Kikwete na semina elekezi kwa Mawaziri - Dodoma 2011

I believe you mean 'epusha'. Sasa inamaana kuwa hawa watu wasipewe changamoto na wao ndio watendaji wakuu wa serikali nzima kisa vifo vya mama na watoto? Unajua vitu vingine bwana, nikama kumwambia mtu asimnunulie mke wake mkufu wa dhahabu kisa watu wanakufa njaa sehemu fulani ndani ya mji anao ishi. Tena huo mfano mbaya kwasababu unaubinafsi nadhani mfano hai utakuwa ni kwamba kwasababu wanafunzi wanakaa chini madarasani basi na kwenye vyuo vya ualimu wakaechini. Ndio unapoint kuwa kuna matumizi mabaya ya fedha yanafanyia.. (moja ya vitu ambavyo vimeongelewa na Rais, na kuongelewa zaidi na CAG) sasa mnataka wanyamaze, wakikaa kimya mnalia. Ivi jamani sisi binadamu sijui tukoje. Ukweli ni kwamba watanzania wengi, wewe nahisi ukiwa mmojawapo tunashindwa kabisa kufanya ukosoaji unaojenga na tunadiriki kulalamika tuuu mwanzo mwisho. Ivi wewe binafsi embu naomba kujua ulishafanya nini kuchangia kupunguza vifo vya kinamama wakati wauzazi? (inaweza kuwa kuchangia kitanda ata kimoja hospitali ata ya kijijini kwenu, kuchangia ata kwa mawazo katika taasisi husika, au mchango gani umetoa katika jamii?) Naomba kujua, na atakama umetoa mchango, point yangu nikwamba wengi hatujafanya hivyo, na hilo ndio tatizo la Tanzania. Wangapi mjini hapa mahodari aw vimada na kuhonga rav-4 na harrier kwa mademu wanashindwa kutoa madawati kumi au kuchangia mfuko wa mikopo wa waalimu. Ukweli ni kwamba tunapenda sana kufanyiwa, kodi zenyewe tunakwepa. Serikali si Mungu, nadhani Jack Kennedy RIP alikuwa na akili sana aliposema ' Uliza wewe utaifanyia nini Nchi yako na si nchi yako itakufanyia nini wewe' Lazima niseme ukweli aisee, watu wamezidi siasa za kujidanganya na kunyoshea vidolee tuu. Tuanze kwa kujitazama sisi, jee tunamchango kiasi gani katika jamii? Asilimia 10 tuu ingefanya hivyo, basi maendeleo mbona tungeyafikia vizuri tuu katika miaka 25 ijayo.


Tunaongea sana sisi watanzania, inawezekana mkuu wangu wewe ni mzalendo maradufu, umetoa mchango wa vitanda 100 katika hospitali mbali mbali kwaajili yakina mama kujifungulia. Chaajabu dada yako au mtoto wangu mimi akienda pale, ma nurse wanataka kitu kidogo laasivyo unaambiwa kazalie kwenye ndoo ya plastiki ama ya chuma. Matatizo ya Tanzania sio serikali peke yake, jamii yenyewe inamatatizo makubwa sana. Haiwezekani serikali kutatua kila kitu bila sisi wananchi kukubali kwanza kuwa tunamatatizo.

WE KWELI POPOMPO!!!!!!!!

Yani unatetea matumzi haya ya ajabu ya serekali kisa CHANGAMOTO? ETI WATENDAJI WAKUU WASEREKALI ndio nini MPUUUUZZZZZZZZZZZZIIIIIIIII wewe yani unatia hasira tafadhali wacha mambo yako haya ! ungekuwa huku kwetu uswazi tungekuchoma moto FISADI MKUBWA WEWE.

yani wewe huoni umuhimu wa WAJAWAZITO KUPATIWA HUDUMA BORA? ndio maana MMENUNUA BAJAJI na bora hata zingekuwa BAJAJI basi zile sijuhi PIKIPIKI MCHINA!

Alafu hiyo mifano yako inaonyesha huwezo wako wakufikiri yani kama ungejuwa na familia wewe unaweza kua hata watoto ili mradi tu uvae suti!

kumbuka KODI yetu tunatoa ili itufanyie haya ninayo lalamika na sio WAPUUZI NYIE KUNYWA CHAI MAOFISINI KWENU KWA KODI ZETU!

