Kilichosababisha kocha Fadlu kuondoka Simba

Kilichosababisha kocha Fadlu kuondoka Simba

Think2

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2025
Posts
2,204
Reaction score
3,983
Kuna kiongozi mmoja wa Simba alimtisha kocha Fadlu Davids kuwa watamfukuza kazi kama Simba itakosa ushindi kwenye Mchezo wowote ule Ujao na kama timu haitocheza vizuri ndani ya mechi mbili zijazo.

Hili lilimfanya kocha huyo kuhisi kuwa kazi yake HAIKO SALAMA na kuhisi kuwa anafanya kazi na kiongozi ambaye hayuko professional . Alisikitika pia kwani alimuona kiongozi huyo sio mtu wa mpira kwani kauli zake hizo zilionesha kutokufahamu kuwa kocha kufungwa kufungwa mara nne mfululizo na timu flani sio jambo la ajabu katika soka (Fadlu alipoteza michezo minne mfululizo aliyocheza na Yanga) na kiongozi huyo hakuelewa kwamba Timu Kuanza mechi ya kwanza ya msimu kwa taratibu na tempo ya Chini ni jambo la kawaida sana katika soka.

Fadlu Davids alifanya Maamuzi ya Kuondoka Simba baada ya mazungumzo na kiongozi huyo na akamfahamisha Mo Dewji ambaye alimsihi sana asiondoke .Mo Dewji alimpa ofa ya kumuongezea mshahara Fadlu Davids lakini alikataa .

Soma Pia: Klabu ya Simba Sc yathibitisha kuachana na kocha wake mkuu Fadlu Davis Kwa matakwa yake Binafsi

Ni kama mambo yalifuatana kwani punde tu baada ya Fadlu kumaliza mazungumzo na kiongozi huyo wa Simba ,simu ya maboss zake Fadlu wa Zamani,Raja Cassablanca iliita ,walimuulizia uwezekano wa yeye kurudi Raja kama kocha Mkuu huku wakimpa mshahara mnono zaidi ya ule anaoupokea akiwa Simba ,pamoja na bonasi kibao pindi akiwapa Mafanikio miamba hao wa Afrika na Fadlu hakuwaza sana haswa Baada ya kukorofishana na kiongozi huyo na akawakubalia Raja bila wasiwasi.

Fadlu na Simba waliagana siku moja Kabla ya mchezo dhidi ya Gaborone United na walikubaliana kuwa kocha atasimamia mchezo huo na baada ya mchezo huo yeye pamoja na wasaidizi wake hawatarudi Dar Bali watabaki Afrika Kusini na Kuanza safari Kwenda Cassablanca.

Isingekuwa rahisi kwa Fadlu Kuondoka Simba eti kwa Sababu Raja Casablanca wamekuja kwake na Fedha kubwa hapana,Fadlu alipewa project ya Simba ya miaka miwili ama mitatu ijayo na Mo Dewji..Usajili uliofanyika dirisha lililopita aliusimamia yeye,Neo Maema ,De Reuck ,Sowah ,Antony Mligo ,Naby Camara ,wote hao wamekuja kwa mapendekezo ya yeye Fadlu Davids .Maema na De REUCK ni yeye aliwapigia simu waje Kusaini Simba Kwahyo Alikuwa na matumaini ya kuijenga timu tishio
 
Fadlu siyo kocha, ni mtumjanjamjanja tu, lakini hajui kufundisha mpira. Ndiyo maana kila siku aikuwa akidai apewe wachezaji wenye majinia badala ya yeye kuwatengeneza. Nimesikia kilichomuandoa siyo kichapo cha dabi bali ni kwa viongozi kushindwa kumleta Fei Toto.
 
Sio yule aliyemtuuhumu Camara kula rushwa wazi wazi mtandaoni?
 
Kuna kiongozi mmoja wa Simba alimtisha kocha Fadlu Davids kuwa watamfukuza kazi kama Simba itakosa ushindi kwenye Mchezo wowote ule Ujao na kama timu haitocheza vizuri ndani ya mechi mbili zijazo.

