Kilimo cha miti, hasa Mitiki

Jan 12, 2014
10
1
Anayejua gharama za ulimaji mpaka uvunaji

Shamba lako lipo wapi. Gharama zinatofautiana kutokana na eneo ulipo. Nitakupa gharama ninazofahamu mimi kwa mahali nilipo.

1: Natumaini shamba unalo. Kama huna basi ekari moja ni 350k.
2: Kusafisha ekari moja, yaani kung'oa visiki, kukusanya na kuchoma moto uchafu wote ni 200k
3: Kulima kwa trekta (kukatua) kwa shamba jipya bei ni kuanzia 55k mpaka 65k. Si lazima lakini kama utapanda miti pekee.
4: Gharama za kuchimba mashimo na kuotesha miche kwa eka moja si chini ya laki 1 kutegemeana na makubaliano kati yako na kibarua lakini.
5: Mche mmoja unaanzia sh 300 hadi 500. Kutegemea na mazingira
6: Usafiri wa kuleta miche shambani andaa kitu kama elf 30 na kuendelea kitegemea na umbali lakini inaweza kuzidi hapo au kupungua
7: Kwa mwaka utapalilia mara 2 sawa na sh 80k zidisha mara 8 hadi 10. Baada ya muda huo nyasi zitakua ni chache sana maana miti itakua na ukubwa wa kutosha kutengeneza kivuli kingi na kusababisha kuzuia mimea mingine isikue
8: Utahitaji kila mwaka kukata matawi ya pembeni na kuacha moja linaloenda juu ili mti ukue haraka na unenepe pia. Gharama inaweza kuanzia 20k(makubaliano na kibarua). Lazima uwe na kifaa maalum cha kupunguzia matawi ili kuzuia mti kupata vidonda kwa ukataji mbaya wa matawi
9: Kuvuna ni kuanzia miaka 20 ili kupata faida kubwa zaidi. Chini ya hapo utavuna miti ambayo haina unene wa kutosha kutoa mbao. Unaweza kuvuna wewe mwenyewe au ukauza ikiwa shambani.

ANGALIZO
Kilimo cha mitiki ni uwekezaji wa muda mrefu sana. Usitegemee faida baada ya miaka 3. Hiyo ni ulinzi wako wa baadae. Thamani ya mbao haijawahi kushuka tangu mbao zimeanza kuzalishwa so tegemea faida nzuri tu baada ya muda mrefu lakini. Nakutakia kilimo chema. Nimekuwekea picha ya mitiki niliyopanda 2012.

View attachment 1233988
 
Shamba lako lipo wapi. Gharama zinatofautiana kutokana na eneo ulipo. Nitakupa gharama ninazofahamu mimi kwa mahali nilipo.

1: Natumaini shamba unalo. Kama huna basi ekari moja ni 350k.
2: Kusafisha ekari moja, yaani kung'oa visiki, kukusanya na kuchoma moto uchafu wote ni 200k
3: Kulima kwa trekta (kukatua) kwa shamba jipya bei ni kuanzia 55k mpaka 65k. Si lazima lakini kama utapanda miti pekee.
4: Gharama za kuchimba mashimo na kuotesha miche kwa eka moja si chini ya laki 1 kutegemeana na makubaliano kati yako na kibarua lakini.
5: Mche mmoja unaanzia sh 300 hadi 500. Kutegemea na mazingira
6: Usafiri wa kuleta miche shambani andaa kitu kama elf 30 na kuendelea kitegemea na umbali lakini inaweza kuzidi hapo au kupungua
7: Kwa mwaka utapalilia mara 2 sawa na sh 80k zidisha mara 8 hadi 10. Baada ya muda huo nyasi zitakua ni chache sana maana miti itakua na ukubwa wa kutosha kutengeneza kivuli kingi na kusababisha kuzuia mimea mingine isikue
8: Utahitaji kila mwaka kukata matawi ya pembeni na kuacha moja linaloenda juu ili mti ukue haraka na unenepe pia. Gharama inaweza kuanzia 20k(makubaliano na kibarua). Lazima uwe na kifaa maalum cha kupunguzia matawi ili kuzuia mti kupata vidonda kwa ukataji mbaya wa matawi
9: Kuvuna ni kuanzia miaka 20 ili kupata faida kubwa zaidi. Chini ya hapo utavuna miti ambayo haina unene wa kutosha kutoa mbao. Unaweza kuvuna wewe mwenyewe au ukauza ikiwa shambani.

ANGALIZO
Kilimo cha mitiki ni uwekezaji wa muda mrefu sana. Usitegemee faida baada ya miaka 3. Hiyo ni ulinzi wako wa baadae. Thamani ya mbao haijawahi kushuka tangu mbao zimeanza kuzalishwa so tegemea faida nzuri tu baada ya muda mrefu lakini. Nakutakia kilimo chema. Nimekuwekea picha ya mitiki niliyopanda 2012.

20191004_134917.jpeg
 
Asante kaka kumbe hekari 30 zitanitoa roho na mie ni kijana ndo natafuta hela

Anyway mie sihitaji hadi mbao siwez kuuza ikiwa na 5 yrs shambani ili nifanye mambo mengine
Shamba lako lipo wapi. Gharama zinatofautiana kutokana na eneo ulipo. Nitakupa gharama ninazofahamu mimi kwa mahali nilipo.........
 
Ili uvune mtiki ulio kama msitimu wa Umeme nafikiri inaweza ikafika miaka 70
 
Asante kaka kumbe hekari 30 zitanitoa roho na mie ni kijana ndo natafuta hela

Anyway mie sihitaji hadi mbao siwez kuuza ikiwa na 5 yrs shambani ili nifanye mambo mengine
Shamba lako lipo wapi? Unaweza kupunguza hizo gharama kwa kiasi kikubwa kwa kupanda mahindi kila msimu kwa miaka 3 ya kwanza hivyo gharama za palizi na prunning zitatoka kwenye uuzaji wa mahindi.

Mitiki ni hazina bora kuliko hata social security funds, unafanya kazi kwa miaka 30 unaishia kupata pension ya 200m wakati mitiki kwa miaka 20 unapata kwa eka 10 tu unakula 2bn, uamuzi ni wako.
 
Anayeitaji shamba zuri kwa ajili ya mitiki zipo ekari 25 pwani mbele ya msata,Kila ekari laki mbili na nusu,maeneo hayo miti hiyo inakubali Sana Kama morogoro na iringa
 
Shamba lako lipo wapi. Gharama zinatofautiana kutokana na eneo ulipo. Nitakupa gharama ninazofahamu mimi kwa mahali nilipo......


Mkuu blacksamurai nakushukuru kwa elimu yako je kwa uzoefu wako, naweza kufanya uwekekezaji kama huu maeneo ya Rufiji? Je kama eneo husika sio kwa kilimo cha miti, inabidi uombe kibali kutoka mamlaka yeyote?

Ahsante
 
Mkuu blacksamurai nakushukuru kwa elimu yako je kwa uzoefu wako, naweza kufanya uwekekezaji kama huu maeneo ya Rufiji? Je kama eneo husika sio kwa kilimo cha miti, inabidi uombe kibali kutoka mamlaka yeyote?

Ahsante
Mkuu blacksamurai nakushukuru kwa elimu yako je kwa uzoefu wako, naweza kufanya uwekekezaji kama huu maeneo ya Rufiji? Je kama eneo husika sio kwa kilimo cha miti, inabidi uombe kibali kutoka mamlaka yeyote?

Ahsante
Serokali inasisitiza kupanda miti.Panda panda hara rufiji yote.
 
Back
Top Bottom