapi??
Anza na mawaziri
wakuu wa mashirika ya umma
ma RC
MA Dc

Na wengine wengi....serikali ikisema haya magari ya anasa hayaitajiki na mbowe akazidi kuling'angania ntakuwa na mashaka nae..

Hebu kwanz kabla hujamwambia mbowe hebu zungumza na mkuu wa kaya juu ya magari haya...
 
Na wakati huohuo nenda na GIMMYs mkashawishi lumumba waishauri serikali ichome pembe za ndovu zilizoko bohari, kama Kenya walivyofanya. Wasizing'ang'anie
Garai bado analo namshauri alisuse na kuliacha hilo gari kama yeye bingwa wa kususa susa.
 
Back
Top Bottom