Ng`wanakidiku
JF-Expert Member
- Apr 18, 2009
- 1,195
- 232
Mwandishi wetu, Pwani
MWANASIASA mkongwe nchini Kingunge Ngombale - Mwiru ameibuka na kuwataka wenye ushahidi na watu wanaodaiwa kuwa mafisadi wautoe hadharani
"Tuache kupakaziana maneno mabaya kama ufisadi kwani neno hilo lina maana mbaya kuliko inavyodhaniwa na iwapo kuna mtu ana ushaidi na matendo ya ufisadi ya mtu ni bora ayatoe hadharani na kutoa ushahidi kulio kuendelea kuchafuana kwa kuitana kila kukicha mafisadi" alisema Kingunge.
Mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini alisema hayo wakati akizungumza katika mkutano maalumu ulioandaliwa na CCM Wilaya ya Bagamoyo ambao pamoja na mambo mengine ulilenga kuimarishaji chama hicho wilayani humo.
Kingunge alisema hivi sasa imekuwa ni tabia kwa baadhi ya viongozi wakiwamo wa dini na wanasiasa kutumia majukwa yao kuwavunjia heshima viongozi waliopo madarakani kwa kuwaita mafisadi huku wakiwa hawajui hata maana halisi ya neno hilo.
Alisema viongozi hao wanadhani kuwapo kwa mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kutoa maoni hapa nchini ni kuruhusu watu kutokuwa na adabu kwa wenzao dhana ambayo alisema si sahihi na hivyo alishauri iachwe mara moja.
"Hili ni jambo lisilowezekana hata kidogo kiongozi anachaguliwa na wananchi halafu wanatokea baadhi ya watu wanamvunjia adabu kiongozi huyo, mimi nadhani huko ni kuwatukana wananchi na hakukubaliki katika mahala popote", alisema Kingunge na kuongeza:
Akizungumzia suala la udini lililoshika kasi hivi karibuni, Kingunge alisema Watanzania wanapaswa kusimamia maadili yao waliyozoea tangu enzi za mababu kwani wapo baadhi ya wanasiasa na viongozi wa dini ambao wamefilisika kimawazo na hivyo wamekuwa wakitumia udini kutaka kuwagawanya wananchi.
Source: http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/21744-kingunge-awafyatukia-wanatamka-ufisadi
Fikra zangu:
Nadhani huyu mzee yupo ICU kiakili na mawazo. Na hii ndiyo inayopeleka CCM shimoni. Watu wanaushahidi wa wizi na uporaji wa rasilimali za serikali, wakienda mahakamani mahaka ni ya CCM, sasa kilichobaki ni hukumu ya wananchi. Wewe wasubiri 2015 moto utawaka!
MWANASIASA mkongwe nchini Kingunge Ngombale - Mwiru ameibuka na kuwataka wenye ushahidi na watu wanaodaiwa kuwa mafisadi wautoe hadharani
"Tuache kupakaziana maneno mabaya kama ufisadi kwani neno hilo lina maana mbaya kuliko inavyodhaniwa na iwapo kuna mtu ana ushaidi na matendo ya ufisadi ya mtu ni bora ayatoe hadharani na kutoa ushahidi kulio kuendelea kuchafuana kwa kuitana kila kukicha mafisadi" alisema Kingunge.
Mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini alisema hayo wakati akizungumza katika mkutano maalumu ulioandaliwa na CCM Wilaya ya Bagamoyo ambao pamoja na mambo mengine ulilenga kuimarishaji chama hicho wilayani humo.
Kingunge alisema hivi sasa imekuwa ni tabia kwa baadhi ya viongozi wakiwamo wa dini na wanasiasa kutumia majukwa yao kuwavunjia heshima viongozi waliopo madarakani kwa kuwaita mafisadi huku wakiwa hawajui hata maana halisi ya neno hilo.
Alisema viongozi hao wanadhani kuwapo kwa mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kutoa maoni hapa nchini ni kuruhusu watu kutokuwa na adabu kwa wenzao dhana ambayo alisema si sahihi na hivyo alishauri iachwe mara moja.
"Hili ni jambo lisilowezekana hata kidogo kiongozi anachaguliwa na wananchi halafu wanatokea baadhi ya watu wanamvunjia adabu kiongozi huyo, mimi nadhani huko ni kuwatukana wananchi na hakukubaliki katika mahala popote", alisema Kingunge na kuongeza:
Akizungumzia suala la udini lililoshika kasi hivi karibuni, Kingunge alisema Watanzania wanapaswa kusimamia maadili yao waliyozoea tangu enzi za mababu kwani wapo baadhi ya wanasiasa na viongozi wa dini ambao wamefilisika kimawazo na hivyo wamekuwa wakitumia udini kutaka kuwagawanya wananchi.
Source: http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/21744-kingunge-awafyatukia-wanatamka-ufisadi
Fikra zangu:
Nadhani huyu mzee yupo ICU kiakili na mawazo. Na hii ndiyo inayopeleka CCM shimoni. Watu wanaushahidi wa wizi na uporaji wa rasilimali za serikali, wakienda mahakamani mahaka ni ya CCM, sasa kilichobaki ni hukumu ya wananchi. Wewe wasubiri 2015 moto utawaka!