Kikwete atekeleze ahadi zake za serikali kutenga maeneo mbadala ya wamachinga kufanya biashara

Tatizo la ajira nchi hii litatuandama hadi tutakapokuwa na viongozi wenye mtazamo hasi juu ya ukosefu wa ajira. Hapa Tanzania watawala wanaamini kuwa tatizo la ajira litatatuliwa na wazungu kupitia njia ya uwekezaji, yaani wakileta mitaji yao hapa nchini. Kwa nchi ambayo ina inflation ya 20% katika uchumi unaokuwa kwa 7% utawapata wawekezaji matapeli kama wa Dowans. Hata ukienda Marekani na nchi yoyote iliyoendelea the biggest employer is SMALL BUSINESSES. Wenye Salon, Mashine za kuchomelea, viduka vidogo, migahawa, mama Lishe nk ndio sehemu kubwa ya ajira inakotokea hata katika uchumi ulioendelea. Kinachotakiwa ni serikali kuzisimamia vizuri na kuzisajili hizi biashara ndogo ndogo ili ziende katika mfumo ulio rasmi na zilipe kodi. Dalili kubwa kabisa ya uchumi wa hovyo hovyo na ukosefu wa ajira duniani ni uwingi wa wachuuzi au machinga. Kama ulivyosema Mh Mnyika, na nashukuru kuwa umekuwa kiongozi wa kwanza Tanzania kulizungumzia hadharani na kuweka ukweli bila kujali kama unauma, tatizo la ajira ni kubwa kuliko wanasiasa wanavyolizungumzia na hakuna hata mtu mmoja atakuja kifua mbele kutuambia ana takwimu sahihi za tatizo la ajira. Utazipataje kama hata vitambulisho vya utaifa hakuna, hakuna hata national database ya ajira...
 
Abdulhalim
umenifurahisha sana, sasa hao wafanyabiashara wadogo wadogo unataka wasubili long term plan!!!! navyojua mimi kwenye malengo kuna short term na long term plan, sasa mtu analala njaa leo unamwambia nina mpango mzuri juu yako subiri baada ya mwaka au miaka 4. njaa ya leo inabidi itatulike leo hata kama ni kwa kupiga debe. Mnyika pambana leo pia jitahidi upambane kesho.
Mimi najua kunawafanya biashara pale wanajua kuhesabu pesa tuu kwa sababu hata kusoma hawajui, unawasaidiaje hao au ndiyo unawapelea elimu ya watu wazima wakasome waache familia inakufaa njaa.


Tuombe Mungu atusaidie tuvuke na hapa
Labda ndugu wewe useme hao machinga wapelekwe wapi. Long-term plans ndio mpango mzima hakuna short-cut kuelekea maendeleo ya kweli, hizi short-term solutions za kupeleka watu huku na huko zilikuepo toka zamani na hakuna mafanikio yeyote zaidi ya watu zaidi kuingia kwene biashara hizi zisizo rasmi na waliohamishwa kurudi tena kulekule walikokuepo. Mtu mwenyewe binafsi kabla ya kuingia kuweka biashara kwene hifadhi ya barabara au sehemu isiyoruhusiwa umeamua mwenyewe kuchukua risk, ni sawa na mimi leo nijitokee zangu nivamie kile kiwanja chako cha kule Mbezi Beach nianze kujenga kibanda cha kuishi, siku ukija mwenyewe kuchukua chako sina haki tena ya kudai eti unipe short-term solution ya makazi maana unayo hata haki ya kunishtaki kwa kuvamia eneo lako! nikianza sarakasi za kukudai fidia ndio hapo nitaonekana kichaa zaidi. Lazima watu wawe responsible na options wanazochukua, unapoamua kuinvest kwene premises isio yako au ambayo inakiuka utaratibu, be prepared for your own short-term solutions.
 
Mkuu Kituko!

Hayo mnayoyaeleza mbona Mnyika kayazungumzia kwenye thread?
Abdul kaja moja kwa moja na matusi kwa Mnyika utafikiri alimpania huku akisahau anachoeleza ni upande wa pili wa hoja ya Mnyika!

Machinga ni waathirika wa mfumo kama jamii lazima kuwe na ufumbuzi wa immediate problems hyo haimaanishi hamna long-term plans!

Machinga wanaenda na soko, hii ni nchi ya kichuuzi saiv chochote sokoni twende ndio tulichoambulia toka kwenye sera za utandawazi, sasa leo hii kuja kuwalaani Machinga nadhani itabidi tufikirie nani wa kupimwa akili hapa!