Eti nichangie nichangie mara ngapi? VAT, na PAYEE nayotoa haitoshi? inaenda wapi kiongozi wewe wa serekali?

au ndio mnataka haya mambo ya haibu wachina kuja kutoa misaada mpaka ya kandambili tena IKULU? Ndio mnakomaa tutoe misaada na sisi?

attachment.php

kikwete+china+4.jpg
 
porojo tupu hicho ni kichwa cha mwendawazimu!!unless CCM is out of power otherwise mafisadi wataendelea kuinyoa bila huruma nchi hii
 
JK leo kawaambia mawaziri wake wajitahiidi kusoma ili waweze kuzifahamu wizara zao , kwani amegundua kuwa wapo ambao hawasomi kazi yao ni kuangalia TV Libya kuna nini , kwa Osama nini na kusoma magazeti, na amewaambia kuwa ukiona hivyo ujue waziri kazi imemshinda.

Mytake, sasa ameanza kuelewa kelele za muda mrefu kuwa baraza lake ni kubwa na halina kazi za kufanya . Mf. yupo waziri wa maji, yupo wa klilimo na ushirika, yupo wa mifugo na uvuvi , yupo wa mazingira, yupo wa ardhi :sasa mipaka YAO ya kazi ili wasiingiliane kwenye majukumu yao ni wapi? kama kuna eneo lina mgogoro wa wakulima , wafugaji na mbuga za wanyama ina maana wote watatu wawepo?
 
tatizo kubwa ni kutoa maelekezo mazuri mazuri lakini kwa vile mawaziri wanadharau na wanajua yeye JK na waziri mkuu si wafuatiliaji na wala hawajui kuwajibisha watu hivyo hamna atakae hangaika kutimiza aliyosema maana hata yeye hayatimizi hivyo hatoi mfano bora na kuchukua hatua.
 
JK give us a break yaani una mawaziri/viongozi wanaokunywa hadi kujisahau na kuomba msaada kuchukuliwa nyumbani na wewe bado unawaweka kwenye uwaziri au vyeo vyao? Sasa wewe una kazi gani? I mean unakuja kuwashitaki kwetu wakati uwezo huna au vipi? Kwanza sioni ni sahihi wewe kama rais kutoa changamoto kwenye hii semina endelevu wapo ambao hii ni kazi yao au ndio katika kutafuna pesa za walipa kodi? Inaonyesha uliowachagua hawajui kazi na muda huna maana miaka yako ndio inatokomea hivyo, Je, Mafisadi papa bado unabishana nao tu au mmekubaliana yaishe na sisi walipa kodi tuendelee kuumia tu? Je ni nani anaongeza mfumuko wa bei? I mean literally .... ....
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hii JF nayo inaboa pale ambapo jitihada zinafanyika ambazo zinaleta matumanini ya maendeleo lakini watu wengine bado wanaponda. Yani ni kama biashara kichaa vile. Watanzania wenyewe ndio sisi, kama PUNDA, mpaka tusukumwe, iwe kazini iwe wapi. Rais ni binadamu tuu, na japokuwa kiboko anacho punda nao mbishi ati. Kubalini mtu akifanya positive step. JF move away from promoting sewage talk and towards more constructive criticism. The majority of political views in this forum, which I dare say are not too divergent, seem to be unable to produce objective and constructive critiques of the government or the ruling party. Perhaps it is true that there is little to be lauded in their actions but being unable to demonstrate objectivity is definitely a sign that when such an entity comes into power, they themselves will be unable to withstand political dissidence. If you cant be objective in your thinking, then you most certainly will not in your actions.

On this seminar, congratulations JK, and I hope these public servants of yours will heed the words.

Mkuu vipi? Ama ndiyo tena mtu akisha penda? Kuna nini cha maana hapo kodi zetu kuteketezwa kwa semina elekezi? Wote hao wameteuliwa na Jk. Wakati anawateua hakutuuliza sisi wananchi. Sasa kama wanatenda kinyume yeye akawawajibishe. Katiba yetu ya sasa inampatia madaraka hayo. Sasa analalamika nini? Inaboa sana!
 
