Msema hovyo
Senior Member
- Jul 3, 2011
- 195
- 86
Taarifa za ndani, zinapasha kwamba katika harakati za uchaguzi wa Rais za mwaka 2005, Kikwete alijiandaa kuhamia CHADEMA iwapo NEC ya CCM isingempitisha kugombea Urais. Na inasemekana kwamba mkakati kabambe ulishaandaliwa na mafisadi wa CCM (Rostam na Lowassa) kuhakikisha kwamba Kikwete anashinda Urais kupitia CHADEMA. Mkapa alinusa hilo, ndiyo maana aliamua kumuacha Kikwete apite hata kama target yake ilikuwa ni Salim A Salim
Inasemekana pia, kwamba Mheshimiwa Mbowe alikuwa well informed kuhusu hilo, na alikuwa anasubiri tu maamuzi ya NEC ya CCM, ndipo aamue nani awe mgombea Urais kupitia CHADEMA. Kwa taarifa za ndani, ni kwamba baada ya Rostam kujiuzulu, mafisadi wengine pia kama Lowassa na Chenge watajiuzulu, na watajitahidi kutumia vyombo vya habari na pesa kujisafisha kutoka sasa hadi hapo 2014 ambapo watahamia rasmi CHADEMA. Maamuzi ya ama kuwa CHADEMA au chama kingine yatategemea pia mtizamo wa akina Mbowe na Slaa ambao wanaonekana kuwa ni threat kwa hao mapacha watatu.
Binafsi ninaungana na Lowassa kuhamia CHADEMA, nina imani kwa kufanya hivyo atawezesha upinzani kushika dola kama ambavyo aliamini angemuwezesha Kikwete kushika dola kupitia CHADEMA. Tena kwa kuwa atakuwa ana kisilani na CCM Lowassa akiingia madarakani kupitia CHADEMA atahakikisha anawashughulikia wale wafujaji wa mali za umma wote waliopo CCM akiwemo na Kikwete, na kujitahidi kufanya vema zaidi katika uongozi wake ili kuwaonyesha CCM kwamba yeye si kama wao.
Zaidi ya yote mimi ninamuona Lowassa kama ni strong leader, akishika nafasi ya Urais atafanya vema. Nawaombeni CHADEMA mpokeeni Lowassa.
Lakini msiniulize source, sawa!!?
Nawasilisha.
Inasemekana pia, kwamba Mheshimiwa Mbowe alikuwa well informed kuhusu hilo, na alikuwa anasubiri tu maamuzi ya NEC ya CCM, ndipo aamue nani awe mgombea Urais kupitia CHADEMA. Kwa taarifa za ndani, ni kwamba baada ya Rostam kujiuzulu, mafisadi wengine pia kama Lowassa na Chenge watajiuzulu, na watajitahidi kutumia vyombo vya habari na pesa kujisafisha kutoka sasa hadi hapo 2014 ambapo watahamia rasmi CHADEMA. Maamuzi ya ama kuwa CHADEMA au chama kingine yatategemea pia mtizamo wa akina Mbowe na Slaa ambao wanaonekana kuwa ni threat kwa hao mapacha watatu.
Binafsi ninaungana na Lowassa kuhamia CHADEMA, nina imani kwa kufanya hivyo atawezesha upinzani kushika dola kama ambavyo aliamini angemuwezesha Kikwete kushika dola kupitia CHADEMA. Tena kwa kuwa atakuwa ana kisilani na CCM Lowassa akiingia madarakani kupitia CHADEMA atahakikisha anawashughulikia wale wafujaji wa mali za umma wote waliopo CCM akiwemo na Kikwete, na kujitahidi kufanya vema zaidi katika uongozi wake ili kuwaonyesha CCM kwamba yeye si kama wao.
Zaidi ya yote mimi ninamuona Lowassa kama ni strong leader, akishika nafasi ya Urais atafanya vema. Nawaombeni CHADEMA mpokeeni Lowassa.
Lakini msiniulize source, sawa!!?
Nawasilisha.