Kikwete hajui maana ya urais!

Apr 7, 2012
47
55
Tangu aingie madarakani jk ameshimdwa kuongoza nchi kwa sababu:

1.watu anaowateua wote ni washikaji hivo kila waziri na wakurugenzi wanafanya wanavotaka bila kumuogopa.

2.Amekuwa kama mzazi anayewapangia kazi watoto kazi wafanye na hachukui hatua yoyote wasipofanya.

3.Haoneshi dhamira ya dhati kwani serikali yake haina mipango maalumu inayoeleweka. Mfano, bajeti ya 2011/2012 waliahidi ajira elfu 60 lkn sijui hiyo hoja imeenda wapi na mwaka wa fedha umeisha.

4.Safari za nje ni nyingi mno kana kwamba ikulu kuna kunguni. Aige mfano wa Paul Kagame wa rwanda!

5.Amekuwa mtu wa maneno mno kuliko vitendo, mara ari mpya,kasi mpya na nguvu ya ajabu, kilimo kwanza, maisha bora kwa kila mtanzania, tanzania bila ukimwi inawezekana,

6.Waziri mkuu wake ni kama kituko cha karne! Hakuwahi kuonesha chochote cha maana tangu ateuliwe. Mda wote ni mtu wa kulalamika na kulaani.

Historia itawahukumu maana kila waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wengine wanaiba kwa kasi mpya ili 2015 wakastaafu salama. Watanzania msitegemee chochote mda uliobaki. Jiandae kwa hali ngumu zaidi!
 
Amekuwa ni mtu wa kucheka mno. kucheka kumezidi, hata siku ile analaani mauwaji ya albino alikuwa anacheka tu baada ya kukasilika sana aonekane vitendo hivyo vinamwuzi
 
Jamaa ni Check bob flani hivi, anaona noma kuwatosa washkaji zake eti kijiwe kitaharibika
 
Hata ule utaratibu aliouacha mzee Mkapa wa kufanya interview kwa wanaoutaka ukurugenzi wa maendeleo wa wilaya (DED) kaondoa. Watu wanateuana kishikaji tu. Tutafika kweli?
 
Ikulu ni mahali patakatifu,hakueilewa hii kauli au aliipuza na ndiyo sababu kaanguka kwa kasi na ari zaidi.m2 wa motoni yule na analaana ya wtz.na azidi kulaaniwa.
 
Naamini jk naye atakuwa sio mwaminifu, kivipi??
--kwani haiwezekani mtu ukampa kazi mtu ambaye cag amemprove kuwa ni mwizi na ukasuasua kumchukulia hatua, mazingira aya yamejaa shaka dhidi ya mkuu wa kaya na ni wazi hata yeye alofanya uteuzi huo sio mwaminifu hata
 
Tangu aingie madarakani jk ameshimdwa kuongoza nchi kwa sababu:

1.watu anaowateua wote ni washikaji hivo kila waziri na wakurugenzi wanafanya wanavotaka bila kumuogopa.

2.Amekuwa kama mzazi anayewapangia kazi watoto kazi wafanye na hachukui hatua yoyote wasipofanya.

3.Haoneshi dhamira ya dhati kwani serikali yake haina mipango maalumu inayoeleweka. Mfano, bajeti ya 2011/2012 waliahidi ajira elfu 60 lkn sijui hiyo hoja imeenda wapi na mwaka wa fedha umeisha.

4.Safari za nje ni nyingi mno kana kwamba ikulu kuna kunguni. Aige mfano wa Paul Kagame wa rwanda!

5.Amekuwa mtu wa maneno mno kuliko vitendo, mara ari mpya,kasi mpya na nguvu ya ajabu, kilimo kwanza, maisha bora kwa kila mtanzania, tanzania bila ukimwi inawezekana,

6.Waziri mkuu wake ni kama kituko cha karne! Hakuwahi kuonesha chochote cha maana tangu ateuliwe. Mda wote ni mtu wa kulalamika na kulaani.

