Kile kipindi ambacho nilipotea

Nyamisati... dah umenikumbusha hapo sehemu tushapanda sana dau kwenda Mafia.. Maisha haya...
 
Nikiwa pale bandari bubu upande wa pili wa bahari nikamwona mtu mrefu sana akiwa kavaa kanzu nyeupe na kitambaa kichwani Chenye rangi nyeusi na nyeupe hiki kitambaa kilimfunika uso wote kasoro macho
Huyu mtu mrefu sana alikuwa anatembea kwenye tope kuja tulipo (kumbuka ilikuwa maji kupwa )mshangao wangu ulikuwa ni yule jamaa kutembea juu ya tope bichi bila kuzama na kanzu yake nyeupe
Ilibidi niwaambie wenyeji wangu wale vijana wala majani wakanicheka sana wakasema hakuna kitu kama hicho hayo ni maruerue tu ya 'bichi'
Sikutaka kuendeleza ubishani kwakuwa najua ila yule mtu mrefu alikuja na kutupita karibu kabisa...mimi nilimuona wengine hawakumuona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…