Kilichonikuta huku kuangaika kwetu, tukitulizege

Bin wamakamo

Member
Dec 12, 2021
77
92
"Taratibu simu kiganjani naperuzi, nikiwa nimetulia zangu katika sofa, akili yangu haikuwa hata katika simu, hapo nina machungu na mahasira yamekaa katika koo toop, kila picha ya mdada iliyokuwa inajitokeza katika ukurasa wangu wa facebook nilikuwa nikiipita tu tena kwa speed kali sana, ni jana yake tu nimetoka kukataliwa mbele za watu tena nakuchambwa juu sasa bora angenichamba ningejiondokea zangu kulala lakini kweli mimi wakuniambia kichwa kama pieree rikwidii🥲

Yaani mwezi ulioisha nimetoka kuachwa tena nimeachwa kwa shughuli ndefu kama alivyooimba khalid chokoraa, nikaaiyona pisi imesuswa tu pisi kalii vijana hawana habari nayo angalau basi nifutie machozi kilichonikuta, kiukweli ilikuwa aibu yaani hata misele ikapungua😔


Basi bhana" moyo na nafsi acha zianze kuvutana,

Moyo akaanza choko choko "Kaka futa aibu usimuache kula sahani nae moja mie nakuaminia ukatagi tamaa" nikatikisa kichwa kushilia kweli swala la kukata tamaa kwangu uwa nadra sana.

Nafsi nayo ikaanza nasaha zake "Kaka usilazimishe kaka kama kakukataa achana nae kuwa lody music kaka kubali tu" nikabaki njia panda sijui hata nichukue ushauri wa nani?🙆


"Acha kumkatisha tamaa " moyo ukabwatuka🗣️

"Nisikie jamaa yangu, kwanza ukimpata cv zote zitarudi kwako, mtaa mzima utakuimba na lazima uonekane wnoma yaani ukipita tuu lazima usikie mwamba huyu hapa" yes nikaona moyo umegonga kwenye point mule mule🤔 kabla ya nafsi kuleta nasaha zake

"Kaka huyo anakupotosha uwezi jua mungu anakuepusha na nini kaka"

"Kuepushwa nini toka zako ,embu kwanza livutie picha toto likiwa kitandani si raha tupu mzee mwenzangu" ndiyo je rahaa maana kusema ukweli toto lilikuwa toto sio toto toto yaani toto😂 munataka nianze kusema ana guu la bia kalioo kama kachanjia macho ukiyatazama kakuibia, sio nianze ndo nawaambia hivyo😂

Nikayafata ya moyo na

Ya moyo matamu kwakweli aliyesema moyo usichanganye na mengine nani ni mnunulie choda,

Doria likaendelea wala siku choka, sijui kwanini kwenye kutafuta majaka ya moyo tuna kuwa mahodari sana, michambo ikaaendelea na mimi sikuchoka nishapewa bichwa tena na moyo mie sikati tamaa nimuangushe kwanini?


Jioni moja mvua za rasharasha zikiikung'uta ardhi nikasikia sauti nyororo ikibisha hodi, moyo ulini lipuka nani huyo maana sikuwa na demu wala sikuwa na miadi na mwanamke yoyote siku hiyo ,pisi niliyokuwa na ifukuzia ndo hivyo ilisha nitishia kuniletea mpaka polisi nikashindwa yakazinenga! , nikashusha pumzi nyingi sana kabla ya kuitika

"Karibuu" nikiuendea mlango , unajua nguvu zilinishia yaani sikuamini macho yangu nilichokiona, si ile pisi niliyokuwa naifukuzia wamakamo wenzangu, niliganda kama sekunde mbili nikiwa si amini ni macho yangu au niko ndotoni.

"Vipi mbona unashangaa" akani gandua

"Amna karibu karibu ndani pita tu" nikaongea kipupa na kufungua mlango vizuri binti akazama mpaka ndani, mie bado niko kwenye tafakali zito, nikiwaza kimemsibu nini leo kuja kwangu tena geto yaani mbuzi kafia kwa muuza supu, yasije yakawa ya husen machozi nikaona nimerogwa "Ila potelea mbali uchawi auendi kwa mentali"

Nikasema moyo acha ushangilie "Baba ua baba ua uwanja wako tena uwanja wa nyumbani" unani sisitiza,

Tukapiga sana soga kujitetea kukawa kwingi mara hakuwa akini amini sasa amethibitisha na yuko teyari kuwa na mimi, moyo ukasema woyoo "Piga kelele "Weuweeeee"

Ndovile tena mabusu mabusu yakawa meengi uzungu uzungu ukawa mwingi uzandu uzandu ndo usiseme, hata sitaki kuwaambia kuwa nilifahidi akuu , furaha ikawa tena, tena ungenikuta siku iyo we ungesema tu unakujwa kinywaji gani? Ela si unayo, alafu ungechagua kuosha vyombo au kwenda kupiga deki kwa mwenye kinywaji chake😂

Ilidumu furaha yenyewe😭 kuangaika kwetu huku tuulizege najuta.

"Dondolaa" niliitwa nikishikwa bega

Kugeuka ni mama mmoja wa mtaani ni mama ambaye tunaeshimiana sana "Hujamboo? Akasalimu "Sijambo mama shikamoo "Nikatoa heshima zangu kwa bashasha "Marhaba baba yangu " akaitika kisha kimya kikafuata "Kuna nini mama mbona unanisalimu unanitazama na uongei kitu nini shida" nikazungumza nikajua kama kawaida ya wamama muda mwengine maswahibu yakiwazidi uwafata vijana kuomba ushauri "Amna mwanangu ni wewe ndo unafanya natafakali sijui nianzie wapi kukwambia" ohoo macho yakanitoka hayo mambo gani tena haya ya kutaka kutongozwa na wamama lakini ngoja "Niambie tu mama usiogope mimi mwanao" nikazidi mdadisi "Mwanangu jana kuna msichana nimemuona anatoka ndani kwako, yule msichana ameathirika" nini macho yakanitoka zaidi kuathirika kupi kwanza nikajifanya kuto kuelewa "Kaathirika!

Nikauliza kwa msisitizo "Ndiyo kaathirika ana ukimwi wa kuzaliwa nao " akanijibu bila kupepesa macho "Sasa kuwa makini mwanangu" huyo akaondoka zake, nilihisi kuna kitu kinapanda kichwani alafu kinashuka miguuni jamani jamani , nilitaka kuhisi ni muongo lakini sikuwa na matani nae hata kidogo yule mama au ananitaka kiukweli hapana nilianza kudadisi nikagundua kuwa ni kweli, mengi yakaibuka kichwani ndomana mtaani hapakuwa na mtu mwenye habari nae loo hata kuniambia, kwaherini kwaherini migomigo sinza kwa herini, ikabidi nikapime sasa niko nasubiri majibu jasho linanitoka plesha iko juu daktari akaniambia niko salama sina maambukizi... Ooh asante mungu


Haya munitafutie demu sasa😅
 
unaona nn ww?
Muunganiko wa herufi mbalimbali zisizo na maana, au ulikua unajaribu kuunda neno na hatimae sentensi yenye maana ila kwa bahati mbaya umeshindwa??

Usijari, jirekodi sauti au video ukiwa unatoa huo ujumbe wako halafu tuma hapa. Kuna waandishi mahiri watakusaidia kufupisha na kuandika vizuri story ikaeleweka.
 
Back
Top Bottom