Kinana aunguruma Sumbawanga, sasa hivi...!

Kinana aunguruma Sumbawanga, sasa hivi...!

Hahahaha hata Mijusi ya Kisomali inakuja kuunguruma Tanzania! Hizi ni staajabu za Abunuwasi
 
Mwambieni aache kuangamiza Tembo wa Tanzania kwa Meno yao! Arudi Somalia enough is enough
 
Hili neno Mheshimiwa sasa linatumika vibaya.

Ama tulifute kabisa kulitumia au tupeane semina elekezi nani anastahili kuitwa hivi

mwalimu Nyerere alikataa kuitwa hayo majina uheshimiwa.
 
wale viongozi wako wa vyuo vikuu kwa miaka mitano hujamaliza kuelezea.

huyu kinana mwambie mzigo wa pembe za ndovu unaozea kule china.
wachina anaowafukuza wamepewa kibali na serikali ya china.

kuhusu barabara umekuwa wimbo utachuja sasa hivi.
 
MKUU hapa naona kuna kutokuelewa maana ya "... Chama tawala CCM kuisimamia serikali yake...". Katibu mkuu KINANA hana mamlaka ya kuiagiza serikali, kwa kisingizio cha chama kusimamia serikali. CCM kuisimaia serikali siyo kupitia mtu mmoja mmoja, bali vikao:mkutano mkuu, NEC & CC, hivi vina mamlaka ya kuisimamia serikali siyo KINANA mkuu, tunapaswa kuelewa hili. Jambo hili ni sawa na BUNGE kusimamia serikali: MBUNGE mmoja mmoja hana mamlaka ya kutoa maagizo kwa serikali, bali MBUNGE (SOMA IBARA 63 ya KATIBA TZ 1977).

NAKUMBUKA alipoingia Sec Gen MKAMA naye alizunguka nchi nzima na kutoa ahadi "mpya kabisa" na kukoromea serikali, aliitwa na kuambiwa anakosea na akapotelea kusikojulikana. MOJA ya ahadi za MKAMA ni kujenga hospitali ya RUFAA eneo la Kwangwa MUSOMA , yenye pia na chuo kikuu cha afya kama MUHIMBILI, MJINI MUSOMA, na akasema isipojengwa hadi 2015 basi CCM isichaguliwe ... TUNASUBILIA TUONE. KINANA naye anapita mle2, haya bwana: naona hawajajua kuwa CHAMA KUSHIKA HATAMU ILISHAKWISHA ZAMAAAAAAAAAAAAANI ...

Unakosea na unasahau nafasi ya Kinana katika Chama Cha Mapinduzi.,maagizo ya vikao vya chama, mkutano mkuu wa chama na sekretarieti zinaratibiwa na huyo bwana nae ndie mwenye wajibu wa kuyasema na kuyabeba maagizo ya Chama kwa serikali, lakini pia kuwaeleza wananchi maagizo hayo ya Chama kwa serikali na pia kuwaeleza serikali bayana kuwa maagizo hayo ni lazima yatekelezwa kama yalivyoainishwa katika ilani na sera za CCM.

Mind U.,maagizo haya si ya Kinana, na ndio maana katika kauli yake ameeleza bayana kuwa " " Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" akimaanisha kuwa hayo ni maagizo yanayotokana na CCM wala si kinana kama yeye. Bahati mbaya ya walio wengi ni kuwa wanashindwa kuielewa nafasi ya Chama Kwa serikali na nafasi ya serikali kwa wananchi...!
 
Nimerudia takribani mara nne kuisoma hoja hii naona kunamgongano wa kimadaraka.

Msimamizi mkuu wa chama ameingia mojakwamoja kutenda majukumu ya mawaziri bila kufuata taratibu za kiprotocal na nani afanye nini na kwanini.

Muda si mrefu magufuri na wenziwe watakuwa na wakati mgumu kutekeleza majukumu yao maana watakuta kinana kapita kila kona ametoa maelekezo na sizani

anayoyatolea maelekezo yote yamo ndani ya ilani kiasi kwamba isiwachanganye as a point of reference.