Historia itawahukumu maana kila waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wengine wanaiba kwa kasi mpya ili 2015 wakastaafu salama. Watanzania msitegemee chochote mda uliobaki. Jiandae kwa hali ngumu zaidi!

Mbona hueleweki hayo uliyoyasema yana uhusiano gani na thread yako? Istoshe naona uko kimajungu zaidi. Unazo takwimu zinazoonesha kwamba mpaka sasa hakuna watu walioajiriwa na kuonesha kuwa hadi Rais anamaliza muda wake atakuwa hajatimiza ahadi zake? Huwzi kufananisha Tanzania na Rwanda hasa katika suala zima za mahusiano ya kimataifa na mifumo ya kiutawala. Ukumbuke kwamba Rwanda mara nyingi ilikuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe hivyo inawezekana kabisa Rwanda wasiwe na mahusiano mazuri na nchi nyingine, na mfano mwingine wa Rwanda ni Zimbabwe.

Kuhusu nia ya dhati ya serikali ya JK mimi kwa upande wangu naona kama nia wanayo ila kuna vikundi vya watu wachache ambao wapo kwa ajili kuupotosha umma kuwa Serikali haifanyi kitu. Watu hao ni kama wewe mwandishi wa hii Thread na ndiyo maana hata ulichokiandika kinaonesha wazi ni majungu, wapo wanasiasa na mafisadi waliotoswa nao wapo kwa ajili ya kuibeza Serikali ilioko madarakani. Kwa mtindo huo wa propaganda juhudi za Serikali haziwezi kuonekana kwani ni sawa na kuchota maji kwa kijiko na kuyamwaga baharini.
 
Amekuwa ni mtu wa kucheka mno. kucheka kumezidi, hata siku ile analaani mauwaji ya albino alikuwa anacheka tu baada ya kukasilika sana aonekane vitendo hivyo vinamwuzi
Kulia hakumaanishi kuguswa na Jambo, unaweza kulia kwa kujoki. Kama ni suala la kulia iweje Waziri Mkuu atupiwe lawama kuwa hawajibiki wakati tatizo la mauaji ya Albino lilimgusa hadi chozi likamdondoka?
Tuache kupiga majungu ya kigeu kigeu.
Wana JF wamekuwa vigeu geu, vigeu geu. Jk mtu wa watu bwana tumpe support atufikishe 2015 pale tutakapopata mtihani wa nani wa kuziba pengo lake, japo tunajifariji kuwa mtu kama SLAA anaweza kuongoza, subutu. Kelele zote kwa sababu tu eti alitamka kuwa nchi haitatawalika, sasa anataka alazimishe isitawalike wakati huo haangalii boriti iliyoko kwenye jicho lake. Tusubiri 2015 tuone tutakavyo garagazwa na wanafiki kuwa watatuletea maendeleo zaidi ya tulio nayo sasa wanasahau kuwa sasa hivi dunia inaongozwa na mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yako juu ya uwezo wa nchi changa. Mabadiliko tabia nchi, mabadiliko ya kiuchumi, kukuwa kwa teknolojia na utandawazi.
 
Naamini jk naye atakuwa sio mwaminifu, kivipi??
--kwani haiwezekani mtu ukampa kazi mtu ambaye cag amemprove kuwa ni mwizi na ukasuasua kumchukulia hatua, mazingira aya yamejaa shaka dhidi ya mkuu wa kaya na ni wazi hata yeye alofanya uteuzi huo sio mwaminifu hata

JK siyo mtu wa papara Mkuu, angalia suala la madaktari alivylimaliza kistaarabu?
 
Niliwahi kupigwa ban niliposema uongozi wa Jk hauna tofauti na wa Juha.

Japo sitasema hivyo tena, huo ndio uhalisia
 
Mbaya zaidi hata sisi wenyewe hatujui maana ya kuwa na raisi, laiti tungejua tungeshamtimua! Tena angekuwa kwao soga analima mihogo, kwenye shamba la wajamaa, ambalo tungelianzisha kila kona Tanzania. Tusiropoke tu, upuuzi ni wetu wenyewe kuamini katika mifumo isiyokidhi haja ya mazingira na nyakati tulizonazo....eti demokrasia, kisa mzungu kasema, PUMBAVU!
Mungu wetu anaita, yu tayari kutushindia vitani, tuitike sasa katika umoja na kuthubutu!
 
