Kimya Hiki, Is Not Right!, There Must Be Something Wrong Somewhere! Or Am, I Wrong!?

Janga la tetemeko ni la kustukiza sana, inawezekana kuna mambo anayafuatilia kimya kimya kuhusiana na mapokezi ya janga kama hili haswa kwa vikosi husika vinavyopaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanaathirika wanafarijika. Vinginevyo tusubiri kujulishwa.
 
Bila shaka nilisikia mtendaji mkuu wa shughuli zote za serikali alifika kwenye tukio husika ingawa sina uhakika Kama alitoa tamko lolote kwa wahanga.

Huu ukimya inawezekana ukawa unakuja na kitu kizuri kwa wahanga au kukawa kuna kitu kimeenda ndivyo sivyo.

Hakika wote hapa hatujui anachofikiria kwa kwa wakati huu. Cha msingi tuwe na subira huenda anajipanga aje.

Ingawa wakati mwingine subira huponza sana na ukiangalia wahanga wapo katika hatari kubwa sana.
 
Kuapishwa sio lazima picha ziwepo bana,mkuu yuko salama salimini anachapa kazi kama kawaida
 
Kwani ni kiongozi gani unaye mzungumzia ndugu yangu GT?
 
Siye wa darasa la pili tumeshafikiria labda sababu tulichagua wapinzani ambao kiafrika wanaitwa VIBARAKA,kwa hiyo ndiyo tunasomeshwa number.

Halafu tunanyooka maana hii baridi na mvua za baada ya Tetemeko si mchezo.Mbaya zaidi vile vibranketi tulivyopewa na Kibaraka mkuu wetu vimenyang'anywa ni shida,bora umeuliza labda Mzee wetu Mtukufu kabisa atakujibu
 
ifutwe ili ?tulia ikuingie
 
Uso umeumbwa na aibu kina Ruge mzee wa Escrow ndio wenye uwezo wa kuiponya Bukoba ndani ya dakika tu lakini umeshatangaza unataka waishi kama mashetani.

Mabalozi waliambiwa wasiingilie mambo ya ndani wanashangaa wameitwa jumba jeupe kuombwa msaada baba mwenye nyumba haonekani, na mkumbuke wenzetu wazungu ni watu wa kukeep record, bado wana kumbukumbu na walimsikia Baba mtukufu akitamba Tanzania hatutaki misaada, je hata wewe Pasco utaanza vipi kuwaface watu kama hao uliowatambia?

Maskini hana kiapo na Shabaan Robert alituhasa tuweke akiba ya maneno.

Yale mapesa ya MCC zaidi ya dollar millioni 800 tuliyapiga teke leo kumfuata mzungu kumuomba msaada inaweza kusababisha waanzishe research center ya kuzifanyia research akili zetu.

Cha msingi tuendelee kumuombea tu.
 
Kama ndivyo hivyo... basi asingekatisha ziara ya kukutana na wenzake Lusaka. Angeenda kwa amani kulitumikia taifa.

Kuahirisha safari kwa sababu ya maafa... afu bado kimya kikatawala hili ndo linapasua kichwa kwenye huu mjadala.

Kwanini kimya kwenye janga la kitaifa? Kuna tatizo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…