Naiona hoja ya Mgema ukimsifia tembo hulitia maji.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe. Abdurahaman Kinana anazungumza katika wilaya ya Sumbawanga Mjini ambako amezungumzia juu ya suala la kero za Usafiri na Barabara, ambapo amesema tayari serikali imeshatenga fedha ya kutosha kwa ajili ya barabara hiyo ambapo tayari baadhi ya makandarasi wanaendelea na ujenzi wa makaravati tayari kwa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Pia Mheshimiwa kinana amezungumza juu ya suala la Uhifadhi wa mazingira ambapo amewataka wachina ambao wanaendesha zoezi la uchimbaji wa madini katika mbuga ya katavi kuondoka mara moja katika hifadhi hiyo na kusisitiza kuwa suala la uhifadhi wa mazingira ni jambo muhimu na kimsingi linaendana na siasa ya CCM ya kupambana na umasikini, alisema " Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" alimalizia kueleza kuwa Mazingira ni nyenzo muhimu ya maendeleo na suala mtambuka, ambalo linagusa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Kisha Mheshimiwa Kinana alizungumza juu ya suala la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea hasa kutokana na rasilimali zetu akisisitizia zaidi juu suala la kilimo na utekelezaji wa sera ya kilimo kwanza. Akahimiza vijana kuchakalika na kutumia kikamilifu fursa ya kijiografia ya sumbawanga ambapo hupata mvua nyingi na ya kutosha.

Hivi sasa Mheshimiwa Nape Nnauye, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya itikadi na Uenezi anashambua jukwaa...,updates zaidi hivi punde...!

Something is wrong here. Na hii inaweza kuifanya hii kitu iwe na upungufu wa ukweli na kuficha vitu fulani ambavyo vinasemwa na wengine hapa kuwa vimetokea huko kwenye huo mkutano...yaani Kinana alizungumza kabla ya Nape na Nape akazungumza baada ya Kinana au...just quizzical mind.

Sasa mkiwatimua Wachina nani atakuwa anazipokea zile pembe za ndovu au ndiyo mnaanza kulipa kisasi ili wasiendelee kuwaumbua. Mnawafukuza Wachina kwa maneno. Wamejiweka pale? Vipi wale Wamarekani mnaotaka kuwamilikisha karibu ardhi yote ya Katavi na Rukwa nzima katika mkakati mkubwa wa...kwa bei cheeee na wao wanapaswa kuondoka? Usanii bwana.

Naona maandalizi ya uchaguzi mdogo, eti ziara ya kukagua barabara.
 
Huyu kinana hamna kitu amewekwa pale na kina Lowassa kwa janja ya Mkapa ili kuichanganya Serikali na CCM.

Mawaziri wengi wameshamshtukia sasa, soon wataanza kumchamba.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe. Abdurahaman Kinana anazungumza katika wilaya ya Sumbawanga Mjini ambako amezungumzia juu ya suala la kero za Usafiri na Barabara, ambapo amesema tayari serikali imeshatenga fedha ya kutosha kwa ajili ya barabara hiyo ambapo tayari baadhi ya makandarasi wanaendelea na ujenzi wa makaravati tayari kwa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Pia Mheshimiwa kinana amezungumza juu ya suala la Uhifadhi wa mazingira ambapo amewataka wachina ambao wanaendesha zoezi la uchimbaji wa madini katika mbuga ya katavi kuondoka mara moja katika hifadhi hiyo na kusisitiza kuwa suala la uhifadhi wa mazingira ni jambo muhimu na kimsingi linaendana na siasa ya CCM ya kupambana na umasikini, alisema " Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" alimalizia kueleza kuwa Mazingira ni nyenzo muhimu ya maendeleo na suala mtambuka, ambalo linagusa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Kisha Mheshimiwa Kinana alizungumza juu ya suala la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea hasa kutokana na rasilimali zetu akisisitizia zaidi juu suala la kilimo na utekelezaji wa sera ya kilimo kwanza. Akahimiza vijana kuchakalika na kutumia kikamilifu fursa ya kijiografia ya sumbawanga ambapo hupata mvua nyingi na ya kutosha.

Hivi sasa Mheshimiwa Nape Nnauye, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya itikadi na Uenezi anashambua jukwaa...,updates zaidi hivi punde...!
katavi-and-mahale-national-park.jpg
P96WF00Z.jpg

Aberdares1.jpg
 
WANGEKUWA wanafanya hayo unayosema, sawa. TATIZO wana personalise, "nina... nita...". HAPO ndo nasema hawana mamlaka hayo, nashkuru nawe umekubali kuwa hawana mamlaka hayo, ni ya vikao vya chama CCM.