Kenge unaonesha moyo wa kitanzania kwelikweli, manaake watanzania hatuna kisasi, hatujali kuhusu raslimali zetu kama nchi, mtu akiiba asiibe yote ni sawa, kweli sote tunakuwa kama jinsi jina lako lilivyo! Hebu soma thrd ya Maige uona jinsi alivyokamatwa na TISS harafu! akili ni mali kila mtu anazake, lakini za kikwetu zina mushkeri!
 
Mkapa aliwahi kuuliza hivi "Kwani Kikwete ni robot"?

Yaani mika 48 ya muungano, bado hiyo ndiyo unaona umeongea point kweli? teh te teh teh, kazi kweli kweli. Ehe endeleza mkuu akajibu vipi?. Yaani mchango wako sijui niweke kundi gani? umbea si umbea, chuki binafsi si chuki binafsi, majungu si majungu, nabaki najiuliza huyu alichangia hivi ni mtu au Robot? teh teh teh, ala kumbe Wewe ni ROBOT, pole sna.
 
Mbona hueleweki hayo uliyoyasema yana uhusiano gani na thread yako? Istoshe naona uko kimajungu zaidi. Unazo takwimu zinazoonesha kwamba mpaka sasa hakuna watu walioajiriwa na kuonesha kuwa hadi Rais anamaliza muda wake atakuwa hajatimiza ahadi zake? Huwzi kufananisha Tanzania na Rwanda hasa katika suala zima za mahusiano ya kimataifa na mifumo ya kiutawala. Ukumbuke kwamba Rwanda mara nyingi ilikuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe hivyo inawezekana kabisa Rwanda wasiwe na mahusiano mazuri na nchi nyingine, na mfano mwingine wa Rwanda ni Zimbabwe.

Kuhusu nia ya dhati ya serikali ya JK mimi kwa upande wangu naona kama nia wanayo ila kuna vikundi vya watu wachache ambao wapo kwa ajili kuupotosha umma kuwa Serikali haifanyi kitu. Watu hao ni kama wewe mwandishi wa hii Thread na ndiyo maana hata ulichokiandika kinaonesha wazi ni majungu, wapo wanasiasa na mafisadi waliotoswa nao wapo kwa ajili ya kuibeza Serikali ilioko madarakani. Kwa mtindo huo wa propaganda juhudi za Serikali haziwezi kuonekana kwani ni sawa na kuchota maji kwa kijiko na kuyamwaga baharini.
Huwezi tambua hilo mkuu kwa sababu na wewe ni mmojawapo wa wanaonufaika na mfumo wa sasa wa hii serikali ya JK. Kweli shibe mwana malevya na njaa mwana malegeza. Kama unafikia kuona ni kweli serikali imewafanyia kitu kikubwa watanzania basi umepofuliwa macho hadi roho yako. Eeeeh mwenyezimungu angamiza hiki kizazi kinachokandamiza wanyonge. Tunaweka ktk mikono yako hawa wahalifu na wanyonyaji wa uchumi wetu.
Wewe pekee ndio unajua ni jinsi gani ya kuangamiza kundi hili la wachache ili tupate ahueni ya maisha yetu. Muangamize kabisa KENGEMUMAJI ikiwezekana umpe upofu au hata awe kiziwi ili asiendelee kutudhihaki kwa hizi kauli zake chafu na za kejeli kwa watanzania!
 