Ametoa mfano wa Msemaji wa Ikulu ya Marekani kuwa amekuwa akitoa taarifa kila wiki na akiulizwa swali hasemi ngoja nikamuulize Rais Barack Obama kwa kuwa anajua kinachoendelea na hivyo anajibu tu.

White house spokesman anatoa briefings almost kila siku sio kila wiki. Watch C-Span
Mawaziri wenyewe Masters na PhD ndio hizo za kuungaunga online tena from unaccredited universities unategemea nini mkuu? Wengi wao hawajui wanalolifanya na hawana confidence ya leadership/Micromanagement.
At least ninakuunga mkono umeliona hilo mwenyewe.

Hakuna haja ya kwenda mbali, hapo Kenya kuna msemaji wa serikali ya Kenya Dr. Alfred Mutua ambaye Msemaji wa Ikulu DSM ak.a Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu inabidi atizame clip hii ya namna ya kutoa habari motomoto akishirikiana na watendaji wa juu wa serikali:

VIDEO KWA HISANI YA 'MSEMAJIKENYA" wa YOUTUBE ambapo unaweza kuangaliza video lukuki za Msemaji wa Serikali ya Kenya Dr. Alfred Mutua. Ktk clip hii ya chini Msemaji wa Serikali na watendaji wanazungumzia 'upungufu wa mafuta aina ya super na utaratibu wa kutoa tenda za kuagiza mafuta Kenya, tarehe 05/05/2011:

 
Last edited by a moderator:
Ametoa mfano wa Msemaji wa Ikulu ya Marekani kuwa amekuwa akitoa taarifa kila wiki na akiulizwa swali hasemi ngoja nikamuulize Rais Barack Obama kwa kuwa anajua kinachoendelea na hivyo anajibu tu.

Huyu jamaa msanii kweli kweli! Sasa yeye anataka Mawaziri wake wafanya kazi zao kama Mawaziri/Maofisa wa Obama, je na yeye yuko tayari kufanya kazi kama Obama!? Obama huviita vyombo mbali mbali vya habari kwa ajili ya news conference na kujibu maswali mbali mbali yanayoulizwa na waandishi hao wa habari papo kwa hapo, je Kikwete naye ataanza rasmi kufanya hivyo? Maana tangu aingie madarakani miaka karibu sita iliyopita hajawahi kufanya kitu kama hicho.
 
Amenichekesha sana aliposema Mawaziri wasipingane ila wateteane. Mkulo anatoka nyumbani kwake kwa mkewe na baada ya waliyoongea huko anaita press na kutangaza lazima Dowans walipwe, halafu anataka mtu Kama Sita asimame na kuunga mkono wakati jambo hilo halikuwahi kujadiliwa ndani ya baraza! Ili wasipingane angewaambia waache kuropoka mambo makubwa kabla hayajawekewa msimamo wa pamoja
 
Jama ****** tangu apige kikombe cha BABU kama anaongea point kweli tena na msisitizo, ila bado tunahitaji tuone utekelezaji na uwajibishaji wake, isije ikawa kelele za chura zinazoshindwa kumzuia tembo kunywa maji.
:bange:
 
Mbatia "anasema,hakuna jipya ktk semina elekezi dodoma zaidi ya polojo,kwa sababu viongozi wa tz ni wasanii sio watekelezaji ni maneno tu",source bbc today.
 
haya jamani Raisi kaanza kazi sasa,ebu soma kipande hiki kutoka gazeti la serikali,HABARI LEO

RAIS Jakaya Kikwete amewataka viongozi na hasa mawaziri wasiowajibika kwa pamoja katika Baraza la Mawaziri na Bungeni, kujiondoa ili watakaobakia wajenge umoja katika kuwatumikia wananchi.


Kama ni kweli atayafuatilia aliyoyanena tunaweza fika tutakako

439x.jpg
 
Kama Uraisi ni kuongeaongea tu bila vitendo hata mimi naweza kuwa raisi wenu ajae, hivi sasa najipanga.
 
Mbatia "anasema,hakuna jipya ktk semina elekezi dodoma zaidi ya polojo,kwa sababu viongozi wa tz ni wasanii sio watekelezaji ni maneno tu",source bbc today.