THEN, hata hivyo vikao havihusiani na watumishi wa umma ila vinapaswa KUPAMBANA NA JK peke yake, yeye ndiye waliyempa udhamini kugombea urais. SAWA HAPO. Hivyo ni kosa kutoa maagizo kwa "watumishi wa umma", hawa si watumishi wa CCM. WATUMISHI hawafanyi kazi at the pleasure of the CCM, JK ndiye anayefanyakazi at CCM's pleasure: wakiwa kwenye vikao hawamuajibishi, wanapiga tu amakofi, wakisha toka ndo "wanaagiza serikali ...", hilo halipo maana you cannot order which you cannot enforce...

Unakosea na unasahau nafasi ya Kinana katika Chama Cha Mapinduzi.,maagizo ya vikao vya chama, mkutano mkuu wa chama na sekretarieti zinaratibiwa na huyo bwana nae ndie mwenye wajibu wa kuyasema na kuyabeba maagizo ya Chama kwa serikali, lakini pia kuwaeleza wananchi maagizo hayo ya Chama kwa serikali na pia kuwaeleza serikali bayana kuwa maagizo hayo ni lazima yatekelezwa kama yalivyoainishwa katika ilani na sera za CCM.

Mind U.,maagizo haya si ya Kinana, na ndio maana katika kauli yake ameeleza bayana kuwa " "Moja kati ya malengo na maudhui ya CCM ni kuona kwamba matumizi ya utajiri wa taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa jitihada za kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi" akimaanisha kuwa hayo ni maagizo yanayotokana na CCM wala si kinana kama yeye. Bahati mbaya ya walio wengi ni kuwa wanashindwa kuielewa nafasi ya Chama Kwa serikali na nafasi ya serikali kwa wananchi...!
 
Ameeleza pia juu ya mwelekeo wa sera za CCM katika miaka ya 2010 hadi 2020, na kutoa ufafanuzi wa kutosha katika baadhi ya masuala muhimu yanayoigusa jamii hiyo likiwemo suala la ardhi.

Naona ameanza kampeni za uchaguzi mdogo wa Sumbawanga mapema. Aanafikiri wananchi watahadaika na hiyo barabara. Sumbewanga siyo ya miaka ile. Sasa hivi ukipita kila kijiji unakuta bendera za CDM ni nyingi kuliko CCM. Magamba hawana chao katika lile jimbo.
 
Katika maelezo yako yote sijaona alipounguruma zaidi ya kujipendekeza kuwaita waheshimiwa.
 
Kimsingi hakuna aliyejitokeza kupinga kuwa wale hawakuwa viongozi wa Chadema katika vyuo husika.,alichofanya makene ni kutaja majina ya viongozi wengine wakiwemo wenyeviti, makatibu, waenezi na watunza fedha na hakukanusha kuwa orodha ile si ya viongozi wa chadema vyuoni bali alisema miongoni mwao si wenyeviti bali hakusema si viongozi.,naomba ufahamu hivyo. Hakuna upotoshaji juu ya jambo hilo.
Unajikanyaga tu kwa sabbu lengo lako lilikuwa watu wahisi wote ni wenyeviti na wote ni wachaga, ni sawa na mpumbavu mmoja ajitokeze achukue majina ya mawaziri na manaibu wakristo tu aende kijijini wasiko na acces ya kujua mawaziri wa nchi hii tena kwenye hadhara ya waislamu na akaseme hii ndio serikali ya tanzania!! Unadhani atakuwa ametenda haki? Huna utetezi mi nakuona m2 wa hovyo tu..
 
Habari ya upotoshaji iliyoandikwa na 2MINE kwanini inaachwa.,mods wamesinzia..???
 
Huku ni sumbawanga, majira ya huku ni tofauti.,bado ni kweupe na mkutano unaendelea ila karibu utafungwa kwani hivi sasa anaongea mzungumzaji wa mwisho.

ahahahahaaaa. so tandaleone sumbawanga iko alaska. kweupee.
 
Back
Top Bottom