John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 712
- 1,240
Tarehe 03/04/2012 wachangiaji kadhaa mmetaka kauli yangu kuhusu matukio yaliyojitokeza Ubungo Mataa, sikutaka kueleza chochote kwenye hatua hiyo mpaka kwanza nikutane na wahusika.
Naomba kuwajulisha kuwa tarehe 04/04/2012 nilifanya mkutano na wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga zaidi ya 500 walioondolewa katika kata ya Ubungo.
Nilianza kwa kuwaeleza wazi kwamba siungi mkono biashara kufanyika katika maeneo hatarishi na maeneo yasiyoruhusiwa kisheria; hata hivyo nimekutana nao kwa kuwa: Mosi; waliniita hivyo nimefika kuwasikiliza kwa kuwa kazi yangu ni kuwakilisha wananchi wote. Pili; kuwaeleza sijaridhika na namna ambavyo serikali imetekeleza zoezi hilo bila kutimiza ahadi zake kwa wafanyabiashara ndogondogo na bila kutushirikisha au walau kutupa taarifa yoyote wakati wowote viongozi wa kuchaguliwa wa eneo husika. Tatu; kukubaliana hatua za pamoja za kuchukua ili kupata mwelekeo muafaka kwa kuzingatia haki, utulivu na fursa kwa waathirika kuendelea na shughuli za kujikimu bila kuwa katika maeneo hatarishi.
Matatizo ya wafanyabiashara ndogondogo katika Jiji na Dar es salaam ni maeneo mengine ya mijini nchini ni ya muda mrefu. Mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni aliahidi kwamba serikali yake ingeyapatia ufumbuzi wa haraka, hata hivyo Oktoba 2006 mwaka mmoja baada ya kuchaguliwa baada ya kushughulikia msingi wa matatizo aliongoza uamuzi wa siasa kanyaboya wa kuwaondoa wafanyabiashara ndogondogo kinyume na alichowaahidi wakati wa uchaguzi.
Maelezo aliyoyatoa Rais Kikwete wakati huo ni kuwa tunawaondoa maeneo yasiyorasmi ili kuwapeleka kwenye maeneo rasmi muweze kupata anuani, mafunzo na mitaji; ahadi ambayo haijatekelezwa kwa ukamilifu.
Mkuu wa Mkoa ametoa kauli sasa kuwa wafanyabiashara walioondolewa Ubungo waende Machinga Complex suala ambalo nalo ni propaganda kanyaboya kwa kuwa anafahamu kuwa eneo hilo lina uwezo wa kubeba wafanyabiashara takribani 4,500 wakati ambapo wafanyabiashara ndogo ndogo katika mkoa wa Dar es salaam walio katika maeneo kinyume cha sheria ni zaidi ya 150,000. Hivyo, Mkuu wa Mkoa anapaswa kuonyesha mfano wa kuwapeleka wafanyabiashara ndogondogo waliombele ya ofisi yake na maeneo jirani katika Machinga Complex, ambao pekee watajaza. Nimewaeleza kwamba kama suala ni kuvutia wafanyabiashara ili soko lizoeleke watekeleze ushauri niliowapa kwenye vikao husika wa kuongeza ruti za daladala kupitia eneo husika watoe likizo ya kodi kwa wafanyabiashara ndogondogo kwa muda maalum katika jengo husika kama inavyofanya kwa wafanyabiashara wakubwa kutoka nje wanapokuja kuwekeza nchini.
Nikawaeleza kwamba nilitarajia serikali iweke mkazo katika kukabiliana na vyanzo vya mgogoro wa muda mrefu katika serikali na wafanyabiashara ndogondogo badala ya kujikita katika kushughulikia matokeo pekee. Wafanyabiashara ndogondogo wajaibuka ghafla katika eneo la Ubungo, walianza taratibu huku serikali ikiwaachia na hata kuwatambua kwa njia mbalimbali; hivyo kuwaondoa lazima kutanguliwa na maandalizi ya maeneo mbadala ya kufanyia biashara.
Aidha, wananchi kufanyia biashara katika maeneo yasiyorasmi ni matokeo ya udhaifu wa muda mrefu wa serikali wa mipango miji na kushindwa kutenga maeneo ya biashara na kuuza kinyemela maeneo machache yaliyotengwa kwa huduma za msingi za kijamii. Hivyo, uamuzi wa kufungua ukurasa mpya kurekebisha hali hiyo lazima uambatane na kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na huduma nyingine za msingi za kijamii.
Serikali ina wajibu huo pamoja na kuwa biashara inaweza kutazamwa kuwa ni suala la mtu binafsi kwa kuwa wanunuzi wa biashara hizo ni wananchi hususani wa kipato cha chini na hali hii ya kuongezeka kwa uchuuji ni sehemu ya athari za kupungua kwa uzalishaji nchini.
