Kumekuwa na kawaida Katibu wa wabunge wa CCM kuitisha kikao cha dharula kila unapotokea mjadala mkali bungeni wa kuelekea kupinga hoja inayoletwa na serikali Bungeni. Matokeo ya kikao hicho ni aidha serikali kuiondoa hoja yake inapotokea wabunge wa CCM kuendelea kukataa kuiunga mkono katika kikao chao au wabunge wa CCM kukubali kuiunga mkono kwa msimamo mmoja. Hata leo baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu Mh Simbachawene alitangaza tangazo la Katibu wa wabunge wa CCM kutaka wakutane ni wazi ni juu wa sheria ya manunuzi vitu vilivyotumika. Hawawezi kukutana kabla ya kuupeleka Bungeni au wanakuwa wamekutana lakini wanabadilishwa na michango ya wapinzani na pili Utaratibu huu unawanufaisha kweli CCM kisiasa?