Kila akitongozwa lazima aniambie

Kila akitongozwa lazima aniambie

iphone 18 promax

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2012
Posts
2,917
Reaction score
2,142
Jamani nina mchumba wangu lakini kila akitongozwa lazima aniambie na hata akitumiwa sms lazima anitumie hivi ananipenda kweli au ndio sera ya wanawake wa siku hizi
 
subiri hiyo hali ndani ya mwaka kama itaendelea...ikiendelea nenda kaoe /kaolewe fasta:wave:
 
Unajua bhana wapenzi wa sasa wako flexible sana, yaani mtu inatokea anakupenda kiukwel lkn baada ya mda anakuona si lolote, akitongozwa anakwambia ili ujue kama: anakupenda, wenzio wanampenda pia, (yaani ni kama swaga flan za kujipaisha ivi!). Wengine wanadanganyatu, pia usisahau - atakuambia tu asiemtaka lkn kwa anaemtaka ....
Hivyo basi ukiambiwa hivyo na mpenzi wako, we chukulia kawaida tu, usijenge inference hapa. Kama anakupenda kweli au hakupendi utajua kwa mambo mengine..!
 
mwambie akwambie na anaowakubali .nipe namba yake nimtongoze niko sure awezi kukwambia sababu hao anaowakataa ni wanaume suruali tu.
 
Anakuonyesha bado ana market na ukimzingua hatochelewa kupata mwingine
 
Kila siku anatongozwa vp na we anakuletea taarifa kila siku? Kama hapana basi hao ni wale anaowapa kibuti tu.wake up!
 
Nakubaliana na wewe.
Akiavha kuwa anahadithia ujue kimeumana.

She is just an iinocent gal na hawezi kukuficha kitu. Wewe ndo ragiki yake na hata akipanga asiseme anajikuta anasema yu.
subiri hiyo hali ndani ya mwaka kama itaendelea...ikiendelea nenda kaoe /kaolewe fasta:wave:
 
Kama unampenda na kumjali mwambie asiwe ana-entertain kutongozwa...
Hatari zilizopo ni hizi;

1. Atakujengea hali ya wasiwasi haswa pale itapotokea kaacha kukupa michapo yoyote ya tongozo, binafsi nadhani hilo litakufanya uhisi kanasa katika moja ya mitego.

2. Inawezekana ni aina mojawapo ya kujihami na kukuonesha kuwa she/he still marketable.

Pamoja na hayo;
Huenda ni namna ambayo yeye kaona inafaa kuonesha uaminifu wake. Kumbuka huwa wanasema wapenzi hawapaswi kuwa wasiri.
 
Jamani nina mchumba wangu lakini kila akitongozwa lazima aniambie na hata akitumiwa sms lazima anitumie hivi ananipenda kweli au ndio sera ya wanawake wa siku hizi

anahimiza ndoa na kukuhabarisha kuwa kuna wengi wanamtaka
 
Jamani nina mchumba wangu lakini kila akitongozwa lazima aniambie na hata akitumiwa sms lazima anitumie hivi ananipenda kweli au ndio sera ya wanawake wa siku hizi

anatafuta namna ya kukufanya umuone kuwa yeye ni muaminifu, lakini ukweli ni kwamba uaminifu wa mtu huupimwi kwa kuonyeshana meseji za kutongozana, uaminifu ni tabia na ile hali ya kukataa na kuacha kujirahisi kutongozwa hovyo na kuepuka mahusiano ya kimapenzi nje na huyo mpenzi mmoja uliyenaye.
 
ukisema shida ucposema siku ukikuta sms nikikwmbia aliwahi kunitongoza unauliza kwnn sikukwmbia aaaaaaagh sa lipi jema kwenu
 
Akimpenda / akimhusudu mtu mwingine njiani atakwambia pia?
 
kawaida kwa mtu anayekupenda kwa 100%...ni kawaida kabisaa
 
Back
Top Bottom