Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,975
- 2,170
Km kweli elimu yake ndogo basi itakuwa shida sana, alafu inauma sana. Kile kigezo cha kujua kusoma na kuandika naomba kingeongezwa cha "elimu ya mgombea ubunge iwe atleast bachelor degree". Ni aibu sana kwa mtu asiyesoma anakwenda KUTUNGA SHERIA alafu anakwenda KUZISIMAMIA, anaowatungia ni wananchi ambao wamemzidi kielimu, naomba kigezo cha elimu nacho kipewe kipaumbele, ndio maana WASOMI miaka hii wanazidi kudharaulika. KIGEZO cha AJUE KUSOMA na KUANDIKA kilikuwa ENZI ya NYERERE maana zamani kujua hivyo ilkuwa shida, miaka hii ni tofauti na zamani. Umuhimu wa elimu haupewi kipaumbele, elimu sio kipaji ila nilazima usome. Watu wanapropaganda sana, mara utasikia naongozwa na Roho Mtakatifu hata kwenye mambo ya kiutaalamu!, tubadilike wagombea wasome waelimike na co umaarufu wao
Rejea rasimu ya pili ya Tume ya Warioba, ilikuwa imependekeza mgombea ubunge awe na elimu angalau ya Form IV; lakini baada ya wana UKAWA kujitoa, waliobaki walikiondoa hiki kipengele na kurudisha angalau ajue kusoma na kuandika (darasa la saba kwenda chini) kama ilivyo kwenye katiba ya sasa toleo la mwaka 1977. Kwa hiyo Kingwendu kateuliwa kwa mujibu wa sharia na kanuni.