Ndio maana nkasema tuwe na utaratibu wa kusoma katikati ya mistari, Mnyika kaeleza vitu vingi kwa pande zote!
Weka wazi tu kuwa wewe ni ass-kisser na una kichwa kigumu kama nazi. Mimi nazungumzia wapinzani waibane Serikali ktk mambo ya msingi ambapo ni kuwa na mipango ya muda mrefu kuondoa tatizo la ajira na kukuza uchumi, Mnyika anaongelea Rais atimize ahadi za kuwahamisha machinga, kana kwamba huo ndio muarobaini..sadly wewe unaona this is the same argument na eti unasema ninatukana! pole sana, maana wahenga walisema, ni bora usieleweke kuliko kutowaelewa wengine.
 
safii sana jouneGwalu waambie hao wasioelewa hata wakieleweshwa! Mie nimemwelewa sana kamanda Mnyika, ila kutokana na ulimbukeni na umaskini wa fikra wa wengi wetu tunatarajia mabadiliko bila mikakati! Tunafikiri kuanzisha sera kama za kufufua viwanda ni rahisi?, leo hii Tz hatuna viwanda vingi lakini umeme unatutosha? Na kama haututoshi?, viwanda vikiwepo itakuaje kwenye suala la umeme? Na je wabunge hasa makamanda wetu hawapigi kelele kuhusu hilo la umeme bungeni?
Je serikali imechukua hatua stahiki? Jamani tuache kua maskini wa fikra! Watanzania tunashindwa kuwa na fikra za mbali, watu tunahongwa ili tuiangamize Tz yetu na tunakubali, je kwenye umeme tutaweza kua punctual hasa hao mawaziri?
Tuangalie hata sector ya maliasili na utalii watu wakajiuzia wanyama wetu na wakajulikana, jiulize walichukuliwa hatua zozote?
Tz tuna madini je tunayafaidi ili angalau ktk kufaidi kwake kutengeneze ajira!?
Chukulia kwenye ujenzi wa barabara, je makandarasi ni watz?, kama sio hatuna watz wenye uwezo wa kua makandarasi?
Tusiwe maskini wa fikra ila ni lazima tuwe na huduma ya kwanza kwa mgonywa na sio kumtelekeza mgonywa mpaka azidiwe ndio tumpe huduma!
 
safii sana jouneGwalu waambie hao wasioelewa hata wakieleweshwa! Mie nimemwelewa sana kamanda Mnyika, ila kutokana na ulimbukeni na umaskini wa fikra wa wengi wetu tunatarajia mabadiliko bila mikakati! Tunafikiri kuanzisha sera kama za kufufua viwanda ni rahisi?, leo hii Tz hatuna viwanda vingi lakini umeme unatutosha? Na kama haututoshi?, viwanda vikiwepo itakuaje kwenye suala la umeme? Na je wabunge hasa makamanda wetu hawapigi kelele kuhusu hilo la umeme bungeni?Je serikali imechukua hatua stahiki? Jamani tuache kua maskini wa fikra! Watanzania tunashindwa kuwa na fikra za mbali, watu tunahongwa ili tuiangamize Tz yetu na tunakubali, je kwenye umeme tutaweza kua punctual hasa hao mawaziri?Tuangalie hata sector ya maliasili na utalii watu wakajiuzia wanyama wetu na wakajulikana, jiulize walichukuliwa hatua zozote?Tz tuna madini je tunayafaidi ili angalau ktk kufaidi kwake kutengeneze ajira!? Chukulia kwenye ujenzi wa barabara, je makandarasi ni watz?, kama sio hatuna watz wenye uwezo wa kua makandarasi? Tusiwe maskini wa fikra ila ni lazima tuwe na huduma ya kwanza kwa mgonywa na sio kumtelekeza mgonywa mpaka azidiwe ndio tumpe huduma!
wewe ni mrithi mwingine wa shehe yahaya, unajua kipi naelewa kipi sielewi. Kumwelewa Mnyika na kukubaliana na Mnyika ni vitu 2 tofauti, lakini wewe kwa sababu ni grupi mwingine au uelewa finyu wa kupembua, u can't tell the difference. Nachelea hata kurespond zaidi maana ni sawa na kuongea na ukuta.
 
Tukishawahamisha hao, wakija wamachinga wapya inakuwaje?

GT Gaijin,
wanasiasa hawawezi kuliona hilo, imagine pale Machinga Complex hakuna hata machinga mmoja anaeweza kupangisha pale, kodi ni kubwa kulinganisha na mtaji wa huyo mmachinga aliyekusudiwa na ukipita utawakuta wamepanga vitu vyao nje,

Solution inayotakiwa sio ya kuwatafutia eneo la kuwaweka, maana kila siku wanakuja mjini na wala hapatawatosha huko wanakuotaka kuwaweka,

Tatizo la Tanzania kila kitu kinachukuliwa kisiasa, hilo sio jambo la siasa tena, ni la kiserikali kufanya uamuzi wa kutafuta shina la tatizo na kulitatua na wala sio solution ya zima moto (ya kuwatafutia eneo)

Serikali lazima ijiulize kwa nini watu wanatoka vijijini na kukimbilia mjini bila kuwa na misimamo wala cha kufanya?
 
Back
Top Bottom