Kulwa Jilala
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 3,510
- 7,755
Kwa watoto wadogo na wasiojua mambo wanadhani hayati Magufuli alianza kuwa mkali alipokuwa rais wa nchi tu wakati ukweli ni kwamba Magufuli alikuwa mkali na mfuatiliaji tangu akiwa naibu waziri, waziri na baadae rais wa nchi.
Katikati ya mafisadi wakubwa wa awamu za Mkapa na Kikwete lakini walimwogopa Magufuli na aliwashughulikia kila wizara aliyopelekwa, kwa waliokuwepo kwenye wizara ya uvuvi, aridhi na ujenzi enzi za waziri Magufuli watakwambia moto wake.
Swali la kujiuliza aliwezaje kutekeleza bila kutumbuliwa? Je kwenye baraza la mawaziri la sasa kuna waziri anayevaa viatu vyake? Hata baada ya kuwa rais na kufariki dunia mpaka leo miaka 2 imeisha si Chadema , ACT Wazalendo wala CCM waliokuja na ushahidi usiotia shaka juu ya ufisadi wake licha ya kwamba waliahidi pindi tu atakapotoka madarakani basi watakuja na mikataba ya ufisadi na rushwa kubwakubwa zilizosainiwa na yeye.
Mwezi march 2023 imetimia miaka miwili tangu atutoke duniani lakini mahasimu wake ikiwemo ,Lisu, Lema , Nape ,Makamba, Kigogo bado hawajawaletea watanzania ufisadi wa Magufuli.
kinyume chake wanaendeleza mafanikio na miradi ya awamu ya tano kwa kasi kubwa, walipinga kila kitu lakini sasa wanatumia kila kitu walichokipinga! Mbowe akimaliza kutukana anakimbilia kupanda ndege mpya ya Dreamliner impeleke KIA.
Walioahidi kuifunika legacy kumbe hawana uwezo kuifunika hata kidole chake tu!!
Muda utawaumbua zaidi.
Katikati ya mafisadi wakubwa wa awamu za Mkapa na Kikwete lakini walimwogopa Magufuli na aliwashughulikia kila wizara aliyopelekwa, kwa waliokuwepo kwenye wizara ya uvuvi, aridhi na ujenzi enzi za waziri Magufuli watakwambia moto wake.
Swali la kujiuliza aliwezaje kutekeleza bila kutumbuliwa? Je kwenye baraza la mawaziri la sasa kuna waziri anayevaa viatu vyake? Hata baada ya kuwa rais na kufariki dunia mpaka leo miaka 2 imeisha si Chadema , ACT Wazalendo wala CCM waliokuja na ushahidi usiotia shaka juu ya ufisadi wake licha ya kwamba waliahidi pindi tu atakapotoka madarakani basi watakuja na mikataba ya ufisadi na rushwa kubwakubwa zilizosainiwa na yeye.
Mwezi march 2023 imetimia miaka miwili tangu atutoke duniani lakini mahasimu wake ikiwemo ,Lisu, Lema , Nape ,Makamba, Kigogo bado hawajawaletea watanzania ufisadi wa Magufuli.
kinyume chake wanaendeleza mafanikio na miradi ya awamu ya tano kwa kasi kubwa, walipinga kila kitu lakini sasa wanatumia kila kitu walichokipinga! Mbowe akimaliza kutukana anakimbilia kupanda ndege mpya ya Dreamliner impeleke KIA.
Walioahidi kuifunika legacy kumbe hawana uwezo kuifunika hata kidole chake tu!!
Muda utawaumbua zaidi.