Hamduni
Senior Member
- Apr 25, 2020
- 155
- 108
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa ziarani Mkoa wa Mara tarehe 25, Julai amemtembelea Jenerali mstaafu David Musuguri Nyumbani kwake Butiama mkoani Mara ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Mashujaa nchini.
Ndugu Kinana akiwa Nyumbani kwa Jenerali Mstaafu Musuguri amesema amepita hapo ikiwa ni siku ya Mashujaa nchini lakini pia kuchukua Baraka akiwa anaendelea na Ziara yake ya Ukaguzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025.
"Ikiwa leo ni siku ya Mashujaa nchini moja ya shujaa aliyeliongoza Taifa katika Vita ya Idd Amin nchini Uganda ni Jenerali Msuguri. Yeye mbali ya kuliongoza Jeshi kwa miaka nane ameitumikia kwa miaka 50 hii ikiwa ni ishara ya ushujaa, ukombozi na uzalendo".
"Nikiwa Ziarani kikazi Mkoani Mara nimepita nyumbani kwake Butiama ili kuchota Baraka za shujaa huyu wa Taifa la Tanzania na nchi nyingine zilizokombolewa na Tanzania" alisema Kinana.
Katika ziara hiyo Makamu Mwenyekiti ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Sophia Edward Mjema.
#SautiYaMwenezi
#CCMImara
#KaziIendelee
Ndugu Kinana akiwa Nyumbani kwa Jenerali Mstaafu Musuguri amesema amepita hapo ikiwa ni siku ya Mashujaa nchini lakini pia kuchukua Baraka akiwa anaendelea na Ziara yake ya Ukaguzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025.
"Ikiwa leo ni siku ya Mashujaa nchini moja ya shujaa aliyeliongoza Taifa katika Vita ya Idd Amin nchini Uganda ni Jenerali Msuguri. Yeye mbali ya kuliongoza Jeshi kwa miaka nane ameitumikia kwa miaka 50 hii ikiwa ni ishara ya ushujaa, ukombozi na uzalendo".
"Nikiwa Ziarani kikazi Mkoani Mara nimepita nyumbani kwake Butiama ili kuchota Baraka za shujaa huyu wa Taifa la Tanzania na nchi nyingine zilizokombolewa na Tanzania" alisema Kinana.
Katika ziara hiyo Makamu Mwenyekiti ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Sophia Edward Mjema.
#SautiYaMwenezi
#CCMImara
#KaziIendelee