Bibi Ntilie
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 245
- 8
Huyu jamaa ni clean hata CCM-fisadi wakimwaga sumu hawatafanikiwa sana, hata kama atashindwa lakini atakuwa ameleta changamoto kwa siasa za baadae za tanzania.
Luteni, usisahau kwamba kuna heshima ya mtu at steak vile vile. Akishindwa kwa mara ya pili hata kama atakuwa ameleta changamoto yoyote ile huoni kwamba itakuwa imemvunjia heshima na rekodi yake nzuri? Kwa jinsi hali ilivyo sasa hivi SAS mtakuwa mnataka kumuumiza bure kutaka ajiingize kushindana na CCM iliyojaa ufisadi na mbinu chafu zisizojali utu wa mtu. CCM walimwaga sumu wakati ule wakafanikiwa watashindwa kumwaga sumu kali zaidi katika wakati huu ambao wako katika hali ya kutapatapa? Tafuteni vijana wazalendo wenye mwelekeo wa kutaka kulitumikia taifa kwa uadilifu ili wakapate nasaha na ushauri kutoka kwenye kisima cha busara za kila aina alichonacho kutokana na uzoefu wake wa siasa za ndani ya nchi na za kimataifa.