Kinachopooza kampeni za Magufuli ni nini?

Kinachopooza kampeni za Magufuli ni nini?

Paul Alex

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2012
Posts
4,344
Reaction score
9,845
Kampeni ya Magufuli imekuwa ya kukatisha tamaa kwakweli, nilitegemea ingetoa angalau upinzani wa karibu kwa Lowassa lakini matamaanio hayo yanafifia kila kukicha.

Kwa mtazamo wangu, mambo yanayodhoofisha kampeni ya Magufuli ni:

1.Kukosekana kwa mtazamo chanya kwenye jukwaa: Magufuli hawapi watu moyo,anaogopesha kila mtu. kampeni imekuwa ya kulalamika sehemu kubwa na Magufuli amekosa Kuonyesha ujasiri wa kuwa rais baada ya tarehe 25 October.Ukiangalia jukwaa la Magufuli utaona watu waliokata tamaa tu.

2. Kukosekana kwa ubunifu: Ukiona mgombea anaongea kisukuma, anapiga pushap jukwaani,anaapa bila sababu unaona picha ya ndege anayehangaika ndani ya chumba chenye dirisha ila haoni pakutokea. Mbaya zaidi hana uzoefu wa kampeni level ya urais na hii inafanya akose cha kuiambia timu yake ya kampeni inapomfuata kwaajili ya maelekezo.Kuiga nembo ya M4C, wimbo wa mchaka mchaka na kaulimbiu ya mabadiliko ni alama tu za kukosa ubunifu.

3. Kukosekana kwa uaminifu: Magufuli mwenyewe anasema kuna watu wakonae mchana ila usiku wako UKAWA.Hii kauli inaonyesha kuwa team ya Magufuli ya kampeni hawaaminiani.Siri zote wanazopangilia zinachukuwa dk.5 tu kuwa kwenye mitandao ya kijamii.Hii inavunja moyo mno wale wenye nia ya dhati na Magufuli.

4. Tabia ya Magufuli kupenda kusifiwa peke yake.Unaposema Tanzania ya Magufuli una maanisha nini? Unapoita wenzako kwenye chama kunguni tukueleweje? Magufuli anataka aonekane yeye tu katika chama na hata kwenye mabango yake mengine hamna utambulisho wa chama.

Ujumbe kwa team campaign ya Magufuli: You could still make this loss less embarrassing, you could make it respectable.Don't panic, reorganize and address these very obvious issues.
 
Tatizo ni historia ya chama chake, chama chake kime litenda vibaya taifa hili hasa miaka 20 ilopita.
 
Kampeni za Magufuli zimejaa ulaghai, ahadi anazotoa kila kukicha hazitekelezeki ndiyo maana wapambe wake wanajazia kwa matusi na mipasho.
 
Magufuli ameona upepo huuu sio,anatamani kuachia kijiti ila oooooooooooh
 
Kuna kila dalili kuwa kwenye timu ya kampeni ya Magufuli, akili ndogo inaongoza akili kubwa.
 
Magufuli ameona upepo huuu sio,anatamani kuachia kijiti ila oooooooooooh
It is true, upepo wa kisiasa unamgeuka Magufuli kwa kasi ya kutisha na kwa sasa hauko upande wake kabisa.

Mfano halisi ni yale mapokezi aliyopata jijini Mbeya na wafuasi wa Ukawa hadi akalazimika kukiri kwa kinywa chake mwenyewe kuwashukuru wana Chadema kwa mapokezi yao makubwa kwake na kwa kumalizia kwa kusema Chadema Hoyeeeee......
 
Paul Alex

Anarudia ahadi za Kikwete za 2005 na 2010 ikiwa na maana kwamba hazikutekelezwa na yeye hategemei kuzitekeleza vilevile .CCM ni walaghai jamani hakuna mfano .ila this time wamepatikana mchana kweupe.watanzania walio wengi wameshawastukia ulaghai wao .waliobaki hawajastuka ni wachache sana au wale wanaoshirikiana na CCM kutuibia watanzania
 
Last edited by a moderator:
Ajabu hata sms za ukabila walizokuwa wanasambaza kwa wasukuma baadhi ya wasukuma wanaojitambua waliziponda sana na kusisitiza safari hii hawadanganyiki!
 
Kusema kweli anafurahisha jukwaa, atofautiani sana na kifimbo oyeeeee, kofia oyeeee, watz tujifunz kupiga tobo MTU anapoingia Anya zetu
 
…aamini hata yale anayoyasema ndo maana muda wote anajaribu waaminisha watu kwa haya maneno "mimi ni mkweli,nasema kweli,kweli kabusa"…utadhani anakula kiapo mahakani…
 
Hizo ndizo propaganda za kisiasa....mara zote propaganda ukaribia na ukweli au ukweli unaogusa (kumbuka binadamu yeyote mwenye dhamira ovu hapendi ukweli). I like your thread....umetumia akili kuwaambia wenye akili hapa jf....
 
Tatizo la kampeni za Makufuli ni kuwa watu badala ya kuongelea sera na ilani ya uchaguzi wanaongelea Lowassa. Ukiwasikiliza Nape, Makongoro, Mwakyembe na Bulembo hakuna cha maana wanachoongoea zaidi ya kupoteza muda wa kampeni kuzungumzia watu badala ya masulala. Kwa namna hiyo wamejikuta wanamtangaza zaidi Lowassa kuliko chama chao.
 
Paul Alex

5.LAANA YA PESA NYINGI ZITOKANAZO KODIZA WATaNZANIA KUTUMIWA KUHONGEA WASANII; NA KUWANUNUA WATU WAKAUDHURIE KAMPENI..

LAANA HII INAWALA CCM VIBAYA MNOOOOOOO
 
Last edited by a moderator:
Kama ungekuwa mpira wa miguu tungesema CCM wanacheza bila uelewano.
Kuna pande tatu ambazo huwezi kabisa kuelewa kama zinafanya kazi moja.

1.Kikwete : amecheza game yake peke yake na hakuna anayejua malengo yake, naweza kuweka hela bondi kuwa huweza hata yeye hayajui au hayo malengo hayapo kabisa.

2.Kuna chama : wengi wao ndio Magufuli anaita kunguni ambao kiukweli hawajui future yao katika chama, wengine toka wagombea wao waanguke hawajui waanzie mguu upi kutoka nje, wanaopiga kampeni wamekuwa kama walevi wanaokumbuka neno moja tu : LOWASA.

3. Kuna Magufuli : Yeye alitaka kutengeneza mchanganyiko wa pombe kali bila kujua njia, sasa kaweka whisky,wine,mbege,kiroba,bia,mafuta ya taa,ugoro na asprini kwenye glasi moja na hajui afanyeje tena!

Yaniiii, wanasema~ hapa kazi tu ! Na kweli kazi ipo.
 
We unaona mpaka waandishi wanafukuzwa, watu wasiogope mchezo
 
Bora ya magufuli anaeleweka jee huyo anayepoyeza kimbukuàmbu
 
Back
Top Bottom