Hamduni
Senior Member
- Apr 25, 2020
- 155
- 108
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ametembelea kaburi la hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na kusema ni mwanamapinduzi wa kweli na shujaa wa Afrika.
Amesema wakati Tanzania ikiadhimisha siku ya mashujaa, Mwalimu Nyerere anabaki kuwa shujaa namba moja wa Tanzania.
Kanali Mstaafu Kinana ameyasema hayo leo Julai 25, 2023 baada ya kutembelea kaburi la Mwalimu Nyerere Butiama mkoani Mara akiwa katika ziara kukagua uhai wa Chama, utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuzungumza na wanachama mkoani hapa
Akiwa katika kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na baada ya kuweka shada la maua, Kinana amemwelezea kuwa ni shujaa wa Tanzania na Afrika na kutoa wito kwa nchi zinazotamani kuzikalia nchi nyingine kiuchumi kuiga mema ya baba wa Taifa ambaye aliongoza mapambano ya kumaliza udhalimu wa nduli Idd Amin nchini Uganda.
#SautiYaMwenezi
#CCMImara
#Kaziiendelee
Amesema wakati Tanzania ikiadhimisha siku ya mashujaa, Mwalimu Nyerere anabaki kuwa shujaa namba moja wa Tanzania.
Kanali Mstaafu Kinana ameyasema hayo leo Julai 25, 2023 baada ya kutembelea kaburi la Mwalimu Nyerere Butiama mkoani Mara akiwa katika ziara kukagua uhai wa Chama, utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuzungumza na wanachama mkoani hapa
Akiwa katika kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na baada ya kuweka shada la maua, Kinana amemwelezea kuwa ni shujaa wa Tanzania na Afrika na kutoa wito kwa nchi zinazotamani kuzikalia nchi nyingine kiuchumi kuiga mema ya baba wa Taifa ambaye aliongoza mapambano ya kumaliza udhalimu wa nduli Idd Amin nchini Uganda.
#SautiYaMwenezi
#CCMImara
#Kaziiendelee