Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,026
- 1,622
Baraza la Madiwani Halmshauri Siha Mkoani Kilimanjaro, limesema halipo tayari kuona bei ya maji ikipanda katika Wilaya hiyo na kusababisha usumbufu kwa Wananchi.
Msimamo huo umewekwa wazi, kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani kilichofanyika ukumbi wa Halmshauri hiyo, ambalo katika maswali ya hapo kwa papo Diwani wa Kata ya Kirua Samweli Mmar alihoji uamuzi wa bodi ya maji Lawate Fuka, kupandisha bei ya maji.
Akizungumza kwenye kikao hicho May 17 mwaka huu, Diwani Mmar amesema kuwa amepata malalamiko, Wananchi juu ya kupandishwa kwa bei ya maji kutoka shilingi 700 hadi shilingi 850 kwa uniti moja hali ambayo imeleta mtafaruka kwa Wananchi.
"Ni kweli jambo hili limeleta mtafaruku kwa Wananchi kupandisha bei mara kwa mara mwaka jana uniti moja ilikuwa inauzwa shilingi 700, lakini mwaka huu tena wanapandisha na kufika uniti shilingi 850 kwa kweli Wananchi wangu wameniletea hili jambo, " amehoji.
Diwani huyo haoni sababu za msingi zilizosababisha bodi hiyo kupandisha bei, na hasa ikizingatiwa kuwa miundombinu iliishajengwa na kwamba inatumia mfumo wa maji maji tiririka na hivyo kutokuwa na gharama kubwa za uendeshaji kiasi cha kupandisha bei bila ushirikishwaji wa wananchi.
Juma Jani Diwani wa Kata ya Sanya juu, amesema hao wanapandisha bei, wana mpango wa kuwachafua madiwani, na kwamba asingependa kuona wananchi wanaitisha mgomo kama ulioendeshwa na wafanyabiashara wa Kariakoo.
“Hatutaki kilichotokea Soko la Kariakoo, ambacho ndiyo kama hiki, kabla ya kwenda kwa Wananchi sisi tumekataa na hatupo Tayari, hatuwezi kuruhusu hili jambo,” amehoji Diwani huyo.
Kwa upande mwingine, Diwani wa kata ya Gararagua Zakaria Lukumay, amesema kama bodi imeshindwa kazi, ni vema wakaachia ngazi na siyo kuwasumbua Wananchi, Serikali inatuma fedha nyingi kwenye miradi hii na kwamba ankara wanazolipa wananchi, zinatosha kukarabati miundombinu kama imeharibika
Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Dancan Urasa, Amesema Baraza hilo halipo tayari kuona gharama za maji zinaongezeka na pia halihitaji Wananchi wapate usumbufu kwani mradi ni wakwao na wangeshirikishwa
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, ni Bodi ya Lawate Fuka ndiyo wanapandisha bei ya maji wakati wnzao wa Magadini na Makiwaru wao wameendelea kutoza bei ya zaman ya Sh700 kwa uniti.
Meneja wa Maji Safi na usafi wa Mazingira (Ruwasa), wilayani humo Emmy George, amesema utaratibu wa kupandisha bei upo, japo busara inatuma kuketi na jamii inayohudumiwa na mradi huu ili kukubaliana na bei pendekezwa.
Chanzo: Mwananchi
Msimamo huo umewekwa wazi, kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani kilichofanyika ukumbi wa Halmshauri hiyo, ambalo katika maswali ya hapo kwa papo Diwani wa Kata ya Kirua Samweli Mmar alihoji uamuzi wa bodi ya maji Lawate Fuka, kupandisha bei ya maji.
Akizungumza kwenye kikao hicho May 17 mwaka huu, Diwani Mmar amesema kuwa amepata malalamiko, Wananchi juu ya kupandishwa kwa bei ya maji kutoka shilingi 700 hadi shilingi 850 kwa uniti moja hali ambayo imeleta mtafaruka kwa Wananchi.
"Ni kweli jambo hili limeleta mtafaruku kwa Wananchi kupandisha bei mara kwa mara mwaka jana uniti moja ilikuwa inauzwa shilingi 700, lakini mwaka huu tena wanapandisha na kufika uniti shilingi 850 kwa kweli Wananchi wangu wameniletea hili jambo, " amehoji.
Diwani huyo haoni sababu za msingi zilizosababisha bodi hiyo kupandisha bei, na hasa ikizingatiwa kuwa miundombinu iliishajengwa na kwamba inatumia mfumo wa maji maji tiririka na hivyo kutokuwa na gharama kubwa za uendeshaji kiasi cha kupandisha bei bila ushirikishwaji wa wananchi.
Juma Jani Diwani wa Kata ya Sanya juu, amesema hao wanapandisha bei, wana mpango wa kuwachafua madiwani, na kwamba asingependa kuona wananchi wanaitisha mgomo kama ulioendeshwa na wafanyabiashara wa Kariakoo.
“Hatutaki kilichotokea Soko la Kariakoo, ambacho ndiyo kama hiki, kabla ya kwenda kwa Wananchi sisi tumekataa na hatupo Tayari, hatuwezi kuruhusu hili jambo,” amehoji Diwani huyo.
Kwa upande mwingine, Diwani wa kata ya Gararagua Zakaria Lukumay, amesema kama bodi imeshindwa kazi, ni vema wakaachia ngazi na siyo kuwasumbua Wananchi, Serikali inatuma fedha nyingi kwenye miradi hii na kwamba ankara wanazolipa wananchi, zinatosha kukarabati miundombinu kama imeharibika
Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Dancan Urasa, Amesema Baraza hilo halipo tayari kuona gharama za maji zinaongezeka na pia halihitaji Wananchi wapate usumbufu kwani mradi ni wakwao na wangeshirikishwa
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, ni Bodi ya Lawate Fuka ndiyo wanapandisha bei ya maji wakati wnzao wa Magadini na Makiwaru wao wameendelea kutoza bei ya zaman ya Sh700 kwa uniti.
Meneja wa Maji Safi na usafi wa Mazingira (Ruwasa), wilayani humo Emmy George, amesema utaratibu wa kupandisha bei upo, japo busara inatuma kuketi na jamii inayohudumiwa na mradi huu ili kukubaliana na bei pendekezwa.
Chanzo: Mwananchi