Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
RAIS Jakaya Kikwete amesema, hivi karibuni alibatilisha hukumu 75 za vifo kuwa vifungo vya maisha.
Mbali na kubatilisha huko amesema licha ya Tanzania kuwa na sheria ya Kunyonga katika vitabu vya nchini, kwa muda mrefu haijanyonga mtu.
Rais Kikwete alisema hayo juzi wakati wa chakula cha usiku katika makao makuu ya Jumuiya ya Kilei ya Kanisa Katoliki Duniani la Mtakatifu Eggidio, mjini Rome, Italia.
Ujumbe huo wa Mtakatifu Eggidio uliongozwa na mwanzilishi wa Jumuia hiyo, profesa wa historia katika chuo kikuu cha Rome, Profesa Andrea Riccardi na msaidizi wake wa kiroho, Padre Matteo Zuppi.
Hili ni jambo lililoulizwa na Kamati ya Jaji Nyalali. Watu walikataa kufutwa kwa adhabu ya kifo. Majuzi nilibatilisha kiasi cha hukumu 75 za vifo kuwa vifungo vya maisha. Lakini bado waliohukumiwa kifo kwenye magereza yetu ni wengi, pengine kufikia watu 200, hata kama sijahesabu.
Rais Kikwete alisema hapa nchini bado idadi kubwa ya watu wanapinga kufutwa kwa adhabu ya kifo na wanataka adhabu hiyo iendelea kuwapo katika vitabu vya sheria.
Akizungumzia mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yaani albino, alisema mbali na kuonekana mauaji ya kusikitisha lakini ni mauaji ya kijinga kutokea katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia ambayo yameliaibisha taifa la Tanzania.
Kwamba watu wanaweza kuwa wajinga kuamini kuwa ukipata kidole cha albino utatajirika ni jambo gumu sana kuamini katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia. Lakini napenda kuwahakikisheni kuwa sasa Serikali imeyathibiti mauaji haya, alisema Rais Kikwete na kuongeza:
Tuliendesha kura ya maoni. Watu wengi wametiwa mbaroni na wengine wako mahakamani. Kati yao wengine wamehukumiwa kunyongwa,
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=4448
Mbali na kubatilisha huko amesema licha ya Tanzania kuwa na sheria ya Kunyonga katika vitabu vya nchini, kwa muda mrefu haijanyonga mtu.
Rais Kikwete alisema hayo juzi wakati wa chakula cha usiku katika makao makuu ya Jumuiya ya Kilei ya Kanisa Katoliki Duniani la Mtakatifu Eggidio, mjini Rome, Italia.
Ujumbe huo wa Mtakatifu Eggidio uliongozwa na mwanzilishi wa Jumuia hiyo, profesa wa historia katika chuo kikuu cha Rome, Profesa Andrea Riccardi na msaidizi wake wa kiroho, Padre Matteo Zuppi.
Hili ni jambo lililoulizwa na Kamati ya Jaji Nyalali. Watu walikataa kufutwa kwa adhabu ya kifo. Majuzi nilibatilisha kiasi cha hukumu 75 za vifo kuwa vifungo vya maisha. Lakini bado waliohukumiwa kifo kwenye magereza yetu ni wengi, pengine kufikia watu 200, hata kama sijahesabu.
Rais Kikwete alisema hapa nchini bado idadi kubwa ya watu wanapinga kufutwa kwa adhabu ya kifo na wanataka adhabu hiyo iendelea kuwapo katika vitabu vya sheria.
Akizungumzia mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yaani albino, alisema mbali na kuonekana mauaji ya kusikitisha lakini ni mauaji ya kijinga kutokea katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia ambayo yameliaibisha taifa la Tanzania.
Kwamba watu wanaweza kuwa wajinga kuamini kuwa ukipata kidole cha albino utatajirika ni jambo gumu sana kuamini katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia. Lakini napenda kuwahakikisheni kuwa sasa Serikali imeyathibiti mauaji haya, alisema Rais Kikwete na kuongeza:
Tuliendesha kura ya maoni. Watu wengi wametiwa mbaroni na wengine wako mahakamani. Kati yao wengine wamehukumiwa kunyongwa,
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=4448