Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

Mwanasiasa mkongwe wa chama cha mapinduzi na kada mshauri wa chama Kigunge Ngombare Mwilu asema wagombea urais CCM hakuna aliye msafi mwenye kumnyoshea kidole mwingine kwamba ni mchafu.

Ameenda mbali zaidi na kusema wagombea wote watatumia fedha na wote wanahitaji fedha hivyo haina haja ya kuonyoshea vidole wengine hivyo wananchi wanachotakiwa ni kupima utandaji wao.

Chanzo: itv
Yeye mwenyewe Kingubge ana usafi gani?
Mzee wa watesi wa maalbino!
 
kati ya watu wanaoheshimika ndani ya ccm ni kingunge ngombare mwiru. Leo katika mahojiano na mwandishi wa habari itv amezungumza jambo ambalo wananchi hawana budi kuyazingatia. Tuchague viongozi bora na si bora kiongozi. Pia kwa kauli ya kwamba hao wanaojitembeza sasa hivi siyo wasafi,.sasa je ccm imejiandaa vipi kupata mtu msafi? je nani aliyemsafi ndani ya ccm?
Subirini, haraka ya nini? CCM ina hazina kubwa, siyo CHADEMA Slaa akifa leo jawana mtu tena.
 
Huyu mzee ni mtu wa Lowasa saaana, sasa ametolewa kwenye pango na kauli ya Mzee Msuya. Sasa sikia anasema wote si wasafi hivyo tuangalie utendaji, akimaanisha Lowasa ni mtendaji mzuri. Jamani sifa ya kwanza ni UADILIFU, hayo ya utendaji yatakuja kama an added advantage. Kama hakuna msafi wapishe watanzania wengine kutoka UKAWA waongoze nchi.
 
ananchomanisha kama ni fedha wote wanatumia fedha ndani ya ccm hivyo hakuna wa kumnyoshea kidole mwingine
Team LOWASSA wote hiyo ndiyo itakuwa tafsiri yenu kila siku. LOWASSA lazima apigwe chini kama ni ardhi kupasuka na ipauke.
 
Alimaanisha Hakuna aliyekamilika mbele ya Mungu, kila mtu ana mapungufu yake ktk Dunia hii, hata kama sisi binaanadamu hatuujui chafu wako ila mungu anajua zaidi. Malaika pekee ndio hawakosei lkn sio ninaadamu. Kwa hiyo wanao uwania URAISI sio malaika ni binaadamu.

Hapana unamlisha maneno Kingunge hakusema hayo uliyosema wewe. alichosema ni kuwa CCM wasitafute mchawi kwa kuwa hakuna msafi katika wagombea urahisi. Kwa lugha rahisi kingunge amekiri kuwa awamu hii hakuna mgombea safi kutoka CCM hivyo yuko tayari kwa mabadiliko nje ya Chama. jiandaeni kisaikolojia
 
mkuu kama sio msafi mngempa kuwa mshauri mkuu wa chama na serikali
Kwa hiyo ni mshauri wa watu ambao siyo wasafi? acha akili za siasa hizo, akili kama hizo waachie LEMA na Sugu
 
All CCM are dogs..they just differ in barking rate..
 
Hapana unamlisha maneno Kingunge hakusema hayo uliyosema wewe. alichosema ni kuwa CCM wasitafute mchawi kwa kuwa hakuna msafi katika wagombea urahisi. Kwa lugha rahisi kingunge amekiri kuwa awamu hii hakuna mgombea safi kutoka CCM hivyo yuko tayari kwa mabadiliko nje ya Chama. jiandaeni kisaikolojia
Yuko tayari kwa mabadiliko ya chama? Hizi hoja za kuforce mtaziacha lini? Au unafikiri akili za watanzania ni za ki-BAVICHA BAVICHA wanywa viroba.
 
Kwa hiyo ni mshauri wa watu ambao siyo wasafi? acha akili za siasa hizo, akili kama hizo waachie LEMA na Sugu
MKUU hajasema ccm yote hakuna wasafi ila waliotangaza nia ccm mbona ina watu wasafi kama warioba
 
Anauma na kupuliza sio???!!
Ajue tumekua sasa hatuamini kila litokalo kwa wakubwa, tunachanganya na zetu!!
 
Yuko tayari kwa mabadiliko ya chama? Hizi hoja za kuforce mtaziacha lini? Au unafikiri akili za watanzania ni za ki-BAVICHA BAVICHA wanywa viroba.

Kwa kweli CCM mmeanza kuchanganyikiwa. Kama mnaanza kutukana hata wazee wenu laana inawakula vizuri.

Hebu tueleze Mzee kingunge ameanza lini kunywa viroba?

LAANA IMEWAKAMATA MAPEMA KUPITA MAELEZO...
 
Kati ya watu wanaoheshimika ndani ya CCM ni Kingunge Ngombare Mwiru. Leo katika mahojiano na mwandishi wa habari ITV amezungumza jambo ambalo wananchi hawana budi kuyazingatia.

Tuchague viongozi bora na si bora kiongozi. Pia kwa kauli ya kwamba hao wanaojitembeza sasa hivi siyo wasafi,Sasa je CCM imejiandaa vipi kupata mtu msafi?

Je, nani aliyemsafi ndani ya CCM?

Waache kutupigia kelele, hao wanaotuambia na kuwanyooshea wenzao vidole kuwa hawafai, kwanini hawatuambii ni akina nani wanaofaa kushika nafasi hiyo ya urais kwa mwaka huu, badala yake ni kuendesha majungu ya chuki dhidi ya wengine! Ingekuwa ni vema wangetuambia kuwa fulani hafai basi mchagueni fulani ili tuone kama anafaa!
 
huo ndo ukweli wa mambo hakuna wa kimnyoshea kidole mwenzake ndani ya ccm. watangaza nia wote wameandaa milima ya pesa kwaajili ya uchagiuzi na wote wana wapambe na mitandao nchi nzima kuhakikisha wanashinda. kilichopo wanazidiana pesa ndo maana wanaki na Lowasa kila kukicha. nina imani na halmashauri kuu ya ccm kwamba watatenda haki na wtatuletea mtu makini bila kujali majungu ya kimtandao.

Hivi unategemea kuletewa mtu makini toka ukoo wa panya road (ccm)?
Hizi akili za kushikwa ni shidaa....mwenyewe umekiri hakuna msafi bado unataka kuletewa mtu kwenye hao wachafu???

Hii shida sijui lini itawatoka aisee.... Mtalaaniwa na vizazi vyenu vyote kwa kutumika vbayaa.
 
ni katika maana hii wasaka urais na makundi yao waache kuchafuana. mamlaka za kuteua ndo watakao chambua na kuona nani anafaa na nani hafai

David, that is where unakosea, yaani tusuri mamlaka iliyooovu watulete walioowaovu. Haya mambo ya kuwwachia unawaita mamlaka ndiyo yamegarimu taifa hili kwa mua mrefu. Ni kiwakataa pamoja na mamlaka zao hizo.
 
Back
Top Bottom