Kikwete usichanganye urais na uwenyekiti wa CCM

Twalb zubeir

Senior Member
Feb 23, 2015
143
51
Rais Kikwete anapaswa kutenganisha uenyekiti wake wa Chama Cha Mapinduzi na Urais wa Jamhuri ya muungano alio nao kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu.

Mwenyekiti wa CCM taifa anaingiza Ushabiki kwenye suala linalohusu haki za kiraia za wananchi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mfano kauli yake ya kuwataka watu wanaohamasisha watu kulinda kura wazomewe ni kauli ya kichochezi isiyopaswa kutolewa na Mhe.Jakaya Kikwete. Kauli hiyo sio makini kutokana na kuwa ameadi kuwa kukusanyika ili kulinda kura ni kuvunja Sheria.

Je, Ni Sheria ipi itakayokuwa imevunjwa kwani uchaguzi huu si unaongozwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010? Sheria hiyo Kifungu cha 104(1) cha sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 kinasema hairuhusiwi kwa mtu yeyote kutumia picha,nembo au mavazi yenye rangi za chama fulani ndani ya eneo la mzio(Radius) wa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.

Kwa hiyo watu kukusanyika eneo linaloanzia mita 201 haivunji sheria.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Jakaya Kikwete,Jaji Lubuva na IGP Mangu wanapaswa kusoma sheria vizuri.Tena Jaji Lubuva anasikitisha sana katika hili. Asome Sheria vizuri..

Baadhi ya maeneo mwaka 2010,pamoja na kuwa na mawakala wetu ndani bado baadhi ya wagombea wa chama tawala walitoroka na masunduku.Safari hii hilo halitawezekana.

Hilo la kukusanyika baada ya mita 200 halivunji sheria isipokuwa IGP na Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Jakaya Kikwete ndio wanaotaka si kuvunja sheria bali kuivunja kabisa katiba ya nchi hasa ibara ya 20 . Pamoja na ubovu wake ilionao, Katiba ya Nchi, katika Ibara ya 20 (1), imetoa haki kwa mtu au watu kuwa huru kukutana, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine kutoa mawazo hadharani.

Huku kuzuia watu kukutana siku ya uchaguzi inashabihiana na amri za tawala za kiimla zinazoweka curfew(Amri ya kutotembea) hasa pale nchi inapokuwa katika shinikizo kali la kisiasa ambalo maimla wengi ili kujiimarisha madarakani huweka Curfew.

Tangu lini kupiga kura katika nchi ya kidemokrasia kukaendana na jaribio la kukiuka katiba ya nchi hasa ibara hiyo inayotoa uhuru wa kukusanyika au kwenda popote ilimradi havunji sheria hasa hiyo sheria ya uchaguzi ibara ya 104(1) na (2)?

Vilevile, Natoa Raia kwa Tume ya Uchaguzi sasa itoe kauli dhidi ya Matamshi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano aliyotoa kuwa kuna wapiga kura Milioni 28 wakati Tume ilitangaza kuna wapiga kura Milioni 22.7 tu.

Inapotokea watu wenye dhamana wakafanya mambo yanayoashiria uvunjaji wa sheria hasa sheria ya Takwimu inayokataza kutoa Takwimu za uongo hadharani tunashindwa kuwaelewa malengo na dhamira zao katika kujenga taifa lenye haki, linalofuata misingi ya Utawala bora wa sheria..
 
leo siku ya nyerere nilikuwa naongea na mkereketwa mmoja kuhusu uchaguzi. akanihakikishia kuwa wanaelekea kushindwa. lakini watatumia mbinu mbadala. nimemdharau right away. ni aibu kuweka maslahi binafsi mbele ya taifa.
 