Baada ya magamba ni hii "Funika kombe mwanaharamu apite"
 
Maagizo yake yamekuwa hayatekelezwi si tu na mawaziri au makatibu wakuu bali hata vidampa wa mawizarani na kwenye halmashauri. Tushamzoea huyo,hana jipya zaidi.
 
Ndugu watanzania,
Nimekuwa na mawazo mengi juu ya nchi yetu inavyoendeshwa na kuhujumiwa na viongozi wetu hasa marais tuliowapa dhamana ya kulinda rasilimali zetu. Kwanza nimesikitishwa sana na jana kuona jk bado anatumia kodi za wananchi wanyonge kifisadi kwa kile anachokiita "semina elekezi". Hii maana yake ni nini hasa? Maana yake ni kwamba wananchi masikini wataendelea kuteseka kwenye umasikini wakati wakubwa wao kila siku wanafikiria "avenues" za kuteketeza fedha za umma. Kwa mahesabu ya haraka kwenye ile semina kuna jumla ya washikiri wasiopungua mia moja. Wote ni maafisa wakuu wa serikali, ama wameenda dodoma kwa magari ya serikali au ndege. Kwa wastani kila mmoja atamgarimu mlipa kodi si chini ya milioni nne. Zididisha millioni nne mara washiriki mia moja. Hii ni sawa na shillingi milioni 400. If this money was used in its best alternative way (opportunity cost), at least 40 furnished classrooms would be built and save the lives of thousands of Tanzanians.

Maswali yangu kwa JK na washirika wake.
1. Je kwa nini aliwateuwa watu wasiolelewa majukumu na kazi zao?
2. Je wale wliopata semina (ngurudoto) elekezi mara tuu alipochaguliwa kwa mara ya kwanza anawaweka kwenye fungu gani? Kwa nini asingewaengua kwa sababu wao tayari wanajua majukumu yao ili kuokoa fedha.
3. Je amewahi kufanya tathmini ya semina elekezi ya ngurudoto ili kujua mapungufu na faida zake?
4. Katika semina hii mambo mengi jk ameyasema, akiwaagiza washiriki kufanya, je alikuwa hajui muda wote kuwa serikali yake ni mzigo kwa wanainji?
5. Kama hakujua hilo (4 above) kwa nini asiachie ngazi sasa kwa sababu hajui shida za wanainji wake?
6.Baada ya Mh Zitto kusema serikali imefulia, imeonekana serikali ya Mkulo na JK ni mabingwa sana wa kukopa mabenki ya ndani na sasa mkulo anakuja na taarifa kuwa serikali ina ziada kubwa ya fedha. Je hamuoni kudanganya umma ili waonekane kuwa kuna kitu wanafanya kumbe ni watu wasiopenda kushughulisha bongo zao?
7. Kwa nini uwape watu amabao hawawezi kushughulisha bongo zao semina?

Aluta cont...., Mungu Ibariki Tanzania
 
Mimi sioni kama kulikuwa na mantiki yoyote ya kuwa na semina tena wakati walikwishafanya semina mwaka 2006 kule Ngurdoto na kutumia pesa nyingi za walipakodi, hii tena ni ya nini? Pia rais anapowaomba viongozi wajiwabishe badala ya kuwawajibisha huu ni usanii mwingine tena wa kutafuta mvuto kwa wananchi.

Tumechoshwa na longolongo, tunahitaji vitendo na si maneno matupu ambayo kamwe hayatatusaidia.
 
hii semina elekezi kwa mawaziri, manaibu na makatibu wakuu kwa muda wa siku nne ni kuongeza matumizi ya serikali tu.... sasa J.K si ulishawatembelea kwenye wizara zao ukaongea nao sana tu....sasaivi umewaita tena dodoma...huu ni ufujaji wa pesa ya umma.....tuna mambo ya msing mengi sana ambayo hiyo pesa ya posho ingetumika kuyatekeleza.....mheshimiwa umeona bora iende kwenye matumbo manene ya wala nchi....!
Jeikei wake up look meli ako inazama.......!

:israel:
 
Back
Top Bottom