Kili Marathon kugawa barakoa kwenye Mbio zitakazofanyika mwaka huu

Rahma Salum

Member
Sep 7, 2020
30
59
Kampuni ya Kilimanjaro Marathon inayoendesha Mbio maarufu za kila mwaka za “Kili Marathon” zinazofanyika Mkoani Kilimanjaro imetangaza kuwa kutakuwa na zoezi la ugawaji wa barakoa kabla na baada ya mbio kwa wakimbiaji wote wa mbio fupi na ndefu.

Vilevile wameeleza kuwa kutakuwa na kamati maalumu itakayokuwa inagawa vitakasa mikono kwa washiriki kwenye vituo maalumu, njiani mpaka mwisho wa mbio, na uwanjani kwa siku nzima ya mashindano. Watoa huduma wote katika vituo vya maji pamoja na uwanjani watavaa barakoa, gloves, aprons na watahakikisha wanatakasa mikono mara kwa mara muda wote wa mashindano

Wamesema hatua hiyo ni kutokana na wingi wa watu watakaoshiriki katika tukio hilo litakalofanyika Februari 28, 2021 Mjini Moshi. Mbio hizi zinafanyika huku kukiwa na madai ya COVID19 kuenea mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amekanusha madai hayo na kusema mkoa uko salama na magari ya maiti yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni kutoka mikoa mingine.

Pia soma

Kili Marathoni huhusisha ukimbiaji wa mbio fupi/nusu (half marathon) kwa umbali wa Kilomita 21.1 na ndefu/kamili kwa urefu wa Kilomita 42.2.
 
Marathon na barakoa! Sipati picha. Bora wangeahirisha tu.
 
Kwamba watu wakimbie hivi ?
IMG_20210217_145827.jpg
 
Si wahairishe tu?
Utakimbiaje na Mask?
Wataanza kuanguka kama kuku sasa.Maana hewa zitawaishia naturally tu.
 
Kampuni ya Kilimanjaro Marathon inayoendesha Mbio maarufu za kila mwaka za “Kili Marathon” zinazofanyika Mkoani Kilimanjaro imetangaza kuwa kutakuwa na zoezi la ugawaji wa barakoa kabla na baada ya mbio kwa wakimbiaji wote wa mbio fupi na ndefu.

Vilevile wameeleza kuwa kutakuwa na kamati maalumu itakayokuwa inagawa vitakasa mikono kwa washiriki kwenye vituo maalumu, njiani mpaka mwisho wa mbio, na uwanjani kwa siku nzima ya mashindano. Watoa huduma wote katika vituo vya maji pamoja na uwanjani watavaa barakoa, gloves, aprons na watahakikisha wanatakasa mikono mara kwa mara muda wote wa mashindano

Wamesema hatua hiyo ni kutokana na wingi wa watu watakaoshiriki katika tukio hilo litakalofanyika Februari 28, 2021 Mjini Moshi. Mbio hizi zinafanyika huku kukiwa na madai ya COVID19 kuenea mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amekanusha madai hayo na kusema mkoa uko salama na magari ya maiti yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni kutoka mikoa mingine.

Pia soma



Kili Marathoni huhusisha ukimbiaji wa mbio fupi/nusu (half marathon) kwa umbali wa Kilomita 21.1 na ndefu/kamili kwa urefu wa Kilomita 42.2.
Kwa hio watu watakimbia na mabarakoa?
 
Sijapata Logic ya kuvaa barakoa ambayo imeziba pua na mdomo huku ukiwa una trot/Jogging/ Kukimbia... vitendo ambavyo vinahusisha utoaji na uingizaji wa hewa nyingi kupitia mdomo,pua na mapafu

Anyways nisiwe msemaji sana.....


Tuendelee kujifukiza, barakoa, sanitizer, social distance, kuepuka misongamano na kutumia tiba asili


Au nasema uongo ndugu zangu? Mzaha sio mzaha...
 
Hii kitu kuna ulazima kufanyika kwa sasa wakati Corona imechachamaa? Naona kama wanalazimisha, marathon na barakoa wapi na wapi?!?
 
Ukikimbia huku umevaa barakoa unaweza kufa kwa changamoto ya upumuaji
 
Kuna sehemu niliwahi kusoma kwamba hairuhusiwi kufanya mazoezi ukiwa umevaa barakoa
 
Back
Top Bottom