Kwa jinsi ccm walivyopanic ni dhahiri hiyo sheria ua kukaa mita 200 kulinda kura wataumiza watu kwa kutumia jeshi. Nashauri mbinu nyingine nzuri ya kulinda kura, wale walioamua kulinda kura waende vituo vyote toka asubuhi na mapema wawe vituoni. Watakachofanya wakae mstarini kama.kawaida lakini wasiende mbele kupiga kura bali wawe wanawapisha watu wengine wawe wanaenda mbele kama tunavyowapisha wazee, wazazi, wajawazito, walemavu nk. Ila iwapo wataona kitu kisicho cha kawaida wachukue hatua mara moja na kuwapigia cm wananche wengine kuja kituoni hapo haraka.
 
sheria halali za nchi lazima zifuatwe..ukienda kinyume utakua halali ya ffu
 
Kwa jinsi ccm walivyopanic ni dhahiri hiyo sheria ua kukaa mita 200 kulinda kura wataumiza watu kwa kutumia jeshi. Nashauri mbinu nyingine nzuri ya kulinda kura, wale walioamua kulinda kura waende vituo vyote toka asubuhi na mapema wawe vituoni. Watakachofanya wakae mstarini kama.kawaida lakini wasiende mbele kupiga kura bali wawe wanawapisha watu wengine wawe wanaenda mbele kama tunavyowapisha wazee, wazazi, wajawazito, walemavu nk. Ila iwapo wataona kitu kisicho cha kawaida wachukue hatua mara moja na kuwapigia cm wananche wengine kuja kituoni hapo haraka.
Safiii
 
Mimi ninaomba Divine justice ifanyike mara moja kwa kikwete, Magu na wote wanaofanya hila dhidi ya haki na maisha ya Watanzania. Kikwete ni hopeless sijawahi kuona.

Kama alvyokamatwa yule kijana wa kusema Mwamunyange hana afya njema, ninaomba na kikwt akamatwe kwa kueneza habari za uwongo.
 
Nyie mnadhani kakosea takwimu..inawezekana hiyo 28 mil ni idadi kwa goli la mkono..simshasikia kuna hesabu ya vituo hewa...ni shida sijui nani sasa wa kuaminiwa!
 
The remaining 10 day with JK in power to me is just like having 51 years ahead with a fresh CCM!
 
Yani kuna njia nyingi sana walishafanya lakini zimegonga mwamba kutokana na kuwepo na mawasiliano ya haraka... technology katika mawasiliano imekuwa mwiba kwao.... maana lolote walipangalo, lafika mapema kwa wananchi....

Tutafata sheria na katiba katika uchaguzi huu...
 
Angejua tulivomchoka, bora asingeongea. Hizi siku kumi zake kama vile haziishi
 
Wiki 2 zilizopita akiwa anahutubia bunge la Kenya alimnadi Magufuli ilihali JK alikuwa amevaa kofia ya Urais...

Huwa anafanya makusudi kwa kuwa anajua hakuna mamlaka ya kumuwajibisha
 
Kura tutazilinda ukawa ni mpango wa mungu binafsi ninaamini mola atawapa upeo japo wa kuazima viongozi wetu wa jeshi watutendee haki na wasitii maagizo ovu.
 
Rais Kikwete anapaswa kutenganisha uenyekiti wake wa Chama Cha Mapinduzi na Urais wa Jamhuri ya muungano alio nao kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu.

Mwenyekiti wa CCM taifa anaingiza Ushabiki kwenye suala linalohusu haki za kiraia za wananchi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mfano kauli yake ya kuwataka watu wanaohamasisha watu kulinda kura wazomewe ni kauli ya kichochezi isiyopaswa kutolewa na Mhe.Jakaya Kikwete. Kauli hiyo sio makini kutokana na kuwa ameadi kuwa kukusanyika ili kulinda kura ni kuvunja Sheria.

Je, Ni Sheria ipi itakayokuwa imevunjwa kwani uchaguzi huu si unaongozwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010? Sheria hiyo Kifungu cha 104(1) cha sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 kinasema hairuhusiwi kwa mtu yeyote kutumia picha,nembo au mavazi yenye rangi za chama fulani ndani ya eneo la mzio(Radius) wa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.