Hili lilimfanya kocha huyo kuhisi kuwa kazi yake HAIKO SALAMA na kuhisi kuwa anafanya kazi na kiongozi ambaye hayuko professional . Alisikitika pia kwani alimuona kiongozi huyo sio mtu wa mpira kwani kauli zake hizo zilionesha kutokufahamu kuwa kocha kufungwa kufungwa mara nne mfululizo na timu flani sio jambo la ajabu katika soka (Fadlu alipoteza michezo minne mfululizo aliyocheza na Yanga) na kiongozi huyo hakuelewa kwamba Timu Kuanza mechi ya kwanza ya msimu kwa taratibu na tempo ya Chini ni jambo la kawaida sana katika soka.

Fadlu Davids alifanya Maamuzi ya Kuondoka Simba baada ya mazungumzo na kiongozi huyo na akamfahamisha Mo Dewji ambaye alimsihi sana asiondoke .Mo Dewji alimpa ofa ya kumuongezea mshahara Fadlu Davids lakini alikataa .

Soma Pia: Klabu ya Simba Sc yathibitisha kuachana na kocha wake mkuu Fadlu Davis Kwa matakwa yake Binafsi

Ni kama mambo yalifuatana kwani punde tu baada ya Fadlu kumaliza mazungumzo na kiongozi huyo wa Simba ,simu ya maboss zake Fadlu wa Zamani,Raja Cassablanca iliita ,walimuulizia uwezekano wa yeye kurudi Raja kama kocha Mkuu huku wakimpa mshahara mnono zaidi ya ule anaoupokea akiwa Simba ,pamoja na bonasi kibao pindi akiwapa Mafanikio miamba hao wa Afrika na Fadlu hakuwaza sana haswa Baada ya kukorofishana na kiongozi huyo na akawakubalia Raja bila wasiwasi.

Fadlu na Simba waliagana siku moja Kabla ya mchezo dhidi ya Gaborone United na walikubaliana kuwa kocha atasimamia mchezo huo na baada ya mchezo huo yeye pamoja na wasaidizi wake hawatarudi Dar Bali watabaki Afrika Kusini na Kuanza safari Kwenda Cassablanca.

Isingekuwa rahisi kwa Fadlu Kuondoka Simba eti kwa Sababu Raja Casablanca wamekuja kwake na Fedha kubwa hapana,Fadlu alipewa project ya Simba ya miaka miwili ama mitatu ijayo na Mo Dewji..Usajili uliofanyika dirisha lililopita aliusimamia yeye,Neo Maema ,De Reuck ,Sowah ,Antony Mligo ,Naby Camara ,wote hao wamekuja kwa mapendekezo ya yeye Fadlu Davids .Maema na De REUCK ni yeye aliwapigia simu waje Kusaini Simba Kwahyo Alikuwa na matumaini ya kuijenga timu tishio
Sasa si umtaje tu ni yule jamaa mwili nyumba anayeitwa Magori! Yeye na mashabiki wengi wa simba lao ni moja. Wanafikiri mpira unachezwa mdomoni.
 
Sasa si umtaje tu ni yule jamaa mwili nyumba anayeitwa Magori! Yeye na mashabiki wengi wa simba lao ni moja. Wanafikiri mpira unachezwa mdomoni.
Kuna siku nitawataja wote hapa jf, kupoteza makombe ishu sio kocha kunawatu wanaihujumu simba kuwahonga wachezaji wacheze chini ya kiwango
 
Kuna siku nitawataja wote hapa jf, kupoteza makombe ishu sio kocha kunawatu wanaihujumu simba kuwahonga wachezaji wacheze chini ya kiwango
Halafu wakicheza chini ya kiwango anapata faida gani?
 
Hii Patrick Aussems aliwahi kuongelea. Hapo umbumbuni kuna viongozi hawana elimu.

 
Halafu wakicheza chini ya kiwango anapata faida gani?
jamaa huwa wana deal za kupiga hela za usajili,manake wachezaji wakihongwa wakacheza chini ya kiwango wataonekana si wachezaji wazuri,wamehongwa na wapinzani hivyo wamefungwa,wachezaji watafukuzwa na tajiri atatoa tena pesa ya usajili na mzunguko huo utaendelea. Ie mohamed hussein,aishi manula,ngoma, mavambo nk
 
Back
Top Bottom