Kikwete: Wanaokwepa Kodi hawataacha kirahisi, Magufuli endeleza mapambano

MOTOCHINI naona umekimbilia ku like naona hatimaye umesikia sauti ya mfadhili wenu
 
Naona anajibu tuhuma, itajulikana tuu mh. Rais mstaafu, sijawahi kuwaza hata kama uliwaruhusu useme uliwaruhusu, haitapata kutokea
 
Rais mstaafu wa JMT ALIYESHINDWA!!..Kama ningelikuwa mimi ningelijificha nisionekane kabisa!
 
Mzee umejuaje wakwepao kodi hawataacha? Labda ilikuwa kwako kwa Magufuli watasalimu amri tu, wewe fanya usafi acha kutukumbusha machungu ya mabilioni ya kodi zetu yaliyokuwa yanapotea siku kama ya leo.

Eti unamtaka Magufuli aendeleze vita dhidi ya wakwepa kodi na wala rushwa, kwani ilikuwepo?

Watanzania bwaana, huyo huyo jk mlimchagua kwa mbwembwe kama huyu magufuli ni muda mtakuja kula matapishi yenu
 
Anadai yeye, mkewe wala Ridhiwani hawajawahi kuagiza vitu viingizwe bila kodi, basi labda hajui ma dili ya mwanae. Achilia mbali Ridhiwani, marafiki wa Ridhiwani wakifika customs wanapiga simu kwa Ridhiwani, halafu wanawaambia customs hii mizigo ya Ridhiwani, mizigo inapita!

Kuna siku mzigo ulikuja customs jamaa wakasema mzigo wa Ridhiwani, TRA wakafungua mzigo. Weeeee... Mbona Othman Rashid na Said Mwema waliamshwa usiku wa manane kuja customs! Kisa, mizigo ya Ridhiwani imekaguliwa! Hivi mnadhani nyinyi wafalme?

Jilaumu wewe kwa kupoteza kura yako kumchagua huyo kuongozi
 
huyu jamaa anatamani kuendelea kukaa ikulu??? ni basi tu. katiba haimruhusu, alafu kama amestaafu si aende msoga akalee wajukuu nini kinamzungusha kwenye majukwaa ya kisiasa,

si alisema atalala usingizi mnono imekuwaje tena mara amwakilishe raisi kwenye mikutano ughaibuni, ataleta mgongano wa kiutendaji , ni akapumuzike tu kama watangulizi wake
 
Haaaahaaaa kaongea haya kasema mnapoteza muda kumuongelea hagombei tena

Nani alimsema eti akachomoe? Anakujibu kwani alichomeka

Duh ana maneno huyu
 
JK angewekea insurance mdomo wake kwasababu ukimpa mic tu,hakosi la kusema/kujitetea na hata um tight vipi upende usipende atachomoka tu
 
JK kumbe hizo tuhuma zinazoongelewa na yeye zinamuuma? Lakini hata hivyo yeye na uvasco dagama wake ndio ametufikisha hapa tulipo
 
Back
Top Bottom