Kwa hiyo watu kukusanyika eneo linaloanzia mita 201 haivunji sheria.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Jakaya Kikwete,Jaji Lubuva na IGP Mangu wanapaswa kusoma sheria vizuri.Tena Jaji Lubuva anasikitisha sana katika hili. Asome Sheria vizuri..

Baadhi ya maeneo mwaka 2010,pamoja na kuwa na mawakala wetu ndani bado baadhi ya wagombea wa chama tawala walitoroka na masunduku.Safari hii hilo halitawezekana.

Hilo la kukusanyika baada ya mita 200 halivunji sheria isipokuwa IGP na Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Jakaya Kikwete ndio wanaotaka si kuvunja sheria bali kuivunja kabisa katiba ya nchi hasa ibara ya 20 . Pamoja na ubovu wake ilionao, Katiba ya Nchi, katika Ibara ya 20 (1), imetoa haki kwa mtu au watu kuwa huru kukutana, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine kutoa mawazo hadharani.

Huku kuzuia watu kukutana siku ya uchaguzi inashabihiana na amri za tawala za kiimla zinazoweka curfew(Amri ya kutotembea) hasa pale nchi inapokuwa katika shinikizo kali la kisiasa ambalo maimla wengi ili kujiimarisha madarakani huweka Curfew.

Tangu lini kupiga kura katika nchi ya kidemokrasia kukaendana na jaribio la kukiuka katiba ya nchi hasa ibara hiyo inayotoa uhuru wa kukusanyika au kwenda popote ilimradi havunji sheria hasa hiyo sheria ya uchaguzi ibara ya 104(1) na (2)?

Vilevile, Natoa Raia kwa Tume ya Uchaguzi sasa itoe kauli dhidi ya Matamshi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano aliyotoa kuwa kuna wapiga kura Milioni 28 wakati Tume ilitangaza kuna wapiga kura Milioni 22.7 tu.

Inapotokea watu wenye dhamana wakafanya mambo yanayoashiria uvunjaji wa sheria hasa sheria ya Takwimu inayokataza kutoa Takwimu za uongo hadharani tunashindwa kuwaelewa malengo na dhamira zao katika kujenga taifa lenye haki, linalofuata misingi ya Utawala bora wa sheria..


:glasses-nerdy::glasses-nerdy::glasses-nerdy:
 
Kwa jinsi ccm walivyopanic ni dhahiri hiyo sheria ua kukaa mita 200 kulinda kura wataumiza watu kwa kutumia jeshi. Nashauri mbinu nyingine nzuri ya kulinda kura, wale walioamua kulinda kura waende vituo vyote toka asubuhi na mapema wawe vituoni. Watakachofanya wakae mstarini kama.kawaida lakini wasiende mbele kupiga kura bali wawe wanawapisha watu wengine wawe wanaenda mbele kama tunavyowapisha wazee, wazazi, wajawazito, walemavu nk. Ila iwapo wataona kitu kisicho cha kawaida wachukue hatua mara moja na kuwapigia cm wananche wengine kuja kituoni hapo haraka.
wazee nikina dada wale wanoko wanoko awa ruhusiwi kipindi iki kupiga kura
Piga kura linda kura
 
Msiogope msiogope ndugu watanzania, hakuna hila itakayosimama mbele ya haki. Mipango ya hila itajulikana tu, naomba mamlaka husika watu watakaposhikwa na nyaraka za kura wahesabiwe sawa na wabeba nyara za serikali. Pia, pale nguvu ya umma itakapowatia mikononi watu hawa hatuhitaji kusikia mara wamebambikiziwa au imepanda imeshuka. Wapinzani wamejipanga ipasavyo.

Kwa taarifa yenu MKAE MKIJUA kila walipo wanachama 10 wa CHAMA LANGU watano kati ya hao mioyo yao iko UPINZANI, NA HIVYO BASI KILA WANAPOKAA KUPANGA HILA KUNA 48% ZA kuvujisha hila na mipango ya ADUI WA HAKI.

Take it from me
 
Back
Top Bottom