Kilimo cha Bangi for export nchi zinazoruhusu itumike ili tukuze GDP

FRESHMAN

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
8,822
33,527
Habari wadau,

Nimeona kwenye tv watu wamekamatwa wanalima bangi mkoa wa Dodoma. Na nakumbuka nilionaga pia Tarime walikamata mashamba ya bangi hekari kibao.

Ninachojiuliza hivi kama bangi ina faida na ardhi tunayo kubwaaa.

Je, haiwezekani tukaweka mfumo mzuri wa kuruhusu ilimwe na kuuzwa nchi zinazoruhusiwa kama ina faida kubwa kimapato?

Na pia Tanzania ya viwanda nazani tungekomaa zaidi na viwanda vinavyoendana na kilimo tufanye agriculture revolution, yaani tulime mazao yote yanaokubali nchini kwa wingi sana na serikali iruhusu kuuza mazao nje hasa nchi jirani kama Congo, Zambia, Kenya au nchi yoyote bila taratibu ngumu, hii itasaidia kuleta hela nyingi za kigeni nchini.
 
Back
Top Bottom