Hali ya taifa ya kiuchumi na kijamii ni chimbuko la ongezeko la wafanyabiashara ndogondogo Jijini Dar es salaam, mathalani kasi ndogo ya ukuaji wa ajira hasa katika viwanda na kilimo ikilinganishwa na idadi kubwa ya vijana wanaohitimu shule na vyuo; biashara hizo ni sehemu ya jitihada za vijana wenyewe ‘kujiajiri' hivyo kuwaondoa bila mfumo mbadala ni kuchangia katika umaskini.
Pamoja na hatua zinazopaswa kuchukuliwa na Manispaa ya Kinondoni, Wizara zinazohusika na Wafanyabiashara wenyewe; nimetoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kueleza hatua iliyofikiwa katika kutekeleza ahadi yake ya aliyoitoa tarehe Oktoba 2010 wakati wa kampeni ya kujenga Machinga Complex nyingine tano; ili kuwe na maeneo ya namna hiyo ya biashara mawili kwenye kila manispaa. Kama serikali ingekuwa imetekeleza ahadi hiyo katika kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja toka Rais Kikwete aingie madarakani kungekuwa hivi sasa na eneo la wafanyabiashara ndogondogo zaidi ya elfu saba katika Jimbo la Ubungo. Ahadi hii ingeweza kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja kwa kuwa Rais Kikwete alisema mwenyewe Oktoba 2010 kuwa tayari serikali ilikuwa imepata ufadhili wa bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo. Serikali inayokusanya kodi kwa wananchi wote ikiwemo wafanyabiashara ndogo ndogo inawajibu wa moja kwa moja kushughulikia chanzo cha mgogoro uliodumu kwa muda mrefu kati yake wafanyabiashara hao badala ya matokeo. Serikali inatumia nguvu kubwa kwenye kushughulikia matokeo badala ya vyanzo, kama nguvu hizo hizo zingetumika kushughulikia mafisadi wanaoua viwanda na kukosesha ajira kwa vijana au wanaohujumu ruzuku katika kilimo nchi ingepiga hatua kwa haraka zaidi. Hivyo, kusimamia utawala wa sheria kusiishie kwa wafanyabiashara ndogondogo bali nguvu kubwa hiyo itumike pia kuwaondoa katika maeneo yasiyoruhusiwa wafanyabiashara wakubwa ambao wengine wamepora viwanja vya wazi vya umma na wengine wamevamia maeneo ya hifadhi ya barabara.
Naomba kuwajulisha kuwa tarehe 04/04/2012 nilifanya mkutano na wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga zaidi ya 500 walioondolewa katika kata ya Ubungo.
Nilianza kwa kuwaeleza wazi kwamba siungi mkono biashara kufanyika katika maeneo hatarishi na maeneo yasiyoruhusiwa kisheria; hata hivyo nimekutana nao kwa kuwa: Mosi; waliniita hivyo nimefika kuwasikiliza kwa kuwa kazi yangu ni kuwakilisha wananchi wote. Pili; kuwaeleza sijaridhika na namna ambavyo serikali imetekeleza zoezi hilo bila kutimiza ahadi zake kwa wafanyabiashara ndogondogo na bila kutushirikisha au walau kutupa taarifa yoyote wakati wowote viongozi wa kuchaguliwa wa eneo husika. Tatu; kukubaliana hatua za pamoja za kuchukua ili kupata mwelekeo muafaka kwa kuzingatia haki, utulivu na fursa kwa waathirika kuendelea na shughuli za kujikimu bila kuwa katika maeneo hatarishi.
Matatizo ya wafanyabiashara ndogondogo katika Jiji na Dar es salaam ni maeneo mengine ya mijini nchini ni ya muda mrefu. Mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni aliahidi kwamba serikali yake ingeyapatia ufumbuzi wa haraka, hata hivyo Oktoba 2006 mwaka mmoja baada ya kuchaguliwa baada ya kushughulikia msingi wa matatizo aliongoza uamuzi wa siasa kanyaboya wa kuwaondoa wafanyabiashara ndogondogo kinyume na alichowaahidi wakati wa uchaguzi.
Maelezo aliyoyatoa Rais Kikwete wakati huo ni kuwa tunawaondoa maeneo yasiyorasmi ili kuwapeleka kwenye maeneo rasmi muweze kupata anuani, mafunzo na mitaji; ahadi ambayo haijatekelezwa kwa ukamilifu.