Mbona hueleweki hayo uliyoyasema yana uhusiano gani na thread yako? Istoshe naona uko kimajungu zaidi. Unazo takwimu zinazoonesha kwamba mpaka sasa hakuna watu walioajiriwa na kuonesha kuwa hadi Rais anamaliza muda wake atakuwa hajatimiza ahadi zake? Huwzi kufananisha Tanzania na Rwanda hasa katika suala zima za mahusiano ya kimataifa na mifumo ya kiutawala. Ukumbuke kwamba Rwanda mara nyingi ilikuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe hivyo inawezekana kabisa Rwanda wasiwe na mahusiano mazuri na nchi nyingine, na mfano mwingine wa Rwanda ni Zimbabwe.

Kuhusu nia ya dhati ya serikali ya JK mimi kwa upande wangu naona kama nia wanayo ila kuna vikundi vya watu wachache ambao wapo kwa ajili kuupotosha umma kuwa Serikali haifanyi kitu. Watu hao ni kama wewe mwandishi wa hii Thread na ndiyo maana hata ulichokiandika kinaonesha wazi ni majungu, wapo wanasiasa na mafisadi waliotoswa nao wapo kwa ajili ya kuibeza Serikali ilioko madarakani. Kwa mtindo huo wa propaganda juhudi za Serikali haziwezi kuonekana kwani ni sawa na kuchota maji kwa kijiko na kuyamwaga baharini.


I don't want to quote you in any thing, but I strongly believe in INDIVIDUAL DIFFERENCES and Individual PERCEPTION...Haya uliyoandika ni mawazo yako na wala usitake kutulazimisha tuamini kama wewe. To me JK is nothing but like a shadow, it doesn't move unless the object moves....Huyo ndiyo JK. Hata kama ni ushabiki, kumshabikia JK lazima uwe waziri, mkuu wa wilaya, au mtu mwingine mweye cheo kikubwa serikalini au kwenye CCM. Lakini kwa sisi walalahoi...kumshabikia JK ni dhambi, tena dhambi kubwa....Sasa hivi imefikia watu wanavumilia kuwa watz na wala hakuna anayejivunia kuwa Mtz. Kikwete anafanya nini kikubwa ambacho kinaonekana hapo Magogoni?
1. Hakuna uwajibikaji serikalini....pengine kwa sababu na yeye anaogopa atawajibishwa kwa sababu na yeye ni wale wale.
2. Gharama za maisha zinapanga huku shilingi ikizidi kuporomoka....hakuna juhudi za dhati zinazoonekana kuhakikisha hali hii inaondoka.
3. Umeme wa kusua sua kila siku, na ahadi zisizotekelezeka.
4. Huduma za afya mbovu...hakuna dawa, hakuna vitanda na hakuna vifaa vya kufanyia kazi.
5. Elimu iko taabani....hadi leo, miaka hamsini ya uhuru, kuna shule kibao watoto wanakaa chini, waalimu hawana makazi, hakuna vifaa vya kujifunzia wala vya kufundishia
6. Maliasini kama madini, gas, magogo na wanyama, tunabadilishana na neti....
7. Serikalini hakusanyi kodi kwa wafanya biashara wakubwa na wawekezaji...mapato ya serikali leo yanategemea mtu kama mimi ninunue kipande cha sabuni nikatwe VAT...
8. Kilimo kwanza kimefeli...hakuna pembejeo, hakuna maafisa ugani....hakuna mbegu bora...
9. Rushwa imeongezeka na Takukuru haijawahi kuwa na meno wala haina meno....
10. Haki mahakamani hakuna, na wala JK hakuna anayemuwajibisha...kila kitu collapsed
11. Bado watu nchi hii wanasafiri siku tatu kutoka ndani ya nchi hiii, MIUNDOMBINU HOVYO...kutoka Moshi hadi Mpanda au Kigoma, almost three days..
12......
13......
14.......

Unapata wapi ujasiri wa kumsifia JK na CCM yake? Kwa lipi jipya linaoonekana? Aliahidi meli mpya ziwa Tanganyika, ziwa Victoria na Ziwa nyasa....hadi sas karibu 1/3 imeisha hakuna hata dalili za kununua meli hata moja...

Lazime uwe na MTINDIO WA UBONGO KUMSIFIA KIKWETE...LABDA UWE MKEWE WA NDOA......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom