Kinachosemwa na baadhi ya watu kuhusu makinikia na madini hakipaswi kupuuzwa

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,156
Kila naposikiliza au kusoma chambuzi za baadhi ya watu mashuhuri, wanasiasa, wanasheria na baadhi ya wasomi wenye maono chanya katika nchi hii mapigo ya moyo yanaongeza kasi yakiashiria woga wa kinachotabiriwa kutokea!

Ripoti ya Prof. Mruma imeamsha hisia za wengi kiasi kwamba mihemko imetawala kuliko mantiki. Nimemsikiliza Zitto Kabwe, Tundu Lisu, Benson Bana, na nimesoma baadhi ya chambuzi za wanasheria mbalimbali kuhusu mchanga wa madini na hawa wawekezaji wa kimataifa.

Kwa mujibu wa Rais na tume yake, ni kwamba tunaibiwa tena saana tu na kweli huo ndo ukweli na ndio uhalisia na wala si jambo geni na pia hata mtoto mdogo au mtu wa kawaida kabisa ukimuuliza kuhusu Tanzania kunufaika na madini atasema "tunanyonywa" tena hadi tone la mwisho.

Swala la kujiuliza, hivi ni kweli hawa wanyonyaji kina ACACCIA na wenzake ni wazembe kiasi hicho kuiba hadharani tena milango ikiwa wazi!? Hapa ndo kwenye mashaka makubwa!

Hawa kina ACCACIA mitaji yao wanadhaminiwa na kina WORLD BANK na IMF au mataasisi MAKUBWA ya wakubwa huko majuu ambayo ndo washinikizaji wakubwa wa watunga sera wetu! Hivi ni wazembe kiasi hicho cha kutopenyeza vipengere vinavyowalinda kwa lolote wanalolifanya kama MAGUFURI anavyotaka tuamini!?

Mapigo ya moyo yanaenda mbio kwa sababu naona kama tunaingia wazima wazima kwenye mtego kama yale ya meli ya samaki! Utawala wa sheria ni jambo linalohitaji umakini wa hali ya juu sana! Unapoingia mkataba na mtu (achilia mbali nchi au kampuni) masharti yamkataba lazima yaheshimiwe na unapotaka kuuvunja au kuingilia mkataba huo lazima ufanye tafakari ya kina sana kuona faida au hasara ya jambo hilo!

Watanzania tumeibiwa miaka mingi sana, kwa vile Rais ameamua kushughulika na hili la madini hapaswi kwenda moja kwa moja kwenye kukamata na kuzuia na kutuhumu moja kwa moja bali akae chini na tume zake wapitie kipengele baada ya kipingele halafu waje watwambie kwamba ni vipengere vipi vimekiukwa vinavyotupa nguvu ya kugombana nao hao mabwana WAKUBWA!

Hili litatusaidia sana kuepuka kuingia kwenye hasara ya kulipa fidia na kupoteza diplomasia ya nchi katika uwekezaji. Tusipokuwa makini, tutaingia hasara kubwa kuliko faida tunayoitarajia!

Rais afahamu kuwa si kila pongezi za wabungi na mawaziri hasa wa chama tawala zinatoka moyoni! Wengine wanapongeza tu ili waonekana wako upande wako!
 
Wewe sio mzalendo wa nchi hii hakianani wenzio tunahamasishwa kuwa wazalendo na tukaambiwa na AG kwamba kama tutalipishwa basi ni kwa watanzania wote na si mtu na mtu, hebu jifunze kuwa mzalendo bhanaa kama watakavyo baadhi ya wabunge wetu.
 
Nimekusikia Uncle Jei Jei .

Unaonaje tukisubiri mpaka kipengele cha mwisho ndipo tutoe hukumu. Sasa hivi watu wanabwabwaja dhidi ya ACACIA au serikali bila ya taarifa zote.

Hii ni haki kweli?
 
Nimekusikia Uncle Jei Jei .

Unaonaje tukisubiri mpaka kipengele cha mwisho ndipo tutoe hukumu. Sasa hivi watu wanabwabwaja dhidi ya ACACIA au serikali bila ya taarifa zote.

Hii ni haki kweli?

si haki kabisa na inazidi kutokuwa haki pale ambapo ACCACIA nao wanalalamika kutoshirikishwa na hizi kamati! Ukiangalia mikataba tuliyoingia inataka kila tunachofanya tuwashirikishe na wao....hapa hatutatoboa kama yatafika huko mbele! any way, tusubiri tu ila niliongelea wasiwasi wangu tu!
 
Kila naposikiliza au kusoma chambuzi za baadhi ya watu mashuhuri, wanasiasa, wanasheria na baadhi ya wasomi wenye maono chanya katika nchi hii mapigo ya moyo yanaongeza kasi yakiashiria woga wa kinachotabiriwa kutokea!

Ripoti ya Prof. Mruma imeamsha hisia za wengi kiasi kwamba mihemko imetawala kuliko mantiki. Nimemsikiliza Zitto Kabwe, Tundu Lisu, Benson Bana, na nimesoma baadhi ya chambuzi za wanasheria mbalimbali kuhusu mchanga wa madini na hawa wawekezaji wa kimataifa.

Kwa mujibu wa Rais na tume yake, ni kwamba tunaibiwa tena saana tu na kweli huo ndo ukweli na ndio uhalisia na wala si jambo geni na pia hata mtoto mdogo au mtu wa kawaida kabisa ukimuuliza kuhusu Tanzania kunufaika na madini atasema "tunanyonywa" tena hadi tone la mwisho.

Swala la kujiuliza, hivi ni kweli hawa wanyonyaji kina ACACCIA na wenzake ni wazembe kiasi hicho kuiba hadharani tena milango ikiwa wazi!? Hapa ndo kwenye mashaka makubwa!

Hawa kina ACCACIA mitaji yao wanadhaminiwa na kina WORLD BANK na IMF au mataasisi MAKUBWA ya wakubwa huko majuu ambayo ndo washinikizaji wakubwa wa watunga sera wetu! Hivi ni wazembe kiasi hicho cha kutopenyeza vipengere vinavyowalinda kwa lolote wanalolifanya kama MAGUFURI anavyotaka tuamini!?

Mapigo ya moyo yanaenda mbio kwa sababu naona kama tunaingia wazima wazima kwenye mtego kama yale ya meli ya samaki! Utawala wa sheria ni jambo linalohitaji umakini wa hali ya juu sana! Unapoingia mkataba na mtu (achilia mbali nchi au kampuni) masharti yamkataba lazima yaheshimiwe na unapotaka kuuvunja au kuingilia mkataba huo lazima ufanye tafakari ya kina sana kuona faida au hasara ya jambo hilo!

Watanzania tumeibiwa miaka mingi sana, kwa vile Rais ameamua kushughulika na hili la madini hapaswi kwenda moja kwa moja kwenye kukamata na kuzuia na kutuhumu moja kwa moja bali akae chini na tume zake wapitie kipengele baada ya kipingele halafu waje watwambie kwamba ni vipengere vipi vimekiukwa vinavyotupa nguvu ya kugombana nao hao mabwana WAKUBWA!

Hili litatusaidia sana kuepuka kuingia kwenye hasara ya kulipa fidia na kupoteza diplomasia ya nchi katika uwekezaji. Tusipokuwa makini, tutaingia hasara kubwa kuliko faida tunayoitarajia!

Rais afahamu kuwa si kila pongezi za wabungi na mawaziri hasa wa chama tawala zinatoka moyoni! Wengine wanapongeza tu ili waonekana wako upande wako!
watanzania inaonekana elimu ya International Trade iko chini sana, tutashitakiwa kwa sheria ipi? tutalipa shs ngapi? wanasema hawajawahi pata faida yaani wanaendesha kwa hasara kumsaidia mtu asipate hasara nalo ni kosa? akasia wenyewe wiki iliyopita walitangaza hasara ya us$1m kwa siku leo wanatangaza faida ya us$165m tuchukue lipi? wamelipana dividend ya us$ 35m, ukiwadai withholding tax tunaambiwa tutashitakiwa, haya mambo ya hovyo watanzania tunayatoa wapi?
 
Nimekusikia Uncle Jei Jei .

Unaonaje tukisubiri mpaka kipengele cha mwisho ndipo tutoe hukumu. Sasa hivi watu wanabwabwaja dhidi ya ACACIA au serikali bila ya taarifa zote.