Mkuu wa Mkoa ametoa kauli sasa kuwa wafanyabiashara walioondolewa Ubungo waende Machinga Complex suala ambalo nalo ni propaganda kanyaboya kwa kuwa anafahamu kuwa eneo hilo lina uwezo wa kubeba wafanyabiashara takribani 4,500 wakati ambapo wafanyabiashara ndogo ndogo katika mkoa wa Dar es salaam walio katika maeneo kinyume cha sheria ni zaidi ya 150,000. Hivyo, Mkuu wa Mkoa anapaswa kuonyesha mfano wa kuwapeleka wafanyabiashara ndogondogo waliombele ya ofisi yake na maeneo jirani katika Machinga Complex, ambao pekee watajaza. Nimewaeleza kwamba kama suala ni kuvutia wafanyabiashara ili soko lizoeleke watekeleze ushauri niliowapa kwenye vikao husika wa kuongeza ruti za daladala kupitia eneo husika watoe likizo ya kodi kwa wafanyabiashara ndogondogo kwa muda maalum katika jengo husika kama inavyofanya kwa wafanyabiashara wakubwa kutoka nje wanapokuja kuwekeza nchini.
Nikawaeleza kwamba nilitarajia serikali iweke mkazo katika kukabiliana na vyanzo vya mgogoro wa muda mrefu katika serikali na wafanyabiashara ndogondogo badala ya kujikita katika kushughulikia matokeo pekee. Wafanyabiashara ndogondogo wajaibuka ghafla katika eneo la Ubungo, walianza taratibu huku serikali ikiwaachia na hata kuwatambua kwa njia mbalimbali; hivyo kuwaondoa lazima kutanguliwa na maandalizi ya maeneo mbadala ya kufanyia biashara.
Aidha, wananchi kufanyia biashara katika maeneo yasiyorasmi ni matokeo ya udhaifu wa muda mrefu wa serikali wa mipango miji na kushindwa kutenga maeneo ya biashara na kuuza kinyemela maeneo machache yaliyotengwa kwa huduma za msingi za kijamii. Hivyo, uamuzi wa kufungua ukurasa mpya kurekebisha hali hiyo lazima uambatane na kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na huduma nyingine za msingi za kijamii.
Serikali ina wajibu huo pamoja na kuwa biashara inaweza kutazamwa kuwa ni suala la mtu binafsi kwa kuwa wanunuzi wa biashara hizo ni wananchi hususani wa kipato cha chini na hali hii ya kuongezeka kwa uchuuji ni sehemu ya athari za kupungua kwa uzalishaji nchini.
Hali ya taifa ya kiuchumi na kijamii ni chimbuko la ongezeko la wafanyabiashara ndogondogo Jijini Dar es salaam, mathalani kasi ndogo ya ukuaji wa ajira hasa katika viwanda na kilimo ikilinganishwa na idadi kubwa ya vijana wanaohitimu shule na vyuo; biashara hizo ni sehemu ya jitihada za vijana wenyewe ‘kujiajiri' hivyo kuwaondoa bila mfumo mbadala ni kuchangia katika umaskini.
Pamoja na hatua zinazopaswa kuchukuliwa na Manispaa ya Kinondoni, Wizara zinazohusika na Wafanyabiashara wenyewe; nimetoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kueleza hatua iliyofikiwa katika kutekeleza ahadi yake ya aliyoitoa tarehe Oktoba 2010 wakati wa kampeni ya kujenga Machinga Complex nyingine tano; ili kuwe na maeneo ya namna hiyo ya biashara mawili kwenye kila manispaa. Kama serikali ingekuwa imetekeleza ahadi hiyo katika kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja toka Rais Kikwete aingie madarakani kungekuwa hivi sasa na eneo la wafanyabiashara ndogondogo zaidi ya elfu saba katika Jimbo la Ubungo. Ahadi hii ingeweza kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja kwa kuwa Rais Kikwete alisema mwenyewe Oktoba 2010 kuwa tayari serikali ilikuwa imepata ufadhili wa bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo. Serikali inayokusanya kodi kwa wananchi wote ikiwemo wafanyabiashara ndogo ndogo inawajibu wa moja kwa moja kushughulikia chanzo cha mgogoro uliodumu kwa muda mrefu kati yake wafanyabiashara hao badala ya matokeo. Serikali inatumia nguvu kubwa kwenye kushughulikia matokeo badala ya vyanzo, kama nguvu hizo hizo zingetumika kushughulikia mafisadi wanaoua viwanda na kukosesha ajira kwa vijana au wanaohujumu ruzuku katika kilimo nchi ingepiga hatua kwa haraka zaidi. Hivyo, kusimamia utawala wa sheria kusiishie kwa wafanyabiashara ndogondogo bali nguvu kubwa hiyo itumike pia kuwaondoa katika maeneo yasiyoruhusiwa wafanyabiashara wakubwa ambao wengine wamepora viwanja vya wazi vya umma na wengine wamevamia maeneo ya hifadhi ya barabara.