Akiongea kwa jazba,Ngombale alikaririwa akipinga kwanza,kuundwa kwa Baraza la ushauri ambalo litakua na viongozi wakuu wastaafu kwa maana ya marais na mawaziri wakuu wastaafu akidai hatua hiyo itafanya chama kikose watu wa kukilea japo haikueleweka alikua anamaanisha nini!
Pia bwana kingunge alipinga mpango wa kuzuia wabunge kujilimbikizia vyeo vinavyoambatana na posho pia kwa kuwa wajumbe wa NEC.Tayari wabunge pia ni madiwani katika halmashauri wanazotoka na wanahudhuria vikao kama kama madiwani wengine.
Kuhusu mpango wa kuzuia wabunge kuwa wajumbe wa NEC, Ngombale alisema, Huwezi kufanya haya kama unakitakia mema chama hiki. Labda kama mtakuwa mnathibitisha madai kuwa kuna agenda iliyojificha.
Akiongea kwa jazba kali bwana Ngombale alisema,
Naomba mniweke kwenye kumbukumbu kwamba nimelipinga jambo hili. akaendelea kufoka kwa kudai bila kuthibitisha kwamba utaratibu wa kupata wajumbe wa NEC kutoka wilayani eti utakuwa na athari kubwa kwa chama hicho kwenye siku za usoni; kwani utakifanya chama kuwa na makundi makubwa ya ugomvi na visasi!!!
Katika hali inayoonyesha kama walikua wamejipanga kabla ya bwana Ngombale kuchangia, Peter Serukamba , mjumbe wa NEC na mbunge wa Kigoma Mjini,nae alisimama na kupinga utaratibu mpya wa kutaka kuwaundia chombo maalum viongozi wakuu wastaafu na kuwatumia katika kukishauri chama.
Lakini hoja dhaifu za Peter akifuatiwa na Kingunge,zilizimwa na Mh.Abdulrahman Kinana aliyepigilia msumari wa mwisho kwa kueleza kuwa hata wastaafu wenyewe wamekubaliana na jambo hili. iweje nyie ndio mpinge kwa nguvu leo??
Huku akimuangalia rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Kinana alisema, Au siyo Mzee Mwinyi. Mwinyi aliitikia kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana.
.