Kima cha chini kutangazwa mwezi ujao

Kima cha chini kutangazwa mwezi ujao

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,686
"Kwa muda mrefu tulikuwa hatujatangaza kima cha chini cha mshahara, lakini nafurahi kuwajulisha tu kwamba mwezi ujao tutatangaza rasmi,"alisema Kabaka.

Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote.

Akizungumza jana wakati wa mkutano kuhusu sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa Baraza Kuu la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), alisema kwa muda mrefukiwango cha kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote kilikuwa hakijabadilishwa.

"Kwa muda mrefu tulikuwa hatujatangaza kima cha chini cha mshahara, lakini nafurahi kuwajulisha tu kwamba mwezi ujao tutatangaza rasmi,"alisema Kabaka.

Pia alitahadharisha kuhusu utitiri wa vyama katika sehemu moja ya kazi kushauri waajiri wasiruhusu wafanyakaziwaanzishe kwa sababu vitakosa nguvu ya kujadiliana na mwajiri katika kufunga mikatabaya hiyari .

Waziri huyo alisema sekta ya hifadhi ya jamii ina idadi ndogo ya wanachama waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ukilinganisha na idadi ya nguvu kazi iliyopo ambayo ni milioni 22.

Awali Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Irene Isaka alisemahadi sasa michango katika mifuko hiyo imefikia Sh 1.4 trilioni nakwamba mafao yanayolipwa yamepandakutoka Sh500 bilioni hadi kufikia Sh 724 bilioni.

CHANZO: MWANANCHI
 
Afu wanakuja na elfu tatu mia nne selasini na sita, wakati expert analipwa sifuri sita na kazi mwafanya watz
 
Binafs siamini kabsa ongezeko la kima cha chini cha mshahara siku zote( around 15-20%) litabadili maisha ya mfanyakazi wa kawaida, tfdl wafanyakazi wa umma msifarijiane kwa ongezeko hili:crying:.
 
Tatizo mishahara hata ipande vipi haisaidii maana makato nayo yanapanda na bidhaa za madukani na vyakula navyo vinapanda bei.
 
Tangu lini Serikali yetu ikatangaza Neema
Imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei
ndiyo wataweza kuongeza Mishahara.

Serikali inatafuta mapato kwenye leseni
za Udereva & Bodaboda wakati makampuni
makubwa yanakwepa kodi yanatazamwa.

Nchi ya kusadikika,wameshindwa kupinguza
safari zisizo na lazima.
Matumizi ya mashangingi unadhani Mishahara
itapanda ili mvuja jasho anufaike?
 
"Kwa muda mrefu tulikuwa hatujatangaza kima cha chini cha mshahara, lakini nafurahi kuwajulisha tu kwamba mwezi ujao tutatangaza rasmi,"alisema Kabaka.

Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote.

Akizungumza jana wakati wa mkutano kuhusu sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa Baraza Kuu la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), alisema kwa muda mrefukiwango cha kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote kilikuwa hakijabadilishwa.

"Kwa muda mrefu tulikuwa hatujatangaza kima cha chini cha mshahara, lakini nafurahi kuwajulisha tu kwamba mwezi ujao tutatangaza rasmi,"alisema Kabaka.

Pia alitahadharisha kuhusu utitiri wa vyama katika sehemu moja ya kazi kushauri waajiri wasiruhusu wafanyakaziwaanzishe kwa sababu vitakosa nguvu ya kujadiliana na mwajiri katika kufunga mikatabaya hiyari .

Waziri huyo alisema sekta ya hifadhi ya jamii ina idadi ndogo ya wanachama waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ukilinganisha na idadi ya nguvu kazi iliyopo ambayo ni milioni 22.

Awali Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Irene Isaka alisemahadi sasa michango katika mifuko hiyo imefikia Sh 1.4 trilioni nakwamba mafao yanayolipwa yamepandakutoka Sh500 bilioni hadi kufikia Sh 724 bilioni.

CHANZO: MWANANCHI

Serikali hii pia imewasahau kabisa wasaafu na pensheni zao kwa kweli ni ndogo mno !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

 
Ukiondoa mishahara ya vigogo, mi naona watumishi wengi wa umma tayari mishahara yao ni kima cha chini.
 
Ivi mwaka jana mishahara si ilibadilishwa sasa anaposema ni muda mrefu anamaanisha nini? Siasa au wametambua ongezeko lao lilikuwa kiduchu sana? Wanazungumzia kima cha chini wakati ongezeko lolote linawanuaisha wa kima cha juu tu.
 
Back
Top Bottom