Kikao cha dharura cha CCM mchana huu

Kikao cha dharura cha CCM mchana huu

Iwapo watatishwa, watajipambanua wapigania haki na wapigania ufisadi. Na hilo ndiyo uangamivu wao. Si mnasikia Sengerema nako diwani kaachia ngazi? Tunasubi wamalize bunge wengine wajitoe kwa wingi

Diwani gani tena huyo wa Sengerema aliyeachia ngazi?nanmba unijuze maana sijaipata hiyo.
 
Halafu wanakiburi, majeuri...
wanaona wabunge wanapoteza muda tu
Mungu aendelelee kuwafungua macho wabunge wa CCM waungane na wenzao wawatoe viburi vyote viwaishe na iwe fundisho.
ebo!
 
kuna thread nyingine inaendeelea na habari za awali ni kuwa fili kawataja wazi na wengine amesema anaendelea kukusanya ushahidi
 
Mwisho wao umefika...mfa maji haishi kutapatapa
 
Ina maana bunge halijarejea jioni hii??
Hao wabunge 'mafisi' bado wapo kikaoni?

Tatizo la CCM na wabunge wake na serikali yake :blabla::blabla::blabla::blabla::blabla::blabla: mingi sana!!
 
Wabunge wameamua kuleta mabadiliko ya fikra wakiwa humo humo ccm,hakuna kupozwa wala kunyamazishwa.

Ndugu yangu, watu hao mbona wanawezekana kabisa kunyamazishwa? Ukikubali kuwa humo ni lazima pia ukubali kuweka rehani akili zako. Kama unabisha subiri uone.
 
Mbowe anaongea sasa bungeni na anaponda kwa nini Ccm wameleta mawaziri wawaili tu katika kikao cha jioni hii.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
 
Ndugu yangu, watu hao mbona wanawezekana kabisa kunyamazishwa? Ukikubali kuwa humo ni lazima pia ukubali kuweka rehani akili zako. Kama unabisha subiri uone.

Mkuu Komeo uko sahihi. Angalia maneno ya Alphonce Mawazo.

"Nataka kusema kuwa hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya CCM ambaye ana dhamira ya kweli ya kuwasaidia Watanzania na badala yake viongozi wengi wamekuwa wakijinufaisha wenyewe" Alphonce Mawazo, Diwani aliye achia ngazi Arusha.
 
ccm ishakua kama choo cha pale kituo cha polisi msimbazi cdhan kama mtu uliyetimamu unaweza kustahimili kukaa kwa muda mref.
 
Hizo ni janja tu wanajf hawajui wanapoamkia cc tulishapita siku nyingi! Hata wakimnyamazisha tundu, lema na wengine wote mawe yatanena kweupe kwa nguvu ya mungu. Na hakika mungu kama yupo hai kweli ccm wakajenge ughaibuni kambi yao!
 
tuache kelele ktk mitandao ya kijamii

twendeni viwanjani kwa wananchi huko ndiko kwenye uhalisia na tufanye kazi ya kuleta mabadiliko kwa kuwadunga wananchi sindano ya mabadiliko,dozi ya mabadiliko,dawa ya mabadiliko

tuwafanye wananchi waelewe hata kile wasichokielewa sasa,tuwasaidie kupambaua kwa lugha rahisi na mwisho tuwaache bila kuwalazimisha wafanye maamuzi

Well put boss!! Hizi fikra za humu wakishushiwa wananchi, hata 2015 ni mbali!!
 
mmmh wameona mambo hayaendi wanataka kujipanga wakati ni asubuhi usiku mzima wamelala wanakumbuka shuka asubuhi!!
 
if symptoms persist seek medical advise.....rule no 1
shake before to use.........................rule no 2

wanaenda kumsulubu fullkunjombe
over

na filikunjombe ataibuka kidedea!!! Na atasomba wengi!!! Na pengine ndio waziri mkuu mpya wachape kazi bega kwa bega na zitto kabwe!hizi ndio positive politics!
 
Back
Top Bottom