Hii ni haki kweli?

si haki kabisa na inazidi kutokuwa haki pale ambapo ACCACIA nao wanalalamika kutoshirikishwa na hizi kamati! Ukiangalia mikataba tuliyoingia inataka kila tunachofanya tuwashirikishe na wao....hapa hatutatoboa kama yatafika huko mbele! any way, tusubiri tu ila niliongelea wasiwasi wangu tu!
 
watanzania inaonekana elimu ya International Trade iko chini sana, tutashitakiwa kwa sheria ipi? tutalipa shs ngapi? wanasema hawajawahi pata faida yaani wanaendesha kwa hasara kumsaidia mtu asipate hasara nalo ni kosa? akasia wenyewe wiki iliyopita walitangaza hasara ya us$1m kwa siku leo wanatangaza faida ya us$165m tuchukue lipi? wamelipana dividend ya us$ 35m, ukiwadai withholding tax tunaambiwa tutashitakiwa, haya mambo ya hovyo watanzania tunayatoa wapi?

hiyo hasara wametangaza hapa kwetu au huko UK!? kumbuka wanachovuna kinapelekwa na faida zote huko kwao!
 
si haki kabisa na inazidi kutokuwa haki pale ambapo ACCACIA nao wanalalamika kutoshirikishwa na hizi kamati! Ukiangalia mikataba tuliyoingia inataka kila tunachofanya tuwashirikishe na wao....hapa hatutatoboa kama yatafika huko mbele! any way, tusubiri tu ila niliongelea wasiwasi wangu tu!
huo mkataba unao?
 
Tatizo tuliowengi tunachangia hilihali hatuijui sheria ya uwekezaji n.a. sheria ya Madini zinasemaje akina msukuma n.a. lusinde wao wanatafuta kiki kwa jpm tusubiri hukumu ni swala la wakati tu
 
si haki kabisa na inazidi kutokuwa haki pale ambapo ACCACIA nao wanalalamika kutoshirikishwa na hizi kamati! Ukiangalia mikataba tuliyoingia inataka kila tunachofanya tuwashirikishe na wao....hapa hatutatoboa kama yatafika huko mbele! any way, tusubiri tu ila niliongelea wasiwasi wangu tu!

Uncle Jei Jei,
Uko sahihi bro.Tatizo la nchi hii ni Utawala huu wa CCM kwamba hawataki kukosolewa hata pale wanapoona chombo kinakwenda mrama! Huu ni ujinga! Mikataba yote ya madini kati ya SERIKALI YA CCM na ACACIA ilikuwa ni makubaliano ya pande zote mbili na kuna vipengele vinavyosimamia makubaliano haya(Terms and conditions)!!

Leo anapokuja mwana CCM awe ni Rais,Waziri,Mbunge au Mwenyekiti wa CCM anatoa povu kuwa Wapinzani wamehongwa, ni jambo halikubaliki wala haliingii akilini!Ni kuwafanya Watanzania kuwa wajinga na hawajui lolote!Hii si haki hata kidogo!!!!

Tayari ACACIA wameshakaa huko UK kuzungumzia hali iliyojitokeza Tanzania na jinsi ilivyoathiri biashara hii kwa pande xote 2! Tusubiri tamko lao la mwisho litakuwaje! Tanzanians have to think out of the box!!!
 
watanzania inaonekana elimu ya International Trade iko chini sana, tutashitakiwa kwa sheria ipi? tutalipa shs ngapi? wanasema hawajawahi pata faida yaani wanaendesha kwa hasara kumsaidia mtu asipate hasara nalo ni kosa? akasia wenyewe wiki iliyopita walitangaza hasara ya us$1m kwa siku leo wanatangaza faida ya us$165m tuchukue lipi? wamelipana dividend ya us$ 35m, ukiwadai withholding tax tunaambiwa tutashitakiwa, haya mambo ya hovyo watanzania tunayatoa wapi?
pum... kamuulize mkapa
 
Ujanja wa hawa jamaa pale panapokubana wewe katika mkataba waandika kwa maandishi madogo sana na wakati huo wameshakupa chakula na vinywaji na wanakupa vichesho ule muda unasoma, sasa hapo unajikuta hutaki juonekana zoba unatabasamu huku unaanguka na wino
 
Wewe sio mzalendo wa nchi hii hakianani wenzio tunahamasishwa kuwa wazalendo na tukaambiwa na AG kwamba kama tutalipishwa basi ni kwa watanzania wote na si mtu na mtu, hebu jifunze kuwa mzalendo bhanaa kama watakavyo baadhi ya wabunge wetu.
Avatar hiyo inaonyesha siyo miongoni mwa wazalendo tunaowahitaji.
 
Back
Top Bottom