Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kituko nimekiona, hapa kwetu kijijini,
Kuna mtu ni kijana, anaitwa bwana Joni,
Ana sifa ya aina, maana sijabaini,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Wanamuita kinyozi, apitapo mtaani,
Eti yeye ni mjuzi, wa fani ya kizamani,
Wala hakuanza juzi, alianzia mjini,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Na tena hana ofisi, kila siku yu nyumbani,
Kuna kitu ninahisi, kumuhusu bwana joni,
Sijauona mkasi, kaushika mkononi,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Madada wamsifia, eti ni fundi jamani,
Kila anapopitia, wanajigonga kwa joni,
Wakaka wamchukia, kinyozi kinyozi gani,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Beti zangu zimekoma, swali ninalo kichwani,
Isiwe natia noma, nifukuzwe kijijini,
Nilosema nimesema, mnijibuni watani,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Kuna mtu ni kijana, anaitwa bwana Joni,
Ana sifa ya aina, maana sijabaini,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Wanamuita kinyozi, apitapo mtaani,
Eti yeye ni mjuzi, wa fani ya kizamani,
Wala hakuanza juzi, alianzia mjini,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Na tena hana ofisi, kila siku yu nyumbani,
Kuna kitu ninahisi, kumuhusu bwana joni,
Sijauona mkasi, kaushika mkononi,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Madada wamsifia, eti ni fundi jamani,
Kila anapopitia, wanajigonga kwa joni,
Wakaka wamchukia, kinyozi kinyozi gani,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Beti zangu zimekoma, swali ninalo kichwani,
Isiwe natia noma, nifukuzwe kijijini,
Nilosema nimesema, mnijibuni watani,
Kinyozi asiyenyoa, huyo kinyozi wa nini?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)