Nafikiri tatizo la hawa watu liko kwao wenyewe..
Wamezungukwa na mitaji hawatumia..mfano mashamba na mifugo
Kama mmasai ana ng'ombe 100 hataki kujenga, kuvaa na kula vizuri utamfanyaje?
Katibu Mkuu wa CCM, ABDULRAHMAN KINANA amewataka wananchi kuwapuuza wapinzani kwa vile si wakweli. Kwamba, Wapinzani wamekuwa wakipinga kila kitu kinachofanywa na serikali na chama tawala hata kama kitu hicho kiko wazi na wananchi wanakifahamu. Kinana ameyasema hayo huko Ifunda wakati wa Ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM. Aidha, amewataka wananchi wa jimbo la Kalenga kumchagua mbunge atakayeteuliwa kugombea kwa tiketi ya ccm ili aendeleze mazuri yaliyofanywa na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo na ambaye pia alikuwa waziri wa fedha, marehemu Mgimwa.
Source, Star TV Habari za Adhuhuri
Halafu hizo sura mbona hazifanani na za kitanzania?Nguo zilivyo nyingi duniani na hata Mitumba kibao na kwa bei chee, ila bado mtu hawezi kumvalisha mtoto wake?
Yaani hata Majirani hawawezi kumpa huyu kijana nguo ili asininginize MALI zake nje?
Hii inauma sana aisee. Tanzania haitakiwi kabisa mtu atembee uchi wa MNYAMA.
SHAME ON YOU KINANA na wenzako wote mnaopiga propaganda wakati mkiishi peponi na kuwaacha hawa UCHI.
Halafu hizo sura mbona hazifanani na za kitanzania?
Mkuu, wananchi makini wameshazinduka na sasa hawasikilizi tena udaku wa CHADEMA
Ni kweli kabisa huwezi kumpuuza mtu anayekuja kwako na kukuambia una njaa wakati kweli una njaa lakini vile vile utamshangaa sana huyu mtu akikuambia tu kuwa una njaa wakati unafahamu tayari kuwa una njaa lakini kikubwa kabisa, utamshangaa sana akisema na kuondoka bila kukuelezea njia ambayo yeye imemfanya akagundua kuwa una njaa na pia njia za kukufanya usipate njaa tena.Sioni kama itakuwa rahisi kwa wananchi kupuuza ukweli wanao uona, ukweli kuhusu maisha yao. Unaweza ukawa una njaa mtu akaja kukuambia una njaa ukampuuza kweli? Sidhani kama ni rahisi hivyo hayo anayosema huyo mtu,
Nani kawatapeli watanzania hawa? Ni chadema?
Katibu Mkuu wa CCM, ABDULRAHMAN KINANA amewataka wananchi kuwapuuza wapinzani kwa vile si wakweli. Kwamba, Wapinzani wamekuwa wakipinga kila kitu kinachofanywa na serikali na chama tawala hata kama kitu hicho kiko wazi na wananchi wanakifahamu. Kinana ameyasema hayo huko Ifunda wakati wa Ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM. Aidha, amewataka wananchi wa jimbo la Kalenga kumchagua mbunge atakayeteuliwa kugombea kwa tiketi ya ccm ili aendeleze mazuri yaliyofanywa na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo na ambaye pia alikuwa waziri wa fedha, marehemu Mgimwa.
Source, Star TV Habari za Adhuhuri
Kinana ni Jemedari. Anaongea ukweli daima na haogopi mtu. Big Up sana. 2015 wataisoma namba
Kama una hoja ya maana unaweza kumpuuza. ila kama huna hoja endelea kuumia tu
Mkuu, wananchi makini wameshazinduka na sasa hawasikilizi tena udaku wa CHADEMA
Mkuu, kwenye hiyo mikutano si kila anayeenda ni mwana chadema. Kuna wana ccm kibao ambao wapo kistrategy zaidi