Kinana kugombea ubunge Arusha mjini

Kinana kugombea ubunge Arusha mjini

ata aje Jk....asipo tumia pesa na jeshi awezi chukuwa jimbo la arusha!!
 
Unaweza kumuita jembe huyo mwizi? nadhani kuna matatizo hapoo
 
wana arusha wamemchoka sana lema

Wewe kaongelee ya kwenu huko Bukoba na siasa zenu za uoga,sisi wakazi wa Arusha tunampenda mbunge wetu Lema,na kama ccm wana fikra ilibidi wamuweke mtu safi kuliko huyo Kinana na kashfa zake.Kwa Arusha ccm wanawe mikono.
 
CCM akiwekwa na samba au fisi mla watu watu watachagua Simba au fisi mla watu. CCM bye bye na si Arusha tu homa itaenea pia mikoa au kanda zingine. Demography will decide soon very soon!!! CCM itabaki kuwa chama cha upinzani!!
 
Si alitolewa kwa kutokuwa na sifa kisheria....na sasa atakuwa hana sifa kibao ikiwepo ya kimaadili.

Alimaliza muda wake na uchaguzi uliofuata hakuchukuwa za kugombea,tena ubunge.Hilo la kutolewa kwa kutokuwa na sifa ni lako.
 
Aliwekewa pingamizi kwenye TUME ya UCHAGUZI na aliyekuwa mgombea wa Ubunge kupitia NCCR-Mageuzi Makongoro Burito Nyerere kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 kuwa Kinana SIO RAIA wa Tanzania!Kinana alikuwa Waziri wa Ulinzi kwenye serikali ya 1990-95 ya Mzee Mwinyi!

Kabla pingamizi haijaanza kusikilizwa KINANA akajitoa kwenye uchaguzi huo na kupelekea Makongoro kushinda kiurahisi sana!Makongoro aliwaambia waandishi wa habari kuwa USHAHIDI ALIO NAO Kinana hawezi pona!Je karekebisha mambo yake sasa ni raia?


Anaweza akawa hajarekebisha uraia wake, lakini kwa ccm kuongozwa na wageni ni uwekezaji na sera yao inaruhusu. yawezekana kuwekeza akili kutoka nje kama mnadhani hamuwezi, ndo maana mambo chini ya ccm ni shaghala baghala tu bora maisha kwa kila mbongo. Marehemu mwalimu JKN alishashasema kuwa aliowaachia nchi wako radhi kuwekeza kila kitu kwa wakubinafsisha kwa wageni au watu binafsi, akasema anangojea serikali na magereza na polisi navyo viwekezwe.
 
Mojawapo ya kashfa iliyomtoa Arusha 1995 ni mashine za kufulia nguo za wagonjwa Mount Meru Hospital. Kama amezirudisha atashinda ila kama siyo, wala asijidanganye.
 
kwa Arusha hata CCM wakimsimamisha Barack Obama hawawezi kuishinda CHADEMA kamwe.
 
na akipata ubunge atateuliwa kuwa waziri wa mali asili na utalii...., ndan ya mwaka mmoja tembo hatunao tena.
 
Back
Top Bottom