Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

sina maana hiyo.hadi sahizi zaidi ya makada kumi wa ccm wapo kwenye mbio za ubwana mkubwa. ni hao hao walio unda mitandao ya kuchafuana. kimsingi kati ya walio tangaza nia wazi wazi hadi sahz hakuna alie msafi hata amnyoshee kidole mwenzake thus why naaamini NEC na CC watajuwa ni nani atafaa kukabidhiwa bendera ya kijani na si wao kuanza kuvuana nguo
 
Upo sahihi kabisa. Huyu mzee na familia yake walijichukulia tenda ya kukusanya ushuru wa magari pale Ubongo, wakawa wanakusanya zaidi ya milioni 10 kwa siku, halafu wanapeleka jiji milioni 4. Hiyo ndiyo zawadi ambayo Kikwete aliitoa kwa Kingunge na familia yake!

Yote majizi ila yamezidiana viwango tu.Hata Kingunge nae ni wale wale.
 
Mueleweni huyo mzee anamaana CCM itachagua mtu asiye msafi na kumuita msafi kwakuwa hajaitwa kuonywa.Anaelewa kuwa wananchi na vyombo vya habari vinajua uchafu wake hivyo msishangae au musitumie hiyo sifa kumnyima kura yeye na CCM.Mzee hana msaada kwa nchi bor amuwahi mwalimu
 
Nafurah sana kama magamba wenyewe wanakiri kwamba hakuna msafi...UKAWA ndio Habari ya Tanzania
 
David, that is where unakosea, yaani tusuri mamlaka iliyooovu watulete walioowaovu. Haya mambo ya kuwwachia unawaita mamlaka ndiyo yamegarimu taifa hili kwa mua mrefu. Ni kiwakataa pamoja na mamlaka zao hizo.
mkuu kuna watu wanafikiria katika namna ya tofauti sana,kana kwamba jamaa hana historia ya mamlaka teuzi za CCM,ovyo kabisa huyo
 
Hivi alisema hakuna msafi au hakuna asiyetumia hela, na kila mmoja chanzo cha hela yake kinajulikana.
 
Kati ya watu wanaoheshimika ndani ya CCM ni Kingunge Ngombare Mwiru. Leo katika mahojiano na mwandishi wa habari ITV amezungumza jambo ambalo wananchi hawana budi kuyazingatia.

Tuchague viongozi bora na si bora kiongozi. Pia kwa kauli ya kwamba hao wanaojitembeza sasa hivi siyo wasafi,Sasa je CCM imejiandaa vipi kupata mtu msafi?

Je, nani aliyemsafi ndani ya CCM?

Hakuna mtu msafi duniani. Sote tumetenda tu wachafu. Kiongozi wetu tunayentaka ni yeyote Mtu mwenye uwezo wa kutuongoza atakayeheshimu katiba na kusimamia sheria zetu, kanuni na taratibu tulizojiwekea na tutakazoziweka. Tukiamua hakuma ufisad,i hakuna kuiba basi kiongozi huyo asimamie hayo. Aheshimu maamuzi ya wengi, Nk.
 
Kati ya watu wanaoheshimika ndani ya CCM ni Kingunge Ngombare Mwiru. Leo katika mahojiano na mwandishi wa habari ITV amezungumza jambo ambalo wananchi hawana budi kuyazingatia.

Tuchague viongozi bora na si bora kiongozi. Pia kwa kauli ya kwamba hao wanaojitembeza sasa hivi siyo wasafi,Sasa je CCM imejiandaa vipi kupata mtu msafi?

Je, nani aliyemsafi ndani ya CCM?

Ndani ya CCM hakuna mgombea msafi hata mmoja. Mgombea safi na makini atatoka UKAWA.
 
yupo sahihi wasafi wapo sana tena wengi tu subiri wakati ufike.
 
Mueleweni huyo mzee anamaana CCM itachagua mtu asiye msafi na kumuita msafi kwakuwa hajaitwa kuonywa.Anaelewa kuwa wananchi na vyombo vya habari vinajua uchafu wake hivyo msishangae au musitumie hiyo sifa kumnyima kura yeye na CCM.Mzee hana msaada kwa nchi bor amuwahi mwalimu



anao msaada kwani hata ushauri ni msaada pia. amewaasa watanzania "chagueni kiongozi bora na si bora kiongozi na pia neno hakuna aliyemsafi" ni ushauri na huo ni msaada au kwa upande wako neno HAKUNA linamaanisha nini?
 
Hakuna mtu msafi duniani. Sote tumetenda tu wachafu. Kiongozi wetu tunayentaka ni yeyote Mtu mwenye uwezo wa kutuongoza atakayeheshimu katiba na kusimamia sheria zetu, kanuni na taratibu tulizojiwekea na tutakazoziweka. Tukiamua hakuma ufisad,i hakuna kuiba basi kiongozi huyo asimamie hayo. Aheshimu maamuzi ya wengi, Nk.

asante kwa kushiriki. nadhani unajaribu kutengua alichosema. kuna makosa ya kimungu na kuna makosa ya ki bin adam. alichozungumzia yeye ni uchafu wa kimatendo kama rushwa,wizi,ufisadi na hila zote ambazo hatma yake ni mateso kwa watanzania. kila mwanadamu anakasoro zake na kila mwanadamu anatenda vile aonavyo. matendo ya mtume Muhammad au nabii Issah hayawezi na hayatakaa yalingane na summaye au lowasa ingawaje wao walikuwa bin adam kama sisi. Matendo ya Karume ni tofauti na Kikwete
 
kwa mtindo huo hakuna msafi pande zote hata ukawa wenye nguvu ya kupita ugombea ni wachafu bora hata ccm na kama unasema kuna msafi niambieni nani?
 
wotee wale wale fisiem hakuna msafi labda warioba peke yake
 
kwa mtindo huo hakuna msafi pande zote hata ukawa wenye nguvu ya kupita ugombea ni wachafu bora hata ccm na kama unasema kuna msafi niambieni nani?

ukawa hawajai fisidi taifa hili haise unakosea kufananisha tembo na sungura
 
CCM inahitaji wazee km hawa wanaotamka ukweli!!Wazee km kina Msuya, Marcella ni wazee waganga njaa walioacha kutumia ubongo kufikiri na sasa wanatumia utumbo mpana kwa kulamba viatu vya mafisadi na kuishia kutumika kma misukule!!?Ni janga kwa taifa hili na hawafai kabisa kuwa watoa ushauri ktk taifa hili maana nahisi hata familia zao zimewashinda.
 
Ni kidonge kichungu, lakini ni ukweli ambao hawawezi kuukwepa
 
Back
Top Bottom