Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Kuhusu uwanja wa ndege, Kikwete alisema utajengwa Serengeti ili wageni waweze kutua.
"Tuliahidi na tutajenga uwanja wa ndege ili wageni waweze kutua hapa," alisema Kikwete bila kufafanua ujenzi huo utaanza lini.
Ni dhahiri kuwa huo uwanja wa ndege sio kwa manufaa ya wanaserengeti!! Wageni ndio muhimu na ndio maana wanajengewa uwanja.
Wakazi wa Serengeti wanahitaji barabara za lami: Mugumu-Musoma, Mugumu-Bunda, Mugumu-Tarime & Mugumu-Arusha.
Zaidi ya barabara, mugumu wanahitaji huduma za maji na umeme kusambazwa vijijini, tofauti na sasa ambapo huduma za maji ya bomba na umeme vinapatikana mugumu mjini tu.
Kwa hali hii ccm isitarajie ushindi Serengeti mwaka huu, wanaserengeti tutawaonyesha tundu la kutokea kuanzia urais, ubunge hadi madiwani.