Kingwangala: Tabora ni ya CCM, CHADEMA inawahadaa wana Tabora

Kingwangala: Tabora ni ya CCM, CHADEMA inawahadaa wana Tabora

Kwani huko upinzani ulipojenga ngome ccm ilikuwa imetelekeza hiyo mikoa? Kilimanjaro, Mbeya, Kigoma, Dar, Mwanza, Shinyanga, nk, mikoa hii iko mbali kimaendeleo kulinganisha na Tabora, sasa ccm kwavile haipendi watu waelimishwe kuhusu haki zao ndo wanalalamika Tabora wataamka. Ushahidi uko wazi, ona vionngozi na wabunge wa cm wanavyo jaribu kuzuia watanzania kuangalia bunge. Yaani hawataki tuelewe wanavyo tufanya matractlr yao. Naamini siku yaja ccm mtakufa wote
 
Hamna sehemu yeyote ambayo CCM wanaweza kujivunia nayo kwa sasa. Ukiona wananchi wanaishabikia na kuichagua CCM ni kwa sababu hiyo sehemu haijafikiwa. Madamu Tabora imeshafikiwa na CHADEMA, haitatokea iwe the same Tabora.
 
Unahakika hatuna barabara ya lami? Toka enzi za mkoloni tulikuwa na lami. ukituwa airport ya Tabora (mjini) hadi town lami ukipandisha mlimamani camp ya jeshi mara ya mwisho kuwa Tabora ilikuwa 2009 msijenge mtazamo Tabora Bush Mji wetu ina historia sema watu wakisha fanikiwa hawarudi kwao kuiendeleza ndomana I admire watu wa Kilimanjaro wanavyoipenda Mkoa wao!

Acha kulala usingizi wewe! Hicho kipande cha km 5 tu kilichopo hapo manispaa ya Tabora, utasema Tabora kuna lami?
Ebu fikiria adha wanaipatayo wasafiri na wenye magari katika sehemu hizi:
Nzega - Tabora,
Urambo - Tabora,
Sikonge - Tabora,
Igunga - Tabora,
Itigi - Tabora
Ebu niambie hiyo lami iko wapi ktk sehemu hizi?
 
Mbunge huyu wa Nzega amekiri bungeni kuwa wananchi wa mkoa wa Tabora wote huwa wanaichagua CCM, jambo hili linawakera CHADEMA na kuwafanya waende Tabora kuwahadaa wana-Tabora kuwa, nanukuu, "CCM inawahasi na hawatafanya chochote kwani wanajua hata iweje ni lazima muichague CCM."

Hapa bwana Kingwangwala alikuwa akimtahadhalisha Dr Mwakyembe afanye kazi kwani hataki jimbo lake na Tabora ichukuliwe na wapinzani hasa CHADEMA, na zaidi ya yote na maelezo yote aliyoyatoa, amekataa kuunga mkono hoja ya wizara ya uchukuzi.
mikoa yote isiyokuwa na maendeleo ndio ngome za ccm lakini mambo yanabadilika walianza Kigoma sasa Mtwara Tabora watafuatia mkoa ambao hauna barabara ya lami inayoingia katika mkoa huo
 
Back
Top Bottom