ITR
JF-Expert Member
- Sep 22, 2022
- 4,451
- 11,359
Jana kwenye mechi kati ya Simba na Singida tulishuhudia malumbano kati ya mlinda mlango wa Simba Ali Salimu na beki wa simba Che Malone baada ya kutokea kosa la kimawasiliano kati yao ambalo kidogo lisababishe goli.
Beki hata kama amekosea kuna namna nzuri ya kumkemea na kumuambia awe makini na sio staili aliyo itumia Ali Salimu jana ule ulikuwa ni udhalilishaji na sio kumkanya beki, cha kushukuriwa ni busara na ustaarabu uliopitiliza wa Che malone tofauti na hapo tungeshudia aibu ya mwaka ya wachezaji wa Simba wakipigana makonde mbele ya hadhara ya mashabiki na wageni rasmi.
Na mbaya zaidi ukijaribu kuangalia kwa umakini lile tukio ambalo kidogo lingesabsbisha goli kosa lilikuwa kwa Ali Salimu mwenyewe kwa kuwa mzito na kuchelewa kuufuata ule mpira aliokuwa ameachiwa na Malone.
Hebu fikiria Alichokifanya Ali Salimu jana angemfanyia mchezaji mwenye akili mbovu kama Kanote, Inonga au Nyoso sasa hivi huyo dogo si angekuwa Muhimbili na mashine za kupumulia akipambania maisha yake?
Huyu dogo inabidi atulize mapepe na ulimbukeni awe ajifunze kuwa na hekima na busara, asidanganywe na kifua chake ipo siku ataingia choo chakike.
Beki hata kama amekosea kuna namna nzuri ya kumkemea na kumuambia awe makini na sio staili aliyo itumia Ali Salimu jana ule ulikuwa ni udhalilishaji na sio kumkanya beki, cha kushukuriwa ni busara na ustaarabu uliopitiliza wa Che malone tofauti na hapo tungeshudia aibu ya mwaka ya wachezaji wa Simba wakipigana makonde mbele ya hadhara ya mashabiki na wageni rasmi.
Na mbaya zaidi ukijaribu kuangalia kwa umakini lile tukio ambalo kidogo lingesabsbisha goli kosa lilikuwa kwa Ali Salimu mwenyewe kwa kuwa mzito na kuchelewa kuufuata ule mpira aliokuwa ameachiwa na Malone.
Hebu fikiria Alichokifanya Ali Salimu jana angemfanyia mchezaji mwenye akili mbovu kama Kanote, Inonga au Nyoso sasa hivi huyo dogo si angekuwa Muhimbili na mashine za kupumulia akipambania maisha yake?
Huyu dogo inabidi atulize mapepe na ulimbukeni awe ajifunze kuwa na hekima na busara, asidanganywe na kifua chake ipo siku ataingia choo chakike.